-
Itumie Biblia VizuriHuduma ya Ufalme—2004 | Septemba
-
-
Itumie Biblia Vizuri
1 Hata iwe tunapanga kutoa kichapo gani katika huduma, ni muhimu kuchagua andiko lenye kuchochea fikira tunaloweza kusoma pamoja na wale walio tayari kusikiliza. (Ebr. 4:12) Kuchagua andiko lililo katika kichapo unachopanga kutoa kutakuwezesha kuunganisha vizuri kichapo hicho na mazungumzo yako. Katika maeneo fulani, wahubiri wameona kwamba kuna faida ya kuibeba Biblia mkononi mwao wanapomwendea mtu ili kuzungumza naye au wanapohubiri nyumba kwa nyumba.
2 Anza kwa Andiko: Wahubiri fulani huanza mazungumzo yao kwa kumuuliza mwenye nyumba swali rahisi la maoni kuhusu andiko fulani la Biblia, kisha wanalisoma. Hilo huelekeza fikira kwenye Neno la Mungu. Je, baadhi ya matangulizi haya yanaweza kuwa na matokeo katika eneo lenu?
◼ “Ikiwa ungekuwa na uwezo, je, ungeondoa mambo haya?” Someni Ufunuo 21:4.
◼ “Kwa nini tunaishi katika nyakati hatari?” Someni 2 Timotheo 3:1-5.
◼ “Je, unafikiri kwamba eneo letu lingekuwa mahali pazuri zaidi ikiwa kila mtu angefuata shauri hili?” Someni Mathayo 7:12.
◼ “Je, unafikiri kwamba watoto wako watapata kufurahia hali zinazotajwa hapa?” Someni Zaburi 37:10, 11.
◼ “Je, unafikiri kuna siku ambayo maneno haya yatatimia?” Someni Isaya 33:24.
◼ “Je, unaelewa maana ya mapinduzi ya serikali yanayotajwa hapa?” Someni Danieli 2:44.
◼ “Je, umewahi kutaka kumuuliza Mungu swali hili?” Someni Ayubu 21:7.
◼ “Je, inawezekana kuwaona tena wapendwa wetu waliokufa?” Someni Yohana 5:28, 29.
◼ “Je, wafu wanajua mambo ambayo walio hai wanafanya?” Someni Mhubiri 9:5.
3 Fafanua, Toa Mifano, Onyesha Matumizi: Mtu akiwa tayari kuzungumza, usiharakishe mazungumzo bali chukua wakati ufafanue, utoe mifano, na kuonyesha matumizi ya andiko mlilosoma ili mtu huyo alielewe. (Neh. 8:8) Watu wanapoelewa na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu, wanaweza kufanya mabadiliko makubwa maishani mwao.—1 The. 2:13.
4 Endelea kuitumia Biblia vizuri na kuchochea upendezi wa watu. Unaweza kufanya vivyo hivyo unapofanya ziara za kurudia: (1) Chagua andiko linalofaa. (2) Uliza swali rahisi la maoni kuhusu andiko hilo. Kisha mlisome. (3) Fafanua, utoe mifano, na kuonyesha matumizi yake. Jitahidi kuongeza ujuzi wa mtu huyo kuhusu Neno la Mungu kila mara unapomtembelea. Huenda punde si punde utakuwa ukiongoza funzo la Biblia!
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2004 | Septemba
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
“Leo, watu hutafuta mashauri kuhusu ndoa na jinsi ya kuelea watoto kutoka katika vyanzo mbalimbali. Wewe unafikiri ni wapi tunapoweza kupata mashauri bora? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia baadhi ya mashauri yenye hekima kuhusu maisha ya familia yanayotolewa na Muumba wa wanadamu.” Someni Zaburi 32:8.
Amkeni! Ago. 22
“Unaonaje, je, ni muhimu akina baba wajihusishe katika maisha ya watoto wao? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia tatizo linalozidi kuongezeka la akina baba kutojihusisha katika maisha ya watoto wao. Pia linaeleza jinsi akina baba wanavyoweza kufanikisha maisha ya watoto wao.” Someni Methali 13:1.
Mnara wa Mlinzi Sept. 1
“Sisi sote tunataka kuwa na furaha. Je, unafikiri mambo yanayotajwa hapa kwa kweli yanaweza kuleta furaha? [Someni Mathayo 5:4a, 6a, 10a. Kisha mruhusu ajibu.] Gazeti hili linaeleza maana ya maneno hayo yaliyo katika yale Mahubiri ya Mlimani yanayojulikana sana, na pia mambo mengine yanayohitajiwa ili tuwe na furaha.”
Amkeni! Sept. 8
“Inakadiriwa kwamba mtu mmoja kati ya kila watu wanne atapata ugonjwa wa akili wakati fulani maishani mwake. Wengi wetu tunajua mtu fulani aliye na ugonjwa huo. [Fungua makala.] Makala hii inatoa mapendekezo mazuri kuhusu mambo tunayoweza kufanya ikiwa mtu fulani tunayempenda ana ugonjwa huo.”
-
-
Habari Za KitheokrasiHuduma ya Ufalme—2004 | Septemba
-
-
Habari Za Kitheokrasi
◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:
Burundi:Musagara, Nyamaboko, na Vumbi.
Sudan:Al Renk.
Tanzania:Kirando, Korogwe Kaskazini, Korogwe Kusini, na Makongolosi.
-