-
Ungamo Liletalo Ponyo la KirohoMnara wa Mlinzi—2001 | Juni 1
-
-
(1 Samweli 2:22-25) Lakini Yehova humwonyesha fadhili-upendo mtu anayetubu. Rehema Yake, kama maji baridi yenye kuburudisha, itamsaidia aliyekosa avumilie matokeo ya dhambi yake. Hali nzuri inayotokana na kusamehewa na Mungu na ushirika wenye kujenga pamoja na waabudu wenzake unaweza kumponya kiroho mtu aliyekosa. Naam, kwa msingi wa fidia ya Kristo, mtu anayetubu anaweza kupata “utajiri wa fadhili [ya Mungu] isiyostahiliwa.”—Waefeso 1:7.
“Moyo Safi” na “Roho Mpya”
Baada ya Daudi kuungama, yeye hakujiruhusu apatwe na hali ya kuhisi kwamba hafai kitu. Maneno aliyoandika katika zaburi kuhusu maungamo yaonyesha kitulizo alichopata na pia azimio lake la kumtumikia Mungu kwa uaminifu. Kwa mfano, tazama Zaburi ya 32. Twasoma hivi kwenye mstari wa 1: “Heri aliyesamehewa dhambi, na kusitiriwa makosa yake.” Hata dhambi iwe nzito namna gani, inawezekana kuwe na matokeo mazuri ikiwa mtu anatubu kwa unyofu. Njia moja ya kuonyesha unyofu huo ni kukubali matendo yako yote, kama vile Daudi alivyofanya. (2 Samweli 12:13) Hakujaribu kujitetea mbele ya Yehova au kujaribu kulaumu wengine. Mstari wa 5 unasema: “Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA, nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.” Toba ya kweli huleta kitulizo, kwa hiyo mtu hachomwi na dhamiri yake kwa sababu ya makosa ya wakati uliopita.
Baada ya kumsihi Yehova amsamehe, Daudi alisihi: “Uniumbie moyo safi, ee Mungu, uweke ndani yangu roho mpya na thabiti.” (Zaburi 51:10, BHN) Kuomba “moyo safi” na “roho mpya” kwaonyesha kwamba Daudi alitambua mwelekeo wa dhambi uliokuwa ndani yake na kwamba alihitaji msaada wa Mungu ili asafishe moyo wake na kuanza maisha upya. Badala ya kuanza kujisikitikia, aliazimia kusonga mbele katika utumishi wake kwa Mungu. Alisali hivi: “Ee Bwana, uifumbue midomo yangu, na kinywa changu kitazinena sifa zako.”—Zaburi 51:15.
Yehova aliitikiaje toba ya unyofu na azimio la Daudi la kumtumikia? Alimpa Daudi hakikisho hili lenye kuchangamsha moyo: “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; nitakushauri, jicho langu likikutazama.” (Zaburi 32:8) Hapa tunahakikishiwa kwamba Yehova anajali sana hisia na mahitaji ya mtu anayetubu. Yehova
-
-
Maswali Kutoka kwa WasomajiMnara wa Mlinzi—2001 | Juni 1
-
-
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
Kwa kuwa Yehova yuko tayari kusamehe dhambi kwa sababu ya manufaa ya dhabihu ya fidia, kwa nini ni lazima Wakristo waungame kwa wazee katika kutaniko?
Kama tuonavyo katika kisa cha Daudi na Bath-sheba, Yehova alimsamehe Daudi dhambi zake japo zilikuwa nzito, kwa sababu Daudi alionyesha toba ya kweli. Nathani alipozungumza naye, Daudi alikiri hivi waziwazi: “Nimemfanyia BWANA dhambi.”—2 Samweli 12:13.
Hata hivyo, mbali na kukubali ungamo la kweli la mtenda-dhambi na kumsamehe, Yehova hutoa maandalizi ya upendo ili kumsaidia mkosaji afanye maendeleo na kurudia hali nzuri ya kiroho. Katika kisa cha Daudi, msaada ulitolewa kupitia nabii Nathani. Leo, katika kutaniko la Kikristo, kuna wazee wakomavu kiroho. Mtume Yakobo aeleza hivi: “Je, kuna yeyote mgonjwa [kiroho] miongoni mwenu? Acheni awaite kwake wanaume wazee wa kutaniko, na acheni wasali juu yake, wakimpaka mafuta katika jina la Yehova. Na sala ya imani itamfanya huyo asiyejisikia vizuri apone, na Yehova atamwinua. Pia, ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.”—Yakobo 5:14, 15.
Wazee wenye uzoefu wanaweza kusaidia sana kupunguza huzuni ya moyoni ambayo humpata mkosaji mwenye kutubu. Wao hujitahidi
-