-
Matumizi ya Internet—Uwe Chonjo Kuhusu Hatari Zake!Huduma ya Ufalme—1999 | Novemba
-
-
za mfuatano, na nyingi zaidi—kwa kila mtu aliye katika kitabu chao cha anwani za elektroni.”
31 Imekuwa hivyo na barua za kompyuta zinazoenezwa kwa ndugu wengi—habari kama vile vichekesho au hadithi zenye kuchekesha juu ya huduma; shairi linalodhaniwa kuwa lategemea itikadi zetu; vielelezo kutoka kwenye hotuba mbalimbali zilizosikiwa kwenye makusanyiko, mikusanyiko, au kwenye Jumba la Ufalme; mambo yaliyoonwa katika huduma ya shambani; na kadhalika—mambo yanayoonekana kuwa yasiyo na kosa. Wengi hupeleka barua za kompyuta kama hizo bila kuchunguza kiini, ikifanya iwe vigumu kujua kikweli ni nani aliyekuwa mwanzilishi, jambo ambalo humfanya mtu ajiulize kama habari hiyo ni ya kweli.—Mit. 22:20, 21.
32 Ujumbe mbalimbali wa kipuuzi kama huo mara nyingi si wenye maneno yenye afya ambayo Paulo alikuwa nayo akilini alipomwandikia Timotheo, akisema: “Fuliza kushika kiolezo cha maneno yenye afya ulichosikia kutoka kwangu pamoja na imani na upendo vinavyohusiana na Kristo Yesu.” (2 Tim. 1:13) “Lugha iliyo safi” ya kweli ya Kimaandiko ina “kiolezo cha maneno yenye afya” yanayotegemea hasa kichwa cha Biblia cha kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova kupitia Ufalme wake. (Sef. 3:9) Twapaswa kujitahidi sana kutumia wakati wetu wote na nishati iliyopo kuunga mkono kutetewa kwa enzi kuu ya Yehova.
33 Kwa kuwa tumo kabisa katika wakati wa mwisho wa huu mfumo wa mambo, huu si wakati wa kuacha kuwa macho. Biblia hutuonya hivi: “Tunzeni akili zenu, iweni wenye kulinda. Mpinzani wenu, Ibilisi, hutembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta sana kunyafua mtu fulani.” (1 Pet. 5:8) Yaendelea kusema: “Vaeni suti kamili ya silaha kutoka kwa Mungu ili mpate kuweza kusimama imara dhidi ya mbinu za Ibilisi.”—Efe. 6:11.
34 Internet ikitumiwa vibaya, inaweza kuwa njia ya Shetani ya kushinda wale wanaoshawishwa na uwezo wake. Ijapokuwa inaweza kuwa na manufaa ya kadiri, kuna hatari mtu asipojihadhari. Hasa wazazi wanahitaji kujali jinsi watoto wao wanavyotumia Internet.
35 Kudumisha maoni yaliyosawazika kuhusu Internet ni ulinzi. Twathamini kikumbusha cha wakati ufaao cha Paulo: “Acheni wale . . . wanaoutumia ulimwengu [wawe] kama wale wasioutumia kwa ukamili; kwa maana mandhari ya ulimwengu huu inabadilika.” (1 Kor. 7:29-31) Kukumbuka mambo hayo kutatusaidia sisi na familia zetu kutokengeushwa na mambo yote ambayo ulimwengu waweza kutoa, kutia ndani mambo yapatikanayo kwenye Internet.
36 Ni muhimu kwetu kuwa karibu na ndugu zetu katika kutaniko na kutumia wakati unaobaki kwa hekima, hivyo tukijitoa kwa ajili ya kuendeleza masilahi ya Ufalme. Mfumo huu ukaribiapo kukoma, acheni “[tu]siendelee tena kutembea kama vile mataifa watembeavyo pia katika ukosefu wa faida wa akili zao,” bali acheni “[twendelee] kufahamu mapenzi ya Yehova ni nini.”—Efe. 4:17; 5:17.
-
-
Sanduku La SwaliHuduma ya Ufalme—1999 | Novemba
-
-
Sanduku La Swali
◼ Ni nani mwenye daraka la kusafisha Jumba la Ufalme?
Jumba la Ufalme lililo safi na lenye kuvutia hufanya watu wavutiwe na ujumbe tunaohubiri. (Linganisha 1 Petro 2:12.) Kuliweka jumba likiwa nadhifu ni jambo muhimu, na kila mtu anaweza kushiriki kulisafisha. Hatupaswi kutazamia watu wachache tu wabebe mzigo wote. Mara nyingi, usafi hupangwa kulingana na vikundi vya Funzo la Kitabu la Kutaniko, kiongozi wa funzo au msaidizi wake akichukua uongozi. Katika majumba ambamo zaidi ya kutaniko moja hukutania, wazee watapanga mambo ili makutaniko yote yashiriki kazi ya kulidumisha katika hali nzuri.
Twaweza kutimizaje daraka hilo vizuri zaidi? Jumba la Ufalme lapasa kusafishwa kulingana na ratiba ya kawaida. Vifaa vya kusafishia vyapaswa kuwepo ili vitumiwe kusafishia. Orodha ya mambo yanayohitaji kufanywa yapasa kuandikwa na kubandikwa mahali ambapo wafanyakazi wanaweza kuiangalia wapate mwelekezo. Kwaweza kuwa na orodha mbili tofauti, moja ya kufanya usafi wa ujumla wa haraka baada ya mkutano na nyingine ya kufanya usafi kikamili wa kila juma. Kiongozi wa funzo la kitabu apaswa kuratibu usafi unaofanywa kikamili uwe siku na wakati ambao wote waliogawiwa watapatikana. Nyasi, maua, na vichaka vyapasa kutunzwa pia. Vijia vya kandokando na mahali pa kuegesha magari hapapaswi kuwa na takataka. Kila mwaka usafi kamili wapasa kufanywa, labda kabla tu ya Ukumbusho. Hiyo yaweza kutia ndani kusafisha madirisha na kuta, kung’arisha sakafu, na kufua pazia.
Bila shaka, sisi sote twaweza kufanya mzigo uwe rahisi kwa kutoangusha chingamu au takataka ndani au nje ya jumba. Twaweza kusafisha choo baada ya kukitumia, tukikiacha kikiwa safi kwa ajili ya mtu mwingine. Jihadhari kutovunja vyombo au kuharibu viti. Uwe mwepesi kuona viti vilivyoharibika, matatizo ya mifereji, taa zilizoungua, na kadhalika, na uripoti mambo hayo bila kukawia kwa ndugu anayehusika na udumishaji wa Jumba la Ufalme.
Sisi sote na tuwe tayari kutimiza sehemu yetu. Hiyo hufanya tuwe na nyumba ya ibada yenye kupendeza na inayotutofautisha sisi kuwa watu safi wanaomheshimu Yehova Mungu.—1 Pet. 1:16.
-