-
Kutounga Mkono Upande WowoteKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Bila shaka sivyo. Wao wanajua na wanajitahidi sana kufuata amri hii ambayo Yesu aliirudia: “Mpende jirani yako kama wewe mwenyewe.” (Mt. 22:39) Pia wanafuata lile shauri lililoandikwa na mtume Paulo: “Tuwatendee wote mema, na hasa wale ambao katika imani ni jamaa zetu.” (Gal. 6:10) Wanasadiki kwamba wema ulio mkuu zaidi wanaoweza kuwatendea jirani zao ni kuwatangazia habari njema za Ufalme wa Mungu, ambao utatatua milele matatizo yanayowakabili wanadamu na ambao huwapa wale wanaoukubali tarajio zuri ajabu la uzima wa milele.
-
-
Kuwasiliana na PepoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kuwasiliana na Pepo
Maana: Imani ya kwamba sehemu ya roho ya wanadamu huendelea kuishi baada ya mwili kufa nayo inaweza kuwasiliana na watu walio hai, kwa kawaida inafanya hivyo kupitia mtu anayepitisha habari hizo. Watu fulani huamini kwamba kila kitu chenye mwili na matukio yote ya asili yana roho ndani yake. Ulozi ni kutumia nguvu ambazo inakubaliwa kwamba zinatoka kwa roho waovu. Namna zote za kuwasiliana na pepo zinashutumiwa katika Biblia.
Je, kweli mwanadamu anaweza kuwasiliana na “roho” ya mpendwa aliyekufa?
Mhu. 9:5, 6, 10: “Walio hai wanajua kwamba watakufa; lakini wafu, hawajui lolote kamwe . . . Pia, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari zimepotea, na mpaka wakati usio na kipimo hawana fungu lolote tena katika chochote ambacho kitafanywa chini ya jua. Yote ambayo mkono wako unapata kufanya, yafanye kwa nguvu zako zote, kwa maana hakuna kazi, wala utungaji wala ujuzi wala hekima katika Kaburi, mahali unapokwenda.”
Eze. 18:4, 20: “Nafsi inayotenda dhambi—hiyo yenyewe itakufa.” (Kwa hiyo, nafsi si kitu fulani kinachoendelea kuishi baada ya mwili kufa na ambacho wanadamu walio hai wanaweza kuwasiliana nacho baada ya hapo.)
-