Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sikukuu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Ni kanuni gani za Biblia zinazoonyesha maoni ya Wakristo kuhusu sherehe za kukumbuka matukio mbalimbali katika historia ya kisiasa ya taifa?

      Yoh. 18:36: “Yesu akajibu [gavana Mroma]: ‘Ufalme wangu si sehemu ya ulimwengu huu.’”

      Yoh. 15:19: “Kama [ninyi wafuasi wa Yesu] mngekuwa sehemu ya ulimwengu, ulimwengu ungependa kilicho chake. Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, bali nimewachagua ninyi kutoka ulimwenguni, kwa sababu hiyo ulimwengu unawachukia ninyi.”

      1 Yoh. 5:19: “Ulimwengu mzima unakaa katika nguvu za yule mwovu.” (Linganisha na Yohana 14:30; Ufunuo 13:1, 2; Danieli 2:44.)

      Sikukuu nyingine za sehemu mbalimbali na za kitaifa

      Kuna sikukuu nyingi. Zote haziwezi kuzungumziwa hapa. Lakini historia ambayo imetolewa, inaonyesha mambo tunayoweza kuzingatia kuhusiana na sikukuu yoyote, na kanuni za Biblia zilizozungumziwa zinatoa mwongozo wa kutosha kwa ajili ya wale wanaotamani kufanya mapenzi ya Yehova Mungu.

  • Sikukuu ya Kuzaliwa
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Sikukuu ya Kuzaliwa

      Maana: Siku ya kuzaliwa kwa mtu au ukumbusho wa siku hiyo. Katika sehemu mbalimbali sikukuu ya kuzaliwa kwa mtu, hasa kule kwa mtoto, husherehekewa kwa kufanya karamu na kutolewa kwa zawadi. Hilo si zoea la Kibiblia.

      Je, Biblia inapotaja kuhusu sherehe za sikukuu ya kuzaliwa, inaonyesha kwamba zinafaa? Biblia inataja sherehe mbili tu za aina hiyo:

      Mwa. 40:20-22: “Basi siku ya tatu ilikuwa sikukuu ya kuzaliwa kwa Farao, naye akawafanyia karamu . . . Akamrudisha mkuu wa wanyweshaji kwenye cheo chake cha kunywesha . . . Lakini akamtundika mkuu wa waokaji.”

      Mt. 14:6-10: “Sikukuu ya kuzaliwa kwa Herode ilipokuwa ikisherehekewa binti ya Herodia alicheza dansi na kumpendeza sana Herode hivi kwamba akaahidi kwa kiapo kumpa chochote kile ambacho angeomba. Ndipo yeye, chini ya mwelekezo wa mama yake, akasema: ‘Nipe hapa juu ya sahani kichwa cha Yohana Mbatizaji.’ . . . Akatuma watu wakamkate Yohana kichwa huko gerezani.”

      Kila jambo katika Biblia limo humo kwa sababu fulani. (2 Tim. 3:16, 17) Mashahidi wa Yehova huepuka sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kwa kuwa wanafahamu kwamba Neno la Mungu hutaja mambo yasiyofaa kuhusiana na sikukuu hizo.

      Wakristo wa kwanza na Wayahudi wa nyakati za Biblia walionaje sherehe za sikukuu ya kuzaliwa?

      “Kwa ujumla Wakristo wa kipindi hicho hawakuwa wakisherehekea sikukuu ya kuzaliwa.”—The History of the Christian Religion and Church, During the Three First Centuries (New York, 1848), Augustus Neander (kilichotafsiriwa na Henry John Rose), uku. 190.

      “Waebrania wa baadaye waliziona sherehe za sikukuu ya kuzaliwa kuwa sehemu ya ibada ya sanamu, jambo ambalo lilithibitishwa kabisa na yale waliyoona katika sherehe zilizopendwa ambazo zilihusianishwa na sikukuu hizo.”—The Imperial Bible-Dictionary (London, 1874), kilichohaririwa na Patrick Fairbairn, Buku la 1, uku. 225.

      Desturi zinazopendwa na wengi zinazohusiana na sherehe za sikukuu ya kuzaliwa zilitoka wapi?

      “Desturi mbalimbali ambazo watu leo hutumia kusherehekea sikukuu zao za kuzaliwa ni za tangu zamani. Zilitokana na uchawi na dini. Desturi za kutoa pongezi, zawadi na kusherehekea—pamoja na mishumaa iliyowashwa—nyakati za kale zilikusudiwa kumlinda anayesherehekea sikukuu ya kuzaliwa asiumizwe na roho waovu na kuhakikisha usalama wake mwaka ujao. . . . Kufikia karne ya nne Wakristo walikataa kusherehekea sikukuu ya kuzaliwa kwa kuwa ni desturi ya kipagani.”—Schwäbische Zeitung (nyongeza ya gazeti Zeit und Welt), Aprili 3/4, 1981, uku. 4.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki