Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Fidia
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • 1 Yoh. 4:9, 10: “Kwa hili upendo wa Mungu ulifunuliwa kwa habari yetu, kwa sababu Mungu alimtuma Mwana wake mzaliwa-pekee kuja ulimwenguni ili tupate uzima kupitia yeye. Hivi ndivyo upendo ulivyo, si kwamba sisi tumempenda Mungu, bali kwamba yeye alitupenda akamtuma Mwana wake kuwa dhabihu ya upatanisho kwa ajili ya dhambi zetu.”

      Rom. 5:7, 8: “Ni vigumu kwa yeyote kufa kwa ajili ya mtu mwadilifu; kwa kweli, labda, mtu anaweza kuthubutu kufa kwa ajili ya mtu mwema. Lakini Mungu hupendekeza upendo wake mwenyewe kwetu kwa kuwa, tulipokuwa tungali watenda-dhambi, Kristo alikufa kwa ajili yetu.”

      Uandalizi huo unapaswa kuwa na matokeo gani kuhusu jinsi tunavyoishi maisha yetu?

      1 Pet. 2:24: “Yeye mwenyewe alichukua dhambi zetu katika mwili wake mwenyewe juu ya mti, ili tuachane kabisa na dhambi na kuishi kwa uadilifu.” (Kwa sababu ya mambo yote ambayo Yehova na Mwana wake wamefanya ili kututakasa dhambi, tunapaswa kujitahidi kushinda maelekeo ya kufanya dhambi. Hatupaswi hata kidogo kufanya kimakusudi jambo lolote tunalojua ni dhambi!)

      Tito 2:13, 14: “Kristo Yesu, [alijitoa] mwenyewe kwa ajili yetu ili atukomboe sisi kutoka katika kila namna ya uasi-sheria na kujisafishia mwenyewe watu walio wake kwa njia ya pekee, walio na bidii kwa ajili ya kazi njema.” (Kuthamini uandalizi huo wa ajabu kunapaswa kutusukuma tushiriki kwa bidii katika kazi hizo ambazo Kristo aliwapa wafuasi wake wa kweli.)

      2 Kor. 5:14, 15: “Upendo alio nao Kristo hutulazimisha, kwa sababu hili ndilo tumehukumu, kwamba mtu mmoja alikufa kwa ajili ya wote; kwa hiyo, basi, wote walikuwa wamekufa; naye alikufa kwa ajili ya wote ili wale wanaoishi wasiishi tena kwa ajili yao wenyewe, bali kwa ajili ya yeye aliyekufa kwa ajili yao na kufufuliwa.”

  • Har–Magedoni
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Har–Magedoni

      Maana: Neno la Kigiriki Har Ma·ge·donʹ, kutoka katika Kiebrania, ambalo hutafsiriwa na watafsiri wengi kuwa “Amagedoni” au “Har–Magedoni,” linamaanisha “Mlima wa Megido” au “Mlima wa Kusanyiko la Vikosi.” Biblia haihusianishi jina hilo na uharibifu wa kinyukilia, bali na “vita [vinavyokuja vya ulimwengu wote] vya ile siku kuu ya Mungu Mweza-Yote.” (Ufu. 16:14, 16) Jina hilo linatumiwa hasa kuhusu “mahali [Kigiriki, toʹpon; yaani, hali]” ambapo watawala wa kisiasa duniani wanakusanywa ili kumpinga Yehova na Ufalme wake kupitia Yesu Kristo. Upinzani huo utaonyeshwa hatua itakapochukuliwa ulimwenguni pote dhidi ya watumishi wa Yehova walio duniani, ambao wanauwakilisha Ufalme wa Mungu.

      Je, wanadamu wataruhusiwa na Mungu waiangamize dunia kwa kile kinachoitwa “Har–Magedoni ya nyukilia”?

      Zab. 96:10: “Yehova amekuwa mfalme. Nchi [Kiebrania, te·velʹ; dunia, yenye rutuba na inayokaliwa, ulimwengu unaoweza kukaliwa] yenye kuzaa pia hufanywa imara ili isitikiswe.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki