Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mkusanyiko wa Wilaya wa 2000 wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu” wa Mashahidi wa Yehova
    Huduma ya Ufalme—1999 | Desemba
    • 8 Panga Kuhudhuria Siku Zote Tatu: Je, Shetani amejaribu kukukengeusha usikazie fikira mambo ya kiroho? Kwa kusikitisha, ndugu na dada wengi na familia zao wanakosa chakula muhimu cha kiroho. Jinsi gani? Kwa kutohudhuria vipindi vya Ijumaa vya mkusanyiko wa wilaya. Katika visa fulani imeonekana kwamba asilimia kubwa ya akina ndugu wanakosa mafundisho ya kiroho na ushirika ambao huandaliwa katika vipindi vya Ijumaa.

      9 Inawezekana kwamba akina ndugu fulani husita kuwafikia waajiri wao kuomba nafasi ya kuhudhuria mkusanyiko. Je, hivyo ndivyo wewe hufanya? Mbona usisali kwa Yehova juu ya jambo hilo na uwe mwenye moyo mkuu wa kumweleza mwajiri wako hali yako? Kumbuka matokeo mazuri ya Nehemia, ambaye alikuwa katika hali kama hiyo. (Neh. 2:1-6) Uwe na imani kwamba Baba wa mbinguni yu tayari kukusaidia, ukijua kwamba ukitanguliza masilahi ya Ufalme, atakuandalia mahitaji ya lazima ya maisha.—Mt. 6:32b, 33.

      10 Mikusanyiko Yetu Hukuathirije? Dada mmoja kutoka mashariki mwa Marekani aliandika hivi: “Asanteni sana kwa mkusanyiko wa wilaya wa 1999. Kushirikiana na akina ndugu ambao mimi huwaona mara moja tu kwa mwaka huniletea shangwe. Nilipata kweli nikiwa tineja mwenye mimba, nami nakumbuka kwa furaha sana aliyejifunza nami Biblia aliponipeleka kwenye mkusanyiko wangu wa kwanza. Nilitazama mawingu katika stediamu hiyo iliyokuwa wazi tulipoimba wimbo wa Ufalme ‘Ndugu Makumi ya Elfu,’ nami nikatoa machozi. ‘Kukiwa na watu hawa wenye kupendeza kando-kando yangu,’ nikajiuliza, ‘Yehova anawezaje kunitaka?’ Siku hiyo nikaamua kumtumikia Yehova kabisa.” Inachangamsha moyo kama nini! Kwa kweli ni jambo lenye kupendeza kushirikiana na watu safi wa Yehova, sivyo?

      11 Tukiwa katika sehemu ya kumalizia ya siku za mwisho, twahitaji mkusanyiko wetu wa wilaya wa kila mwaka zaidi ya wakati mwingine wowote. Ni uandalizi kutoka kwa Yehova kudumisha afya na usawaziko wetu wa kiroho. Kwa hiyo, azimia kuhudhuria sikuzote tatu za Mkusanyiko wa Wilaya wa mwaka huu wa “Watekelezaji wa Neno la Mungu.” Waweza kuendeleaje mpaka mwisho na azimio lako? Mwombe mwajiri wako mapema akupe ruhusa ya kuhudhuria mkusanyiko wote. Ikiwa huna hela za kutosha, anza sasa kuweka kando fedha zinazohitajiwa ili uhudhurie. Mwombe Yehova msaada ushinde kizuizi chochote. Ukifanya hivyo, waweza kutazamia kufurahia ushirika mchangamfu wa ndugu na dada zako na kusikia semi za uhai wa milele kutoka kwa Baba yetu wa mbinguni, Yehova.—Linganisha Yohana 6:68.

  • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2000
    Huduma ya Ufalme—1999 | Desemba
    • Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 2000

      1 Shule ya Huduma ya Kitheokrasi imethibitika kuwa yenye baraka nyingi kwa watu wa Yehova. Zaidi ya miaka 50 iliyopita, imesaidia mamilioni kusitawisha uwezo wao mbalimbali wakiwa wasemaji wa hadharani na walimu wa kweli za Biblia. (Zab. 145:10-12; Mt. 28:19, 20) Je, waweza kuona jinsi ambavyo shule imekusaidia? Inaweza kuendelea kufanya hivyo mwaka wa 2000 ikiwa utashiriki kikamili na kutumia shauri linalotolewa.

      2 Maagizo kuhusu migawo na vichapo vitakavyotumiwa yameorodheshwa kwenye ukurasa wa kwanza wa ratiba ya shule ya mwaka wa 2000. Wakati uliowekwa kwa kila sehemu, chanzo cha habari, jinsi habari hiyo yapasa kutolewa, na mambo mengine yamefikiriwa. Tafadhali chukua wakati usome maagizo hayo kwa uangalifu na kuyatumia.

      3 Usomaji wa Biblia Kila Juma: Kuna programu mbili tofauti za usomaji wa Biblia kila juma ambazo zimeorodheshwa katika ratiba ya shule. Moja ni programu ya usomaji wa kawaida ya kurasa tano hivi za Biblia. Mambo makuu ya Biblia yanategemea usomaji huu. Usomaji ule mwingine ni wa kuongezea nao huwa na habari maradufu. Kwa kufuata programu hii utaweza kusoma Biblia yote kwa miaka mitatu. Inaeleweka kwamba watu fulani huenda wakataka kusoma zaidi ya habari iliyo katika ratiba ya programu ya kuongezea, na wengine huenda wasiweze. Furahia kile unachoweza kutimiza, badala ya kujilinganisha na wengine. (Gal. 6:4) Jambo muhimu ni kusoma Neno la Mungu kila siku.—Zab. 1:1-3.

      4 Ili kujiandikisha katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, unapaswa kuongea na mwangalizi wa shule. Tafadhali chukua migawo yako kwa uzito, na usikose kuitoa bila sababu. Thamini uandalizi wa shule kutoka kwa Yehova. Jitayarishe vema, ijue habari uliyogawiwa vilivyo, na ujieleze kutoka moyoni, kwa njia hiyo, ukinufaika na shule hii ya pekee.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki