Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema
    Huduma ya Ufalme—2002 | Mei
    • Imani Yetu Hutuchochea Kufanya Kazi Njema

      1 Imani ilimfanya Noa, Musa, na Rahabu kutenda. Noa alijenga safina. Musa aliacha faida za muda za maisha katika makao ya Farao. Rahabu alificha wapelelezi, akatii maagizo yao, na hivyo akaokoa familia yake. (Ebr. 11:7, 24-26, 31) Imani yetu hutuchochea kufanya kazi gani njema leo?

      2 Kuhubiri: Imani hutuchochea kuongea juu ya Mungu wetu wa ajabu na mipango yake ya kuandaa furaha ya milele. (2 Kor. 4:13) Nyakati nyingine huenda tukasita kuhubiri. Lakini ‘tukimweka Yehova mbele yetu daima,’ tutaimarishwa na pia woga utapungua. (Zab. 16:8) Kisha imani yetu hutuchochea kutumia kila pindi inayofaa kuwahubiria habari njema watu wa ukoo, majirani, wanafunzi, na wengine.—Rom. 1:14-16.

      3 Kukutanika Pamoja: Kuhudhuria mikutano kwa ukawaida ni kazi nyingine njema inayotokana na imani. Jinsi gani? Huonyesha kuwa tunasadiki kwamba Yesu yuko pamoja nasi kupitia roho takatifu ya Mungu tunapokusanyika kwenye mikutano ya Kikristo. (Mt. 18:20) Huonyesha tamaa yetu ya ‘kusikia lile ambalo roho huyaambia makutaniko.’ (Ufu. 3:6) Tunatii maagizo tunayopokea kwa sababu macho yetu ya imani yanaona kwamba yule anayetufundisha ni Mfundishaji wetu Mkuu, Yehova.—Isa. 30:20.

      4 Mambo Tunayochagua: Usadikisho imara wa mambo ya hakika yasiyoonekana hutuchochea kutanguliza mambo ya kiroho maishani mwetu. (Ebr. 11:1) Mara nyingi hiyo hutia ndani kutofuatilia vitu vya kimwili. Kwa mfano, mzee mmoja alikataa kupandishwa cheo kazini kwa sababu kazi hiyo ingemfanya akose mikutano, awe mbali na familia yake, na kuacha huduma ya upainia. Sisi vilevile na tutumaini kabisa uhakikisho wa Biblia kwamba Yehova atawaandalia wale ‘wanaofuliza kuutafuta kwanza ufalme na uadilifu wake.’—Mt. 6:33.

      5 Watu wengine huona jinsi imani inavyofanya kazi katika maisha yetu. Kwa kweli, imani yetu inajulikana ulimwenguni pote. (Rom. 1:8) Kwa hiyo, sisi sote na tuonyeshe kwa kazi zetu njema kwamba imani yetu iko hai.—Yak. 2:26.

  • Je, Unatumia Broshua Anataka Kuanzisha Mafunzo?
    Huduma ya Ufalme—2002 | Mei
    • Je, Unatumia Broshua Anataka Kuanzisha Mafunzo?

      1 Je, umetambua kwamba ukizungumza na mtu kwa ukawaida kuhusu Biblia na kufuata utaratibu fulani ukitumia mojawapo ya vichapo vinavyopendekezwa, hata ikiwa ni kwa muda mfupi, unaongoza funzo la Biblia? Ndiyo, hata kama unafanya hivyo ukiwa umesimama mlangoni au kwenye simu. Kwa nini usijitahidi kuanzisha funzo la Biblia ukitumia broshua Anataka mwezi wa Mei na Juni?

      2 Jitayarishe Ili Upate Matokeo Mazuri: Unapotoa broshua Anataka, fikiria vizuri kile unachotaka kuzungumzia. Ikiwa unafanya ziara ya kurudia, fikiria yale mliyozungumzia wakati uliopita. Jiulize hivi: ‘Ni mafungu gani katika broshua hii ninayoweza kukazia ili kuendeleza mazungumzo yatakayoelekeza kwenye funzo la Biblia?’ Ikiwa unaenda nyumba kwa nyumba, fikiria mambo yatakayompendeza kijana, mtu mzee, mwanamume, au mwanamke. Zungumzia habari kuu za broshua hiyo, na uchague somo litakaloamsha upendezi wao. Baada ya kuchagua utangulizi utakaotumia, jizoeze mara kadhaa. Hiyo ndiyo mojawapo ya njia za kufanikiwa.

      3 Nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002 ina madokezo manane yanayopatikana chini ya kichwa “Madokezo ya Namna ya Kutoa Broshua Anataka.” Sanduku linalosema “Njia ya Moja kwa Moja” laonyesha jinsi ya kutumia broshua hii kuanzisha mafunzo. Unaweza kutumia dokezo la kwanza ifuatavyo:

      ◼ “Je, unajua kwamba kwa dakika chache tu, unaweza kupata jibu la swali muhimu katika Biblia? Kwa mfano, kwa nini kuna dini nyingi sana zinazodai kuwa za Kikristo? Je, umewahi kujiuliza jambo hilo?” Baada ya mtu huyo kujibu, fungua somo la 13 na mzungumzie mafungu mawili ya kwanza. Wakati ukiruhusu, soma na kuzungumzia andiko moja au mawili. Kisha soma swali la mwisho lililo juu ya ukurasa huo, na useme: “Sehemu inayobaki ya somo hili yakazia mambo matano yanayoitambulisha dini ya kweli. Ningependa kurudi ili tuyachunguze pamoja.”

      4 Endelea Kujitahidi: Tumia kila fursa kuanzisha funzo la Biblia ukitumia broshua Anataka. Omba baraka za Yehova. (Mt. 21:22) Ukiendelea kujitahidi, unaweza kupata shangwe ya kusaidia mtu akubali habari njema!

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki