-
Kupata Matokeo Tunapohubiri Sehemu za UmmaHuduma ya Ufalme—2005 | Juni
-
-
Kupata Matokeo Tunapohubiri Sehemu za Umma
1 Kama walivyofanya wanafunzi wa kwanza wa Yesu, Wakristo leo hujitahidi kuhubiria watu habari njema popote wanapoweza kupatikana. (Mdo. 16:13; 17:17; 20:20, 21) Juhudi zao za kuhubiri sehemu za umma zimewawezesha kupata watu wanaopendezwa ambao hawangeweza kufikiwa kupitia huduma ya nyumba kwa nyumba.
2 Utambuzi unahitajiwa tunapohubiri sehemu za umma. Kwa kawaida, ingefaa kuhubiri kwa njia isiyojitokeza sana. Kwa mfano, wahubiri wengi sana wakihubiri eneo lilelile au kuzuru maduka yaleyale, huenda watu fulani wakahisi kwamba tunavuruga shughuli zao. Hilo hufanya kazi yetu idharauliwe na huenda tusipate matokeo mazuri. Tunaweza kufanya nini ili kuepuka hali hiyo? Makutaniko fulani ambayo yana maeneo mengi ya umma hupanga maeneo hayo yawe maeneo ya kibinafsi. (1 Kor. 14:40) Isitoshe, tunaweza kudumisha utaratibu kwa kuhubiri eneo la kutaniko letu tu isipokuwa kuwe na mipango hususa ambayo imefanywa kupitia Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko ili kusaidia kutaniko lingine.—Ona Huduma Yetu ya Ufalme ya Novemba 1998, uku. 5. fu. 18-19.
3 Kuwafikia Watu: Yesu alipozungumza na mwanamke kwenye kisima, alianza kwa kutaja jambo dogo tu kisha akaendeleza mazungumzo kadiri mwanamke huyo alivyozidi kuonyesha kwamba anapendezwa. (Yoh. 4:7-26) Katika hali fulani, tunaweza kufanya vivyo hivyo pia. Wahubiri fulani hupata matokeo wanapohubiri sehemu za umma kwa kutumia dakika chache kuwasalimu watu na kuwaonyesha upendezi kabla ya kuwapa ujumbe wa Ufalme. Wao hutaja habari fulani inayowavutia watu wa eneo hilo, na mara nyingi hilo huelekeza kwenye mazungumzo. Watu wanapoeleza mahangaiko yao, wahubiri hao husikiliza kwa makini. Muda si muda, wanawapa faraja kutoka katika Neno la Mungu—Rom. 15:4.
4 Kukuza Upendezi: Kila mara tunapokuwa na mazungumzo mazuri, tunapaswa kupanga kukuza upendezi huo. Tunawezaje kufanya hivyo? Mwishoni mwa mazungumzo, unaweza kutoa daftari yako na kusema: “Nimefurahia mazungumzo ambayo tumekuwa nayo. Kuna njia yoyote ya kuendeleza mazungumzo haya wakati mwingine?” Au useme: “Ningependa usome makala fulani ambayo nina hakika itakupendeza. Nikuletee nyumbani au ofisini?” Wahubiri fulani huuliza: “Unaweza kunipa namba yako ili nikupigie simu?” Mara nyingi maswali hayo huwa na matokeo mazuri.
5 Watu wengi ambao walipatikana katika sehemu za umma mara ya kwanza wamekubali kujifunza Biblia. Mafunzo hayo yanaweza kuongozwa nyumbani kwa mtu huyo, kazini kwake, mahali pa umma panapofaa, au kupitia simu. Na tuazimie kuanzisha mafunzo ya Biblia tunapohubiri sehemu za umma na kupata matokeo.
-
-
Habari Za KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2005 | Juni
-
-
Habari Za Kitheokrasi
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Burundi: Butaganzwa.
Kenya: Naivasha Mirera.
Tanzania: Muleba.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2005 | Juni
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mei 15
“Unafikiri kuna wakati ambapo hakutakuwa na umaskini ulimwenguni? [Mruhusu ajibu.] Ona ahadi ya Mungu. [Soma Isaya 65:21.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi ahadi hiyo ya Mungu itakavyotimia.” Panga kumrudia ili ujibu swali hili: Ahadi hiyo itatimizwa lini?
Amkeni! Mei 22
“Watu wengi wanajua kwamba mazoezi ni muhimu kwa afya, hata hivyo wengi wanakiri kwamba hawafanyi mazoezi ya kutosha. Je, ndivyo ilivyo? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia manufaa ya kufanya mazoezi kwa ukawaida na lina mapendekezo kuhusu jinsi tunavyoweza kufanya mazoezi licha ya shughuli nyingi tulizo nazo.”
Mnara wa Mlinzi Juni 1
“Ijapokuwa karibu kila mtu huzungumzia amani, wanadamu wameshindwa kutokeza umoja ulimwenguni. Je, unafikiri kwamba kupatikana kwa amani ulimwenguni ni ndoto tu? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia serikali inayoweza kuunganisha ulimwengu.” Soma Zaburi 72:7, 8, na upange kurudi ili kuzungumzia jinsi hilo litakavyotimizwa.
Amkeni! Juni 8
“Je, umeona kwamba watu wengi wanahangaishwa na kuongezeka kwa ugonjwa wa kansa ya ngozi? [Mruhusu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! laeleza ni kwa nini leo tumo hatarini hata zaidi na jinsi tunavyoweza kujikinga.” Malizia kwa kuzungumzia ahadi yenye kufariji iliyo katika Ayubu 33:25.
-