Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Deni Letu kwa Wengine
    Huduma ya Ufalme—2005 | Julai
    • Deni Letu kwa Wengine

      1 Mtume Paulo alihisi kwamba ana wajibu wa kuwahubiria watu. Alijua kwamba Yehova alikuwa amefungua njia ili watu wa namna zote waokolewe kupitia damu yenye thamani ya Mwanaye. (1 Tim. 2:3-6) Kwa hiyo, Paulo alisema: “Mimi nina deni kwa Wagiriki na kwa Wabaribari pia, kwa wenye hekima na kwa wasio na akili pia.” Alijitahidi sana kulipa deni lake kwa wanadamu wenzake kwa kuwahubiria habari njema.—Rom. 1:14, 15.

      2 Kama Paulo, Wakristo leo hujitahidi kuwahubiria majirani wao habari njema katika kila fursa. Tunapaswa kuwatafuta haraka watu wenye mioyo minyoofu kwa sababu “dhiki kubwa” inakaribia upesi. Upendo wa kweli kwa watu na utuchochee kuwa na bidii katika kazi hii ya kuokoa uhai.—Mt. 24:21; Eze. 33:8.

      3 Kulipa Deni Letu: Kuhubiri nyumba kwa nyumba ndiyo njia yetu kuu ya kuwafikia watu. Tunaweza kuzungumza na watu wengi ambao kwa kawaida hawapatikani nyumbani tukiweka rekodi sahihi na kurudi nyakati mbalimbali. (1 Kor. 10:33) Tunaweza pia kuwafikia watu kwa kuhubiri katika eneo la biashara, barabarani, katika bustani, kwenye maegesho ya magari, na kupitia simu. Ni vizuri tujiulize, ‘Je, ninajitahidi kutumia njia mbalimbali ili kuwahubiria watu ujumbe wa uzima?’—Mt. 10:11.

      4 Dada mmoja painia alihisi ana jukumu kubwa la kuwahubiria watu wote katika eneo lake. Mapazia ya nyumba moja hayakuwa yakifunguliwa, na hakuwa akimpata mtu yeyote nyumbani humo. Hata hivyo, siku moja ambayo painia huyo hakuwa katika utumishi, aliona gari mbele ya nyumba hiyo ambayo kwa kawaida haikuwa na mtu yeyote. Hakutaka kupoteza nafasi hiyo, basi akabisha hodi. Mwanamume alifungua mlango huo, na baada ya ziara ya kwanza, dada huyo na mumewe walimtembelea mtu huyo mara kadhaa. Mwishowe, mtu huyo alikubali funzo la Biblia, na sasa ni ndugu aliyebatizwa. Anashukuru kwamba dada huyo alihisi ana deni au jukumu la kuwahubiria wengine.

      5 Mwisho unapokaribia haraka, tunapaswa kulipa deni letu kwa wanadamu wenzetu sasa kwa kujitahidi kabisa katika kazi ya kuhubiri.—2 Kor. 6:1, 2.

  • Sehemu ya 11—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Julai
    • Sehemu ya 11—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      Kuwasaidia Wanafunzi Kufanya Ziara za Kurudia

      1 Mwanafunzi wa Biblia anapoanza kuhubiri, atakutana na watu wanaopendezwa na habari njema. Tunawezaje kumsaidia mhubiri mpya afanye ziara za kurudia kwa njia nzuri na kuwasaidia watu wanaopendezwa?

      2 Matayarisho kufanya ziara ya kurudia hufanywa katika ziara ya kwanza. Mtie moyo mwanafunzi apendezwe kikweli na wale anaowahubiria. (Flp. 2:4) Mzoeze hatua kwa hatua kuwatia moyo wanafunzi wajieleze, kusikiliza maelezo yao, na kutambua mambo yanayowahangaisha. Mtu akipendezwa, mwambie mhubiri huyo mpya aandike habari fulani muhimu kuhusu ziara hiyo. Tumia habari hiyo kumsaidia kujitayarisha kwa ajili ya ziara nyingine.

      3 Kujitayarisha Kurudi: Pitia habari kuhusu ziara ya kwanza, na umwonyeshe mwanafunzi jinsi ya kuchagua ujumbe fulani kuhusu Ufalme ambao utamvutia mwenye nyumba. (1 Kor. 9:19-23) Tayarisheni pamoja utangulizi mfupi unaotia ndani andiko la Biblia na pia fungu moja katika kichapo cha funzo. Vilevile, tayarisheni swali linaloweza kuulizwa mwishoni mwa mazungumzo ili liwe msingi wa ziara itakayofuata. Mwonyeshe mhubiri huyo mpya jinsi ya kumfundisha mwenye nyumba jambo fulani kutoka katika Neno la Mungu kila mara anapomtembelea.

      4 Ni vizuri pia kumzoeza mwanafunzi utangulizi mfupi wa ziara ya kurudia. Baada ya kumsalimu mwenye nyumba, anaweza kusema hivi: “Nilifurahia mazungumzo yetu ya wakati uliopita, na nimerudi ili tuzungumzie habari nyingine kutoka katika Biblia [taja habari hiyo].” Huenda ukahitaji pia kumwonyesha mhubiri huyo mpya jambo analoweza kufanya akimkuta mtu mwingine nyumbani.

      5 Kufanya Ziara za Kurudia kwa Bidii: Mtie moyo mwanafunzi huyo aweke mfano mzuri kwa kuwarudia bila kukawia wote wanaopendezwa. Ili kuwapata watu nyumbani huenda tukahitaji kurudi tena na tena. Mfundishe mwanafunzi jinsi ya kupanga ziara za kurudia, na umsaidie kuelewa umuhimu wa kurudi kama anavyoahidi. (Mt. 5:37) Mzoeze mhubiri huyo mpya kuwa mwenye fadhili, mwenye kujali, na mwenye heshima anapowatafuta wale ambao ni mfano wa kondoo na kusitawisha upendezi wao.—Tito 3:2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki