-
Kurudi kwa KristoKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
‘Yesu, unikumbuke utakapoingia katika ufalme wako.’ Naye akamwambia: ‘Kwa kweli mimi nakuambia leo, Utakuwa pamoja nami katika Paradiso.’” (Chini ya utawala wa Yesu, dunia yote itakuwa Paradiso; wafu walio katika kumbukumbu ya Mungu watafufuliwa na kupewa nafasi ya kupata uzima mkamilifu duniani milele.)
Ona pia ukurasa wa 284-289, chini ya kichwa, “Siku za Mwisho.”
-
-
Kusema kwa LughaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Kusema kwa Lugha
Maana: Uwezo wa pekee ambao wanafunzi fulani walipewa katika kutaniko la kwanza la Kikristo kupitia roho takatifu uliowawezesha kuhubiri au kumtukuza Mungu katika lugha nyingine.
Je, Biblia inasema wote walio na roho ya Mungu ‘wangesema kwa lugha’?
1 Kor. 12:13, 30: “Kwa kweli kwa roho moja sote tulibatizwa katika mwili mmoja . . . Je, wote wana zawadi za maponyo? Je, wote husema kwa lugha?” (Ona pia 1 Wakorintho 14:26.)
1 Kor. 14:5: “Basi ningependa ninyi nyote mseme kwa lugha, lakini napendelea zaidi kwamba mtoe unabii. Kwa kweli, yeye anayetoa unabii ni mkubwa kuliko yeye anayesema kwa lugha, isipokuwa, kwa kweli, yeye atafsiri, ili kutaniko lijengwe.”
Mtu akisema kwa maneno ya kusisimuka katika lugha ambayo hajapata kujifunza kamwe, je, hilo linaonyesha kwamba ana roho takatifu?
Je, uwezo wa ‘kusema kwa lugha’ unaweza kutokana na chanzo kingine isipokuwa Mungu wa kweli?
1 Yoh. 4:1: “Wapendwa, msiamini kila neno lililoongozwa na roho [“kila roho,” UV, ZSB], lakini yajaribuni maneno yaliyoongozwa na roho ili kuona kama yanatokana na Mungu.” (Ona pia Mathayo 7:21-23; 2 Kor. 11:14, 15.)
Kati ya wale ‘wanaosema kwa lugha’ leo ni Wapentekoste na Wabaptisti, pia Wakatoliki, Waepiskopali, Wamethodisti,
-