Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo
    Huduma ya Ufalme—2004 | Novemba
    • Sehemu ya 3: Kutumia Maandiko kwa Matokeo

      Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      1 Kusudi letu la kuongoza mafunzo ya Biblia ni ‘kufanya wanafunzi’ kwa kuwasaidia watu waelewe na kukubali mafundisho ya Neno la Mungu, kisha kuyatumia maishani mwao. (Mt. 28:19, 20; 1 The. 2:13) Kwa hiyo, tunapaswa kukazia Maandiko tunapoongoza funzo. Mwanzoni, huenda ikafaa kuwaonyesha wanafunzi jinsi ya kutafuta maandiko katika Biblia zao. Hata hivyo, tunawezaje kutumia Maandiko kuwasaidia wanafunzi hao wafanye maendeleo ya kiroho?

      2 Chagua Maandiko ya Kusoma: Unapojitayarisha, chunguza jinsi kila andiko lililotajwa bila kunukuliwa linavyohusiana na jambo linalozungumziwa, kisha uamue ni yapi utakayosoma na kuzungumzia wakati wa funzo. Kwa kawaida, itafaa kusoma yale yanayoonyesha msingi wa imani yetu. Si lazima usome maandiko yanayotoa habari za ziada. Fikiria mahitaji na hali za kila mwanafunzi.

      3 Tumia Maswali: Badala ya kumfafanulia mwanafunzi maandiko ya Biblia, mwache yeye akufafanulie. Unaweza kumchochea afanye hivyo kwa kutumia maswali kwa ustadi. Ikiwa maana na matumizi ya andiko ni wazi, unaweza kumwuliza jinsi andiko hilo linavyounga mkono jambo linalozungumziwa kwenye fungu. Kuhusu maandiko mengine, huenda ukahitaji kuuliza swali fulani hususa au maswali kadhaa ili kumsaidia mwanafunzi apate kuelewa maana ya maandiko hayo. Ikiwa unahitaji kueleza zaidi, unaweza kufanya hivyo baada ya mwanafunzi kutoa maelezo yake.

      4 Usieleze Mambo Mengi: Mara nyingi mpiga-mishale stadi huhitaji kutumia mshale mmoja tu ili kulenga shabaha. Vivyo hivyo, mwalimu stadi hahitaji kutumia maneno mengi ili kukazia jambo fulani. Anaweza kueleza jambo kwa njia rahisi, iliyo wazi, na sahihi. Huenda wakati mwingine ukahitaji kufanya utafiti katika vichapo vya Kikristo ili kuelewa andiko fulani na kulieleza kwa usahihi. (2 Tim. 2:15) Lakini epuka kujaribu kueleza kila jambo katika andiko wakati wa funzo. Eleza tu yale yanayohusiana na jambo linalozungumziwa.

      5 Onyesha Jinsi ya Kutumia Maandiko: Inapofaa, msaidie mwanafunzi aone jinsi anavyoweza kutumia maandiko katika maisha yake. Kwa mfano, unapozungumzia andiko la Waebrania 10:24, 25 pamoja na mwanafunzi ambaye bado hajaanza kuhudhuria mikutano ya Kikristo, unaweza kutaja mojawapo ya mikutano na kumwalika ahudhurie. Usifanye mwanafunzi ahisi kama analazimishwa kuhudhuria. Badala yake, acha Neno la Mungu limchochee kuchukua hatua inayohitajiwa ili kumpendeza Yehova.—Ebr. 4:12.

      6 Tunapotimiza kazi yetu ya kufanya wanafunzi, na ‘tuendeleze utii kwa njia ya imani’ kwa kutumia Maandiko kwa matokeo.—Rom. 16:26.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2004 | Novemba
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Okt. 15

      “Watu fulani huamini kwamba wakiwa na pesa nyingi watakuwa na maisha yenye kuridhisha. Je, unafikiri hiyo ni kweli? [Ngoja jibu.] Ona jinsi mwanamume aliyekuwa tajiri sana alivyoandika. [Soma Mhubiri 5:10.] Gazeti hili linazungumzia kanuni zenye thamani kuliko utajiri.”

      Amkeni! Okt. 22

      “Watu wengi wanaona umuhimu wa kuwazoeza watoto tangu wakiwa wachanga. Je, unaona uhitaji wa kufanya hivyo leo? [Ngoja jibu. Kisha soma Methali 22:6.] Gazeti hili la Amkeni! linazungumzia mambo hususa ambayo wazazi wanaweza kufanya ili kuwasaidia watoto wao wawe watu wazima wanyofu na wenye mafanikio.”

      Mnara wa Mlinzi Nov. 1

      “Watu wengi hawaamini kwamba viongozi wa kibinadamu wana uwezo wa kutatua matatizo ya sasa. Je, unafikiri kuna yeyote anayeweza kutimiza yale yaliyotabiriwa katika mistari hii? [Soma Zaburi 72:7, 12, 16. Kisha ungoje jibu.] Gazeti hili linaeleza kiongozi huyo aliyetabiriwa ni nani na atatimiza nini.”

      Amkeni! Nov. 8

      “Watoto wanahitaji mwongozo ili kukabiliana na mikazo wanayopata leo, sivyo? [Ngoja jibu. Kisha soma Waefeso 6:4.] Gazeti hili linazungumzia maana halisi ya nidhamu. Pia linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwaongoza na kuwarekebisha watoto wao bila kuwavunja moyo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki