Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Januari
    • Jinsi ya Kutumia Mapendekezo ya Kutoa Vichapo

      1 Mapendekezo ya jinsi ya kutoa magazeti yetu na vichapo vingine hupatikana kwa ukawaida katika Huduma Yetu ya Ufalme. Tunapohubiri hatuhitaji kutumia mapendekezo hayo jinsi yalivyoandikwa. Yameandaliwa ili kutuonyesha mambo tunayoweza kusema. Kwa kawaida tutakuwa na matokeo zaidi tukitumia maneno yetu wenyewe. Tukijieleza kwa njia ya kawaida mwenye nyumba atajihisi huru, na itaonyesha kwamba sisi ni wanyoofu na tuna uhakika na tunachosema.—2 Kor. 2:17; 1 The. 1:5.

      2 Badili Mazungumzo Yako: Jinsi tunavyohubiri habari njema hutegemea sana desturi za kwetu. Je, unaweza kumsalimu mwenye nyumba na kuzungumza naye kidogo, kisha uingize ujumbe wako katika mazungumzo yenu, au watu katika eneo lenu humtazamia mtu aseme moja kwa moja habari aliyokuwa nayo? Jambo hili hutofautiana katika sehemu mbalimbali, na nyakati nyingine hutegemea mapendezi ya mtu. Tunahitaji pia kutumia busara tunapouliza maswali. Maswali yanayofaa katika sehemu fulani huenda yakawaaibisha watu katika sehemu nyingine. Kwa hiyo, tunahitaji kuwa na busara na kubadili mazungumzo yetu ili yafae watu katika eneo letu.

      3 Isitoshe, tunapojitayarisha kwa ajili ya huduma ya shambani, tunahitaji kufikiria malezi na maoni ya watu katika eneo letu. Yaelekea ungemweleza Mkatoliki andiko la Mathayo 6:9, 10 kwa njia tofauti na ile ambayo ungetumia kumweleza mtu asiyejua ile “Sala ya Bwana.” Tukitumia busara, mara nyingi tunaweza kubadili mazungumzo yetu ili yawavutie zaidi watu tunaokutana nao katika huduma yetu.—1 Kor. 9:20-23.

      4 Hata ikiwa tunapanga kutumia mapendekezo hayo jinsi yalivyo au kuyabadili kidogo, bado tunahitaji kujitayarisha vizuri. Tunapaswa kusoma kwa makini makala au sura tunayotaka kuzungumzia na kutafuta mambo ambayo huenda yakaamsha upendezi. Kisha tutumie mambo hayo katika mazungumzo yetu. Tukijua habari nzuri zinazopatikana katika vichapo vyetu tunaweza kuwatolea wengine vichapo hivyo kwa shauku.

      5 Kutumia Habari Tofauti: Je, ni lazima tutumie mapendekezo yaliyo katika Huduma Yetu ya Ufalme? La. Ikiwa ni rahisi kwako kutumia habari nyingine au andiko lingine, unaweza kufanya hivyo. Unapotoa magazeti hasa, tafuta fursa ya kuzungumzia makala zilizo ndani ya gazeti, zinazowavutia watu katika eneo lenu. Ikiwa kutakuwa na maonyesho kwenye Mkutano wa Utumishi kuhusu jinsi ya kutoa magazeti, mipango inaweza kufanywa ili kuwe na maonyesho yanayofaa katika eneo lenu. Kwa njia hiyo, kila mmoja anaweza kusaidiwa ajue jinsi ya kutoa habari njema kwa matokeo mazuri zaidi.

  • Habari Za Kitheokrasi
    Huduma ya Ufalme—2005 | Januari
    • Habari Za Kitheokrasi

      ◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:

      Burundi: Bugendana, Gatabo, na Muramvya.

      Kenya: Homa Bay na Lwanda Konyango.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2005 | Januari
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Des. 15

      “Katika kipindi hiki, watu ulimwenguni pote husherehekea kuzaliwa kwa Yesu kwa njia mbalimbali. Je, unajua kwamba unabii wa Biblia unahusianisha kuzaliwa kwa Yesu na amani ya milele? [Ngojea jibu. Kisha usome Isaya 9:6, 7.] Gazeti hili linaeleza jinsi amani hiyo itakavyopatikana.

      Amkeni! Des. 22

      “Je, umetambua kwamba watu hukazia sana urembo? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia hatari fulani zinazotokana na kuhangaikia sana urembo. Pia linakazia thamani ya urembo ulio bora.” Soma 1 Petro 3:3, 4.

      Mnara wa Mlinzi Jan. 1

      “Dini nyingi hufundisha kwamba ni lazima watu wapende jirani zao. [Soma Mathayo 22:39.] Unafikiri, basi, ni kwa nini vita vingi na mapigano mengi yanahusisha dini? [Ngojea jibu.] Makala hii ya Mnara wa Mlinzi inazungumzia swali hili, Je, dini inaweza kuwaunganisha wanadamu?”

      Amkeni! Jan. 8

      “Ungejibuje swali hili? [Soma swali kwenye jalada, kisha ungojee jibu.] Mali za asili za dunia zinapungua haraka sana. Hata hivyo, ona ahadi hii yenye kutia moyo. [Soma Zaburi 104:5.] Makala hii ya Amkeni! inazungumzia jinsi sayari yetu itakavyorudishwa katika hali nzuri hivi karibuni.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki