Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 4/02 uku. 2
  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Aprili 8
  • Juma Linaloanza Aprili 15
  • Juma Linaloanza Aprili 22
  • Juma Linaloanza Aprili 29
  • Juma Linaloanza Mei 6
Huduma Yetu ya Ufalme—2002
km 4/02 uku. 2

Ratiba Ya Mkutano Wa Utumishi

Juma Linaloanza Aprili 8

Wimbo 39

Dak. 13: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka Huduma Yetu ya Ufalme. Mahali ambapo kuna video, tia moyo kila mtu atazame video Young People Ask—How Can I Make Real Friends? akijitayarisha kwa ajili ya mazungumzo kwenye Mkutano wa Utumishi wa juma la Aprili 22. Mahali ambapo video hazipatikani, tayarisha sura ya 8 ya kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi kwenye kichwa “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?” Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga kuwe na maonyesho mawili tofauti ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Machi 15 na Amkeni! la Machi 22. Katika kila onyesho, panga kuwe na njia tofauti-tofauti za kujibu kipingamizi cha mtu anayesema “Nina dini yangu mwenyewe.”—Ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 18-19.

Dak. 12: Mahitaji ya kwenu.

Dak. 20: “Fanyeni Lililo Jema Kuelekea Wote.”a Baada ya mazungumzo ya maswali na majibu, hoji mhubiri mmoja au wawili waeleze jinsi wanavyopanua huduma yao.

Wimbo 157 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 15

Wimbo 101

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: Mapainia Waendelea Kusaidia Wengine. Mwangalizi wa utumishi afanye mazungumzo ya kikundi pamoja na mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko, painia, na mhubiri. Mwangalizi wa utumishi azungumzia programu ya Mapainia Wasaidia Wengine kama ilivyoelezwa katika Huduma Yetu ya Ufalme ya Septemba 1998, ukurasa wa 4. Kisha azungumza na kila mmoja katika kikundi hicho daraka lake katika programu hiyo na jinsi inavyotimiza kusudi lake. Ni nini kimefanywa ili programu hiyo ifanikiwe? Mwangalizi wa utumishi awaalika wahubiri wote wamjulishe kama wanataka kupokea msaada katika huduma. Wale ambao walisaidiwa wakati uliopita huenda wakahusishwa tena ili wapate msaada zaidi katika sehemu nyingine ya huduma.

Dak. 20: “Shangwe za Utumishi wa Wakati Wote.”b Tia moyo vijana wafanye upainia msaidizi miezi ya likizo.

Wimbo 199 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 22

Wimbo 90

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ukitumia madokezo yaliyo kwenye ukurasa wa 8, panga mtumishi wa huduma aonyeshe jinsi ya kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi la Aprili 1 na dada aonyeshe jinsi ya kutoa Amkeni! la Aprili 8. Baada ya kila onyesho, rudia sentensi moja au mbili za kwanza zilizotumiwa kuamsha kupendezwa kwa mwenye nyumba.

Dak. 10: Fika kwa Wakati! Hotuba. Mambo yanayohusiana na ibada yetu na utumishi wetu hasa ni mambo ya maana yanayotaka “majira yake.” (Mhu. 3:1) Twataka kufaidika kabisa na mipango ya utumishi wetu kwa Mungu. Mikutano ya kutaniko na ya utumishi wa shambani yapaswa kuanza kwa wakati kamili uliowekwa. Yehova hachelewi kamwe kutekeleza utendaji wake. (Hab. 2:3) Je, twahitaji kufanyia kazi jambo hilo? Pindi kwa pindi, huenda watu wakacheleweshwa na jambo lisiloepukika. Lakini tukiwa na mpango mzuri, hatupaswi kuzoea kuchelewa, tukifika baada ya wimbo na sala ya kwanza ya mkutano au baada ya mipango ya utumishi wa shambani kufanywa. Zungumzia njia zenye kutumika za kusitawisha mazoea mazuri ya kuhakikisha kwamba tutakuwa tukifika kwa wakati katika utendaji wetu wote wa kiroho.—Ona Mnara wa Mlinzi, Juni 15, 1990, ukurasa wa 29.

Dak. 25: Mahali ambapo video hazipatikani, zungumzieni “Naweza Kufanyaje Marafiki wa Kweli?” katika kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi sura ya 8. Mahali ambapo video zapatikana zungumzieni sehemu yenye kichwa “Itikio Changamfu!”c Katika fungu la 1, ruhusu kutaniko liongeze mambo mafupi yaliyoonwa kuhusu video Young People Ask—How Can I Make Real Friends? Kisha mwanze moja kwa moja mazungumzo ya kila swali lililo katika fungu la 2-7. Mwezi wa Juni tutazungumzia video Our Whole Association of Brothers.

Wimbo 191 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Aprili 29

Wimbo 162

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Habari za Kitheokrasi. Wakumbushe wahubiri watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Aprili.

Dak. 15: “Kuhubiri Ufalme Husaidia Kuokoa Uhai!”d Omba wasikilizaji watoe maelezo ya jinsi maandiko yanavyotumika.

Dak. 20: Fanya Utafiti Ukitumia Kitabu Kutoa Sababu. Mazungumzo na wasikilizaji. Mara nyingi katika huduma watu huuliza maswali juu ya habari ambazo hazijaorodheshwa chini ya kichwa “Mazungumzo Makuu” (ukurasa wa 5-6) katika kitabu Kutoa Sababu. “Fahirisi” (ukurasa 439-445) ni yenye msaada zaidi katika kupata Maandiko yanayounga mkono imani zetu. Alika wasikilizaji washiriki kutafuta majibu ya maswali yafuatayo kwa kutazama fahirisi chini ya kila neno lililo katika italiki: Maoni ya Mkristo ni nini kuhusu nyimbo za kutukuza taifa na bendera? Kwa nini Mungu huruhusu Misiba itokee? Waweza kuelezaje maoni ya Biblia kuhusu talaka? Ni wakati gani na kwa nini nyakati nyingine akina dada wanahitaji kufunga kitambaa kichwani? Twajuaje kwamba 144,000 ni idadi halisi katika Biblia? Mfano wa tajiri na Lazaro wamaanisha nini? Tia moyo kila mtu atumie kitabu Kutoa Sababu katika huduma.

Wimbo 28 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Mei 6

Wimbo 141

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Zungumzieni “Endelea Kunufaika na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!”

Dak. 10: Kupanga Mapema Kwa Ajili ya Likizo. Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Eleza mipango ya kawaida inayofanywa wakati wa likizo: kuhudhuria siku zote za kusanyiko la wilaya, kufanya upainia msaidizi kwa mwezi mmoja au zaidi, kurekebisha vitu nyumbani, na labda kupumzika au kuwa na tafrija. Alika watu wachache waeleze mipango yao ya likizo na jinsi watakavyohakikisha kwamba hawapuuzi funzo lao la familia, mikutano ya kutaniko, na utumishi wa shambani, hata kama watasafiri. Ikiwa kutaniko lina eneo lisilohubiriwa kwa kawaida, tangaza mipango iliyofanywa ya kuhubiri kabisa eneo hilo. Wakumbushe wote wahakikishe kwamba mwangalizi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko anapokea ripoti zao za utumishi wa shambani, iwe watu wako nyumbani au wamesafiri.

Dak. 25: “Familia Zawezaje Kuwa na Nguvu Kiroho?”e Baada ya kuzungumzia makala hii, toa mambo yaliyoonwa yenye kutumika kutoka katika Mnara wa Mlinzi, Februari 15, 1999, ukurasa wa 10-12.

Wimbo 17 na sala ya kumalizia.

[Maelezo ya Chini]

a Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

b Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

c Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

d Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

e Toa maelezo ya utangulizi yasiyozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki