Wimbo 66
Nguvu za Fadhili
1. Tushukuru Mungu sana,
Awafadhilia
Wale wasiostahili,
Wakristo twajua.
Ajapokuwa mukuu
Anazo busara nyingi.
Fadhilize zatuvuta
Kwake na imani.
2. Yesu kweli alifunza.
Kwa ’tulivu, ’pole,
Fadhili alitumia
Kwa walio chini,
Mafundisho ya upendo
Yaliburudisha nafsi,
Wadhambi wakaamini
Mungu kwa mioyo.
3. Neno la Mungu lasema
Tulizae tunda.
Tuwe kama Mungu, Yesu,
Na tubarikiwe.
Tukiwa na matatizo,
Tutayatatua kama
Tukiwa nao upole,
Tena na fadhili.
4. Tutawafaidi watu
Tunapothamini
Fadhili ni zenye kani
Idumuyo, kubwa!
Wapaji wana baraka,
Sio wapokeao tu.
Fadhili zasifu Mungu,
Mupaji uzima.