-
“Mtumikieni Yehova kwa Kushangilia”Huduma ya Ufalme—2003 | Oktoba
-
-
“Mtumikieni Yehova kwa Kushangilia”
1 “Sikuzote shangilieni katika Bwana,” akaandika mtume Paulo. “Mara nyingine tena nitasema, Shangilieni!” (Flp. 4:4) Pendeleo la kutangaza habari njema na kuwasaidia watu walio kama kondoo wamwabudu Yehova huleta shangwe nyingi. (Luka 10:17; Mdo. 15:3; 1 The. 2:19) Hata hivyo, ikiwa nyakati nyingine tunapoteza shangwe katika huduma yetu, tunaweza kufanya nini?
2 Kazi Kutoka kwa Mungu: Kumbukeni kwamba utume wetu wa kuhubiri umetoka kwa Yehova. Ndiyo, tuna pendeleo kubwa sana la kuwa “wafanyakazi wenzi wa Mungu” katika kutangaza ujumbe wa Ufalme na kufanya wanafunzi! (1 Kor. 3:9) Kristo Yesu yuko pamoja nasi katika kazi hii ambayo haitarudiwa tena kamwe. (Mt. 28:18-20) Malaika pia wanahusika, nao hufanya kazi pamoja nasi katika mavuno makubwa ya kiroho yanayoendelea sasa. (Mdo. 8:26; Ufu. 14:6) Maandiko, pamoja na mambo yaliyoonwa kati ya watu wa Mungu, hutoa ushahidi wa wazi kwamba Yehova anategemeza kazi hiyo. Kwa hiyo, tunapohubiri huwa ‘tumetumwa kutoka kwa Mungu, machoni pa Mungu, kwa kushirikiana na Kristo.’ (2 Kor. 2:17) Hiyo ni sababu nzuri sana ya kushangilia!
3 Sala ni muhimu ili kudumisha shangwe yetu katika utumishi wa Mungu. (Gal. 5:22) Kwa kuwa tunaweza kufanya kazi ya Mungu kwa nguvu zake tu, tunahitaji kumwomba atupe roho yake, ambayo huwapa kwa ukarimu wale wanaomwomba. (Luka 11:13; 2 Kor. 4:1, 7; Efe. 6:18-20) Kusali kuhusu huduma yetu kutatusaidia kudumisha mtazamo unaofaa tunapokabili watu wasiokubali ujumbe wetu. Kutatusaidia tuendelee kuhubiri kwa ujasiri na kwa shangwe.—Mdo. 4:29-31; 5:40-42; 13:50-52.
4 Jitayarishe Vizuri: Njia nzuri ya kuongeza shangwe tunaposhiriki katika huduma ni kwa kujitayarisha vizuri. (1 Pet. 3:15) Si lazima matayarisho hayo yachukue muda mrefu. Unaweza kuchukua dakika chache tu kupitia namna mbalimbali za kutoa magazeti ya karibuni au kichapo unachopanga kumtolea mwenye-nyumba. Ili kupata utangulizi unaofaa, unaweza kuchunguza kitabu Kutoa Sababu au matoleo yaliyopita ya Huduma Yetu ya Ufalme. Baadhi ya wahubiri wa Ufalme huandika katika karatasi ndogo maneno machache watakayosema. Mara kwa mara, wanatazama karatasi hiyo ili kujikumbusha. Hilo huwasaidia kuondoa wasiwasi na kuwawezesha kuhubiri kwa ujasiri.
5 Shangwe hutokeza faida nyingi. Tukiwa na shangwe, watu watavutiwa na ujumbe wetu. Shangwe hutupa nguvu ya kuvumilia. (Neh. 8:10; Ebr. 12:2) Zaidi ya yote, utumishi wetu wa shangwe humtukuza Yehova. Kwa hiyo, na ‘tumtumikie Yehova kwa kushangilia.’—Zab. 100:2.
-
-
Habari Za KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2003 | Oktoba
-
-
Habari Za Kitheokrasi
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Burundi: Kibuye na Mbogora.
Tanzania: Senjele.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2003 | Oktoba
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Sept. 15
“Katika ulimwengu wa leo, watu fulani wanahisi kwamba wamenaswa katika ndoa isiyo na upendo. Watu hao wanaweza kupata wapi msaada? [Mruhusu ajibu.] Biblia inatuhakikishia kwamba kanuni za Mungu zinaweza kutusaidia. [Soma Isaya 48:17, 18.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi huchanganua kanuni za Biblia zinazoweza kuimarisha ndoa.”
Amkeni! Sept. 22
“Sisi hushangazwa na uwezo wa wanyama wa kuwasiliana. Lakini, je, unajua kwamba wanadamu wana sifa za pekee? [Mruhusu ajibu. Kisha soma Zaburi 65:2.] Tofauti na wanyama, sisi hutamani kuwasiliana na Mungu. Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kuwa na mawasiliano mazuri kati yetu wenyewe na pamoja na Mungu.”
Mnara wa Mlinzi Okt. 1
“Je, umewahi kujiuliza, ‘Ikiwa Mungu ni mwenye upendo na ana nguvu zote, mbona hawasaidii wale wanaoteseka?’ [Mruhusu ajibu.] Hivi karibuni atakomesha matatizo yote. [Soma Isaya 65:17.] Kwa sasa, Mungu hatazami tu bila kujali huku tunapoteseka, kama vile gazeti hili linavyoonyesha.”
Amkeni! Okt. 8
“Je, umesikia kwamba wakulima wengi wanashindwa kutegemea kilimo ili kujiruzuku? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia tatizo hilo pamoja na ahadi ya Biblia ya wakati ujao ulio bora. [Soma Zaburi 72:16.] Nitakaporudi, nitakueleza jinsi Mungu atakavyotimiza jambo hilo.”
-