Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • “Iweni Tayari”
    Huduma ya Ufalme—2003 | Novemba
    • “Iweni Tayari”

      1 Katika unabii wake mkuu kuhusu umalizio wa huu mfumo wa mambo, Yesu alionya kuhusu kuhangaikia sana mambo ya kawaida ya maisha. (Mt. 24:36-39; Luka 21:34, 35) Kwa kuwa dhiki kuu inaweza kuanza wakati wowote, ni lazima tutii onyo hili la Yesu: “Iweni tayari, kwa sababu Mwana wa binadamu atakuja katika saa msiyofikiria.” (Mt. 24:44) Ni nini kinachoweza kutusaidia kufanya hivyo?

      2 Kupambana na Mahangaiko na Vikengeusha-Fikira: Mojawapo ya mitego ya kiroho ambayo lazima tujilinde nayo ni “mahangaiko ya maisha.” (Luka 21:34) Katika nchi fulani, umaskini, ukosefu wa kazi, na gharama za juu za maisha hufanya iwe vigumu kupata mahitaji ya lazima ya maisha. Katika nchi nyingine, kurundika mali ni jambo la kawaida. Tukianza kufikiria sana vitu vya kimwili tutashindwa kukazia fikira mambo ya Ufalme. (Mt. 6:19-24, 31-33) Mikutano ya Kikristo hutusaidia kuendelea kukazia fikira mambo ya Ufalme. Je, una lengo la kuhudhuria kila mkutano?—Ebr. 10:24, 25.

      3 Leo ulimwengu umejaa vikengeusha-fikira ambavyo vinaweza kutupotezea wakati muhimu sana. Kutumia kompyuta kunaweza kuwa mtego ikiwa mtu anatumia Internet kwa saa nyingi mno, anasoma na kutuma barua-pepe, au anacheza michezo ya kompyuta kwa saa nyingi. Tunaweza kupoteza wakati mwingi tukitazama televisheni, sinema, kufanya mambo tunayopenda, kusoma vitabu vya kilimwengu, na kushiriki michezo huku tukibaki na wakati na nguvu kidogo tu za kufanya mambo ya kiroho. Ingawa burudani na starehe zinaweza kutuburudisha kidogo, funzo la Biblia la kibinafsi na la familia huleta faida za milele. (1 Tim. 4:7, 8) Je, wewe hununua wakati wa kutafakari Neno la Mungu kila siku?—Efe. 5:15-17.

      4 Twaweza kushukuru sana kwamba tengenezo la Yehova limefanya mipango ya mafundisho ya kiroho ya kutusaidia tupate ‘kufanikiwa kuponyoka mambo yote yaliyokusudiwa kutukia, na kusimama mbele ya Mwana wa binadamu’! (Luka 21:36) Na tufaidike kabisa na mipango hiyo ya kiroho na ‘tuwe tayari’ ili imani yetu ipate kuwa “sababu ya sifa na utukufu na heshima wakati wa ufunuo wa Yesu Kristo.”—1 Pet. 1:7.

  • Pongezi Hutia Moyo
    Huduma ya Ufalme—2003 | Novemba
    • Pongezi Hutia Moyo

      1 “Je, sijawa mtoto mzuri leo?” Hivyo ndivyo msichana mdogo alivyouliza huku machozi yakimtiririka wakati wa kulala. Swali hilo lilimshangaza mamake. Ijapokuwa aliona jinsi msichana wake mdogo alivyojitahidi sana kuwa na adabu siku hiyo, alikosa kumpongeza. Machozi ya msichana huyo mdogo yanapaswa kutukumbusha kwamba sisi sote tunahitaji pongezi, tuwe wachanga au wakubwa. Je, sisi huwatia moyo wengine kwa kuwapongeza kwa sababu ya mambo mazuri wanayofanya?—Met. 25:11.

      2 Tuna sababu nyingi nzuri za kuwapongeza Wakristo wenzetu. Wazee, watumishi wa huduma, na mapainia hujitahidi sana kutimiza madaraka yao. (1 Tim. 4:10; 5:17) Wazazi wanaomwogopa Mungu hujitahidi kadiri wawezavyo kuwalea watoto wao kupatana na njia za Yehova. (Efe. 6:4) Vijana Wakristo wanajikakamua sana kuipinga “roho ya ulimwengu.” (1 Kor. 2:12; Efe. 2:1-3) Wengine humtumikia Yehova kwa uaminifu licha ya uzee, matatizo ya afya, au magumu mengine. (2 Kor. 12:7) Wote hao wanastahili pongezi. Je, sisi huwapongeza kwa sababu ya jitihada zao?

      3 Toa Pongezi Hususa kwa Mtu Binafsi: Kwa kweli sisi sote hufurahi kutaniko lote linapopongezwa. Hata hivyo, tunatiwa moyo zaidi tunapopongezwa kibinafsi. Kwa mfano, katika sura ya 16 ya barua yake kwa Waroma, Paulo aliwapongeza kihususa, Fibi, Priska, Akila, Trifaina, Trifosa, Persisi, na wengineo. (Rom. 16:1-4, 12) Bila shaka maneno yake yaliwatia moyo kwelikweli waaminifu hao! Kuwasifu ndugu na dada zetu kwa njia hiyo huwahakikishia kwamba wanahitajiwa na huboresha uhusiano wetu. Je, umempongeza kihususa mtu fulani hivi karibuni?—Efe. 4:29.

      4 Kutoka Moyoni: Ili tuwatie wengine moyo kwelikweli, lazima tuwapongeze kutoka moyoni. Watu wanaweza kujua kama tunaongea kutoka moyoni au ikiwa ‘tunawabembeleza tu kwa ulimi.’ (Met. 28:23) Tunapojizoeza kuona sifa nzuri za wengine, moyo wetu utatuchochea kuwapongeza. Na tuwapongeze wengine sana kutoka moyoni tukijua kwamba “neno linalosemwa wakati unaofaa ni jema kama nini!”—Met. 15:23.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki