-
Siku za MwishoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mtu Akisema—
‘Hali si mbaya sana leo; sikuzote kumekuwako vita, njaa, matetemeko ya nchi, uhalifu’
Unaweza kujibu hivi: ‘Naelewa maoni yako. Tumezaliwa katika ulimwengu ambamo hayo ni mambo ya kawaida. Lakini wanahistoria wanaeleza kwamba kuna jambo fulani lililo tofauti kabisa kuhusu karne ya 20. (Soma manukuu katika ukurasa wa 289, 290.)’
Au unaweza kusema: ‘Kuwako kwa vita, njaa, matetemeko ya nchi, na uhalifu silo jambo la maana. Je, unajua kwamba ishara ambayo Yesu alitoa ina sehemu nyingi?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Yeye hakusema kwamba tukio moja tu lingethibitisha kwamba tumo katika “siku za mwisho.” Lakini ishara yote nzima inapoonekana, hilo ni jambo la maana—na hasa inapoonekana duniani pote na kuanzia mwaka uliowekwa na orodha ya matukio ya Biblia.’ (Ona ukurasa wa 284-289, pia ukurasa wa 397-399.)
‘Unajuaje kama wakati ujao ishara hiyo haitatimia kuliko inavyotimia leo?’
Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni swali zuri, na jibu lake linakazia kwamba tunaishi katika “siku za mwisho.” Jinsi gani? Sehemu ya ile ishara iliyotolewa na Yesu inahusu vita kati ya mataifa na falme. Lakini ingekuwaje leo ikiwa lazima vita vingine vikubwa vitokee kati ya mataifa makubwa ili ishara hiyo itimizwe? Ikiwa watu wowote wangeokoka vita hivyo, wangekuwa wachache sana. Kwa hiyo, kusudi la Mungu la kwamba watu waokoke laonyesha kwamba sasa tuko karibu sana na mwisho wa mfumo huu wa kale.’
Au unaweza kusema: ‘Kupatanisha matukio ya ulimwengu na unabii huu ni kama kupatanisha alama za vidole na mtu mwenyewe. Mtu mwingine hawezi kuwa na alama hizohizo. Vivyo hivyo, matukio yaliyoanza katika mwaka wa 1914 hayatarudiwa wakati fulani ujao.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Kila sehemu ya ishara hiyo inaonekana waziwazi.’ (2) ‘Kwa kweli, hatutaki kuwa kama watu wa siku za Noa. (Mt. 24:37-39)’
‘Mwisho hautakuja tukiwa hai’
Unaweza kujibu hivi: ‘Lakini unaamini kwamba Mungu atachukua hatua wakati fulani, sivyo?’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Yeyote kati yetu anaweza kujua wakati ambapo mwisho utakuja ikiwa tu Mungu angetupatia habari hiyo. Yesu alieleza waziwazi kwamba hakuna mtu anayejua siku wala saa, lakini alisimulia kikamili mambo ambayo yangetukia wakati ambapo ungekuja.’ (2) ‘Masimulizi hayo yanahusu matukio ambayo wewe binafsi umejionea. (Ikiwezekana, zungumzia mambo mbalimbali yanayohusu ile ishara, ukitumia mambo yaliyo katika kurasa zinazotangulia.)’
‘Wakati ujao haunihangaishi’
Unaweza kujibu hivi: ‘Kwa hakika ni vizuri kutohangaikia kupita kiasi wakati ujao. Lakini sisi sote hujaribu kupanga maisha zetu ili kujilinda sisi wenyewe na wapendwa wetu. Ni muhimu kufanya mipango mizuri. Biblia inaonyesha kwamba tunatazamia mambo mazuri wakati ujao, na ni jambo la hekima kufanya mpango ili tunufaike nayo. (Met. 1:33; 2 Pet. 3:13)’
‘Mimi siyafikirii sana mambo hayo mabaya; napenda kuwa na maoni mazuri kuhusu wakati ujao’
Unaweza kujibu hivi: ‘Yesu alisema kwamba wafuasi wake wangekuwa na sababu nzuri ya kutazamia mambo mazuri katika wakati wetu. (Luka 21:31)’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Lakini ona kwamba hawaambii wapuuze mambo yanayotukia ulimwenguni na kuwa wenye furaha. Anasema kwamba matazamio yao mazuri yangekuwa na msingi mzuri, kwa sababu wanaelewa maana ya matukio ya ulimwengu na wanajua matokeo yatakuwa nini.’
-
-
Tafsiri ya Ulimwengu MpyaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
Maana: Tafsiri ya Maandiko Matakatifu iliyotafsiriwa na halmashauri ya mashahidi watiwa-mafuta wa Yehova. Biblia hii ilitafsiriwa katika Kiingereza cha kisasa moja kwa moja kutoka lugha za Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki. Watafsiri hao walisema hivi kuhusu kazi yao: “Watafsiri wa kitabu hiki, ambao wanamwogopa na kumpenda Mungu aliye Mtungaji wa Maandiko Matakatifu, wanatambua kwamba wana wajibu wa pekee kwake wa kupitisha mawazo na matangazo yake kwa usahihi kadiri inavyowezekana.
-