-
Mikutano Ya Utumishi Kwa ApriliHuduma ya Ufalme—1999 | Aprili
-
-
Mikutano Ya Utumishi Kwa Aprili
Juma Linaloanza Aprili 5
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Pitia “Je, Tutoe Kitabu Muumba?” Tia moyo makutaniko yaliyo na vyuo na vyuo vikuu katika eneo lao watolee wahadhiri na wanafunzi vilevile kichapo hiki. Alika wote wenye kupendezwa wahudhurie hotuba ya pekee Aprili 18. Hotuba hiyo ina kichwa “Urafiki wa Kweli Pamoja na Mungu na Jirani.”
Dak. 15: “Hubiri Habari Njema kwa Hamu.” Toa utangulizi wa makala hiyo kwa dakika moja hivi, halafu uendelee na mazungumzo ya maswali na majibu. Malizia kwa kitia-moyo kinachotegemea kitabu Kiongozi cha Shule, ukurasa wa 191-192, fungu la 12-13.
Dak. 20: “Jinsi Ambavyo Washiriki wa Familia Hushirikiana ili Kushiriki Kikamili—Katika Huduma.” Mazungumzo ya kikundi cha familia. Zungumzia sababu ambazo familia zapaswa kuona utumishi wa shambani kuwa jambo la kawaida la kila juma ambalo wote wanapaswa kushiriki. Pitia kitia-moyo kinachotolewa katika Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 1993, ukurasa wa 17-19, fungu la 9-12. Waombe wazazi wanaohudhuria wasimulie jinsi ambavyo wamefanikiwa kupanga utumishi wa kila juma wa familia yao.
Wimbo 67 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 12
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.
Dak. 15: Mahitaji ya kwenu.
Dak. 20: “Kuzidi Kutoa Ushahidi Mwisho Ukaribiapo.” Maswali na majibu. Hoji mhubiri mmoja au wawili ambao hawangeweza kuwazia kwamba wangeshiriki katika kazi ya kuhubiri lakini sasa wanafanya hivyo kwa ukawaida kwa sababu wamekuja kuthamini uhitaji wa haraka wa kueneza ujumbe wa Ufalme. Wakati ukiruhusu, tia ndani mambo mafupi yaliyoonwa kutoka katika kichapo 1997 Yearbook, ukurasa wa 42-48, ukionyesha jinsi ambavyo wahubiri wamezidisha jitihada zao za kutoa ushahidi kwa kwenda mahali ambapo watu wanapatikana.
Wimbo 93 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 19
Dak. 5: Matangazo ya kwenu na Habari za Kitheokrasi.
Dak. 10: “Je, Una Agizo Hususa la Magazeti?” Hotuba itolewe hasa na mzee au mtumishi wa huduma anayeshughulikia magazeti. Julisha kutaniko idadi ya magazeti inayopokewa kila mwezi na wastani wa idadi inayoripotiwa kuwa imeangushwa. Hatupaswi kuacha magazeti yetu bila kutumiwa. Toa madokezo ya kuonyesha jinsi nakala za zamani zinavyoweza kugawanywa.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1993, ukurasa wa 1.
Dak. 30: “Kupainia—Matumizi Yenye Hekima ya Wakati Wetu!” Maswali na majibu. Wape mgawo watu watatu wasimulie mambo yaliyoonwa yaliyo kwenye fungu la 5-7. Malizia kwa kuwaalika wote wanaoweza kufikiria kujiandikisha katika utumishi wa painia-msaidizi au wa kawaida. Fomu za maombi zapatikana kutoka kwa mshiriki yeyote wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko. Taja kwamba si kuchelewa mno kuleta fomu ya ombi la kufanya upainia-msaidizi katika Mei.
Wimbo 165 na sala ya kumalizia.
Juma Linaloanza Aprili 26
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti zao za utumishi wa shambani za Aprili. Tangaza majina ya wale watakaopainia Mei, na utie moyo wengine wajaze ombi. Toa madokezo fulani yenye kusaidia ya kutoa magazeti ya karibuni.—Ona Huduma ya Ufalme Yetu ya Oktoba 1996, ukurasa wa 12.
Dak. 17: “‘Nifanyeje?’” Baada ya kupitia makala kifupi pamoja na wasikilizaji, angalia tineja akiongea na mzazi wake juu ya mipango ya wakati ujao baada ya kumaliza shule ya sekondari. Wanapitia pamoja Huduma ya Ufalme Yetu ya Julai 1998, ukurasa wa 4. Mzazi atoa shauri kupatana na kitia-moyo kilichotolewa katika gazeti Mnara wa Mlinzi la Februari 1, 1996, ukurasa wa 14, na Desemba 1, 1996, ukurasa wa 17-19. Sasa kwa kuwa matakwa ya saa ya mapainia yamepunguzwa, tineja afikiria uwezekano wa kupainia anapomaliza elimu ya kimwili.
Dak. 18: Hoji Mapainia-Wasaidizi. Mwangalizi wa utumishi ahoji baadhi ya wahubiri ambao wanafanya upainia-msaidizi mwezi huu na pia wengine ambao wamefanya hivyo wakati uliopita. Waalike wasimulie baraka ambazo wamefurahia, kile ambacho wametimiza, na kwa nini wanatazamia kwa hamu kufanya upainia-msaidizi tena kwa angalau mwezi mmoja au miwili kila mwaka.
Wimbo 69 na sala ya kumalizia.
-
-
Je, Tutoe Kitabu Muumba?Huduma ya Ufalme—1999 | Aprili
-
-
Je, Tutoe Kitabu Muumba?
Sisi sote tulifurahia kupokea kitabu Je, Kuna Muumba Anayekujali? Kitabu hicho kimekusudiwa hasa wale ambao, ijapokuwa wana elimu ya juu kuhusu mambo ya kilimwengu, huenda ikawa hawamwamini Mungu. Kitabu hiki chashughulika na uhitaji wenye kuongezeka daima.
Kwa sababu zenye kutumika, toleo la fasihi la kila mwezi sikuzote huwa vichapo vyenye kuvutia sana. Je, hiyo yamaanisha kwamba tuepuke kutoa kitabu Muumba? Sivyo hata kidogo! Kitabu hiki chaweza kutolewa wakati wowote mwakani kwa watu ambao hawamwamini Mungu na ambao huenda wakanufaika nacho. Pia huenda kikatolewa kwa watu wanaomwamini Mungu lakini wasiomjua kabisa au wasiojua sifa zake na makusudi yake. Kwa hiyo, unatiwa moyo kubeba nakala moja katika mkoba wako wa mahubiri na kuwa tayari kukitolea mtu yeyote unayefikiri atapendezwa kukisoma.
-
-
Ripoti Ya Utumishi Ya DesembaHuduma ya Ufalme—1999 | Aprili
-
-
Ripoti Ya Utumishi Ya Desemba
Wast. Wast. Wast. Wast.
Idadi ya: Saa Mag. Z. K. Maf. Bi.
B
Pai. Pekee 21 109.5 4.9 50.0 9.3
Mapai. 127 75.9 1.5 37.2 5.6
Pai. Msai. 98 67.0 1.0 27.4 4.2
Wahu. 2,218 16.9 0.5 7.1 1.4
JUMLA 2,464 Kilele Kipya: 2,450
K
Pai. Pekee 165 120.2 30.2 42.6 7.5
Mapai. 1,419 68.3 13.6 19.9 3.6
Pai. Msai. 764 60.1 11.9 12.6 2.1
Wahu. 10,640 13.9 3.1 3.9 0.8
JUMLA 12,988
R
Pai. Pekee 58 133.3 16.6 51.6 8.8
Mapai. 555 74.8 4.7 31.7 4.2
Pai. Msai. 206 66.3 3.0 27.5 3.6
Wahu. 5,172 19.2 1.4 9.2 1.4
JUMLA 5,991 Kilele Kipya: 5,879
S
Pai. Msai. 51 82.3 7.1 58.1 5.5
Wahu. — 14.4 1.8 10.0 1.6
T
Pai. Pekee 70 133.4 38.4 58.7 7.4
Mapai. 642 73.3 13.2 27.5 3.5
Pai. Msai. 305 59.1 9.6 16.2 2.1
Wahu. 5,980 13.4 2.5 4.9 0.7
JUMLA 6,997
U
Pai. Pekee 21 120.2 30.0 42.5 6.9
Mapai. 142 67.6 9.3 26.5 4.8
Pai. Msai. 63 59.1 7.1 21.6 3.7
Wahu. 1,892 12.3 2.2 4.6 1.0
JUMLA 2,118
-