Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi
    Huduma ya Ufalme—1994 | Desemba
    • Alika Wengine Wamfuate Yule Mtu Mkuu Zaidi

      1 Kama ilivyorekodiwa kwenye Mathayo 5:14, Yesu aliambia wanafunzi wake: “Ninyi ni nuru ya ulimwengu.” Wafuasi wa Yesu walikuwa waambie watu kila mahali kuhusu Ufalme wa Yehova na uandalizi Wake wenye upendo wa wokovu kupitia Yesu. Tukiwa na agizo hilo akilini, wakati wa mwezi wa Desemba twatazamia kwa hamu kutoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Hapa pana madokezo ambayo huenda ukataka kuyatumia.

      2 Baada ya kujijulisha, unaweza kusema yafuatayo kwa maneno yako mwenyewe:

      ◼ “Wengi wamejiuliza Yesu alikuwa mtu wa aina gani alipokuwa duniani. Wewe unafikiri ni katika njia zipi alikuwa tofauti na wengine? [Ruhusu jibu] Kitabu hiki chenye kusisimua, Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi, chasimulia mambo makuu ya maisha na huduma yake, nacho huandaa uelewevu wa ndani kuhusu aina ya mtu aliyokuwa. Baada ya kukisoma, watu fulani huhisi kana kwamba walipata kuwa na fursa ya kushiriki naye kibinafsi, kushiriki mateso yake, na kuangalia huduma yake moja kwa moja.” Elekeza kwenye kielezi cha kwanza katika kitabu, ambacho hukazia kichwa. Kisha fungua kwenye utangulizi, na usome fungu la pili chini ya kichwa kidogo “Faidika kwa Kujifunza Juu Yake.” Itikio likiwa zuri, toa kitabu.

      3 Au unaweza kusema jambo kama hili:

      ◼ “Wakati wa majira haya watu wanamfikiria Yesu. Hata hivyo, kwa sababu mambo mengi sana mabaya yanatokea ulimwenguni pote, wengine huenda wakajiuliza ikiwa kweli Yesu anatujali. Wewe wahisije kuhusu hilo?” Ruhusu jibu. Fungua sura ya 24 ya kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na uzungumzie kifupi sababu ya Yesu kuja duniani. Kisha soma Yohana 15:13, ukikazia upendo wa Yesu kwa wengine wa kuhisiwa moyoni. Kumbuka kuwa na magazeti ya karibuni zaidi, broshua, au trakti inayofaa ili uitoe ikiwa kitabu hakikubaliwi.

      4 Hapa pana dokezo jingine:

      ◼ “Vijana walio wengi wanatafuta watu wenye vielelezo vya kuigwa, lakini ni vigumu kuwapata. Yesu Kristo aliweka kielelezo kikamilifu kwa kila mtu. [Soma 1 Petro 2:21.] Maisha yake yote yalikazia ibada ya Baba yake wa kimbingu. Unafikiri ingekuwaje ikiwa watu wengi zaidi wangejaribu kumwiga yeye?” Ruhusu jibu. Rejezea fungu la tatu kwenye kabla ya ukurasa wa mwisho wa kitabu, ambalo laeleza sifa zake za kipekee. Eleza jinsi kitabu Mtu Mkuu Zaidi kinavyoweza kutusaidia sote tuwe Wakristo bora.

      5 Huenda ukataka kutumia jambo kama hili:

      ◼ “Mtu anapotaja Yesu Kristo, watu wengi humfikiria kuwa ama mtoto ama mwanamume anayeteseka akikaribia kufa. Mawazo yao juu ya Yesu hutia ndani kuzaliwa na kufa kwake tu. Mambo ya ajabu aliyosema na kufanya wakati wa maisha yake mara nyingi hayaonwi. Yale aliyotimiza huathiri kila mtu aliyepata kuishi katika dunia hii. Ndiyo sababu ni muhimu tujifunze mengi tuwezayo juu ya mambo mazuri ajabu aliyofanya kwa ajili yetu.” Soma Yohana 17:3. Fungua ukurasa wa kwanza wa utangulizi wa kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na usome fungu la nne. Eleza jinsi kitabu hiki kinavyoweza kupatikana na kutumiwa kwa funzo la kibinafsi.

      6 Hakikisha umeweka rekodi ya kupendezwa na maangusho ili kwamba uweze kufuatia kwa kufanya ziara za kurudia. Kukiwa bado kuna wakati, na tutafute kwa bidii watu wenye mioyo ya kufuatia haki na tuwasaidie wawe wafuasi wa Mwokozi wetu, Yesu Kristo.—Mt. 16:24.

  • Wasihi Wawe Wafuasi Wake
    Huduma ya Ufalme—1994 | Desemba
    • Wasihi Wawe Wafuasi Wake

      1 Kwenye 1 Wakorintho 3:6, Paulo aliandika: “Mimi nilipanda, Apolo akatia maji; bali mwenye kukuza ni Mungu.” Paulo alitumia kusababu huku ili kusaidia ndugu zake kuona uhitaji wa kufanya kazi kwa muungano chini ya ukichwa wa Kristo. Kwa njia hii pia aliwasaidia wathamini sehemu muhimu waliyokuwa nayo katika kazi ya maana ya kupanda na kutia maji.

      2 Kazi hiyo ya kuokoa uhai italetwa kwenye tamati siku hiihii. Tukiwa Wakristo walio wakfu, twashiriki daraka zito la kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu. (Mdo. 13:48) Utafuatiaje kupendezwa ulikoweza kuamsha kwa kutumia kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi?

      3 Ikiwa unarudi kuzuru mtu aliyekubali kitabu, waweza kusema:

      ◼ “Tulipoongea mara ya mwisho, tulizungumzia Yesu Kristo alikuwa ni mtu wa aina gani. Nilifurahia kukuachia kile kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Ni nini kimekupendeza zaidi kuhusu mafundisho ya Yesu na kuhusu utu wake?” Ruhusu itikio. Fungua sura ya 113, na uzungumzie kielelezo bora zaidi cha Yesu cha unyenyekevu. Soma Wafilipi 2:8 kuonyesha jinsi mtume Paulo aliona mwelekeo wa Yesu wa unyenyekevu. Kisha unaweza kueleza jinsi tunavyoweza kujifunza mengi zaidi kupitia funzo la kawaida la Biblia.

      4 Huenda ukapendelea utangulizi huu:

      ◼ “Tuliongea kuhusu mambo aliyofanya Yesu alipokuwa duniani ambayo yaonyesha anatujali kwelikweli. Unafikiri atafanya nini mwishowe ili apumzishe wale ambao wameteseka sana?” Ruhusu itikio. Fungua ukurasa 133, na upitie maelezo yaliyo kwenye fungu la tano. Fungua kwenye picha iliyo katika ukurasa ufuatao, na ueleze kutakavyokuwa wakati mapenzi ya Mungu yafanywapo duniani kama yalivyo mbinguni. Taja manufaa zitakazopatikana kwa kujifunza mengi zaidi.

      5 Ikiwa yaonekana hakuna upendezi wa kutosha kusikiliza, labda unaweza kuanza mazungumzo yako kwa njia hii:

      ◼ “Nafikiri sote wawili twakubali kwamba watu wengi leo hupatanisha maisha zao na mtu fulani wamwonaye kama kielelezo cha kuigwa. Yesu Kristo ni mtu wa kuigwa aliye bora zaidi. Ningependa kushiriki nawe somo la maana sana nililojua kwa kujifunza kielelezo kilichowekwa na Yesu. [Fungua sura ya 40 katika kitabu Mtu Mkuu Zaidi, na utoe uangalifu kwa somo lenye fadhili la Yesu juu ya rehema.] Hili lilinikumbusha kwa mkazo jinsi ninavyohitaji sana kuonyesha wengine sifa hii.” Soma Mathayo 5:7. Ikiwa sasa kunaonekana kupendezwa kwingi zaidi, toa kitabu au broshua Je! Kweli Mungu Anatujali?

      6 Au huenda ukataka kutumia mfikio huu wa moja kwa moja:

      ◼ “Mara ya mwisho nilipokuwa hapa, tulizungumzia umaana wa kupata ujuzi kuhusu Yesu. Yohana 17:3 husema kwamba ‘kwamaanisha uhai wa milele’ kutwaa ujuzi huo. Twaweza kufanyaje hivyo?” Ruhusu itikio. Endelea kwa kueleza mpango wetu wa kujifunza Biblia na jinsi ya kuutumia kwa manufaa.

      7 Paulo asema kwamba mfanya kazi “atapata thawabu yake mwenyewe sawasawa na taabu yake mwenyewe” wakati wa mavuno. (1 Kor. 3:8) Tukijitahidi wenyewe kwa bidii katika kusaidia wengine wawe wafuasi wa Yesu, thawabu yetu itakuwa kubwa kwa hakika.

  • Funzo la Kitabu la Kutaniko
    Huduma ya Ufalme—1994 | Desemba
    • Funzo la Kitabu la Kutaniko

      Ratiba ya mafunzo ya kutaniko katika kitabu Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha.

      Desemba 5: Kurasa 114-122*

      Desemba 12: Kurasa 122*-130

      Desemba 19: Kurasa 131-138*

      Desemba 26: Kurasa 138*-145

      * Hadi au kuanzia kichwa kidogo.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki