Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sehemu ya 7—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Machi
    • Sehemu ya 7—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      Kutoa Sala Wakati wa Funzo

      1 Baraka ya Yehova ni muhimu ili mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. (1 Kor. 3:6) Kwa hiyo inafaa kuanza na kumalizia funzo kwa sala. Nyakati nyingine tunaweza kutoa sala hata tunapojifunza kwa mara ya kwanza pamoja na wanadini. Lakini tunapoongoza funzo pamoja na wanafunzi wengine huenda tukahitaji kutumia busara ili tutambue wakati unaofaa wa kuanza kutoa sala. Unaweza kutumia Zaburi 25:4, 5 na 1 Yohana 5:14 kumsaidia mwanafunzi kuelewa kwa nini tunapaswa kusali, na Yohana 15:16 ili kueleza umuhimu wa kusali kwa Yehova katika jina la Yesu Kristo.

      2 Ni nani anayepaswa kutoa sala wakati wa funzo la Biblia? Ikiwa ndugu aliyebatizwa anaandamana na dada kwenye funzo, ndugu ndiye anayepaswa kutoa sala. Hata hivyo, dada anaweza kuongoza funzo akiwa amefunika kichwa. (1 Kor. 11:5, 10) Kwa upande mwingine, ikiwa mhubiri mwanamume ambaye hajabatizwa anaandamana na dada aliyebatizwa kwenye funzo, dada ndiye anayepaswa kutoa sala. Katika kisa kama hicho, dada anapaswa kufunika kichwa anapotoa sala na anapoongoza funzo.

      3 Mambo Unayoweza Kutaja Katika Sala: Si lazima utoe sala ndefu kwenye funzo la Biblia, lakini unapaswa kutaja mambo hususa. Mbali na kumwomba Mungu abariki funzo na kumshukuru kwa kweli mlizojifunza, inafaa kumsifu Yehova kwa sababu yeye ndiye Chanzo cha mafundisho hayo. (Isa. 54:13) Tunaweza pia kutaja mambo yanayoonyesha kwamba tunamjali sana mwanafunzi na tunathamini tengenezo ambalo Yehova hutumia. (1 The. 1:2, 3; 2:7, 8) Tunapomwomba Yehova abariki jitihada za mwanafunzi za kuishi kupatana na yale anayojifunza, huenda akaona umuhimu wa kuwa ‘mtendaji wa neno.’—Yak. 1:22.

      4 Kuna faida nyingi za kusali wakati wa funzo. Sala hutuletea baraka za Mungu. (Luka 11:13) Umuhimu wa kujifunza Neno la Mungu hukaziwa tunaposali. Mwanafunzi hujifunza jinsi ya kusali anaposikiliza sala zetu. (Luka 6:40) Zaidi ya hayo, sala zinazotoka katika moyo uliojaa upendo kwa Mungu na shukrani kwa sifa zake zisizo na kifani zinaweza kumsaidia mwanafunzi kuwa na uhusiano wa karibu pamoja na Yehova.

  • Habari Za Kitheokrasi
    Huduma ya Ufalme—2005 | Machi
    • Habari Za Kitheokrasi

      ◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:

      Kenya: Cherengani, Mwimuto, na Uplands.

      Tanzania: Igamba na Mbeya Isanga.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2005 | Machi
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Feb. 15

      “Mara kwa mara tunasikia habari kwamba mwujiza umetukia. [Taja kisa kimoja.] Watu fulani hutilia shaka habari hizo, na wengine huziamini. Gazeti hili linazungumzia kama tunaweza kuwa na hakika kwamba miujiza inayotajwa katika Biblia ilitukia, na kama miujiza hutukia leo.” Soma Yeremia 32:21.

      Amkeni! Feb. 22

      “Zamani za kale, Mungu aliwaamuru watoto waheshimu mama na baba. [Soma Kutoka 20:12.] Je, unafikiri kwamba akina mama wanaheshimiwa ifaavyo leo? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia magumu ambayo akina mama katika nchi mbalimbali wanakabili na jinsi wanavyopambana na magumu hayo.”

      Mnara wa Mlinzi Mac. 1

      “Je, unafikiri kwamba hali ya ulimwengu ingekuwa bora ikiwa watu wangefuata ushauri huu? [Soma Waroma 12:17, 18, kisha ngojea jibu.] Jambo la kusikitisha ni kwamba kutoelewana hutokea mara kwa mara. Gazeti hili linaonyesha jinsi ushauri wa Biblia unavyoweza kutusaidia kusuluhisha ugomvi na kufanya amani.”

      Amkeni! Mac. 8

      “Uhitaji wa nishati huongezeka kila mwaka. Je, unaweza kuwazia jinsi ambavyo hali ingekuwa ikiwa vyanzo vya nishati kama vile petroli vingeisha? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia maendeleo ambayo yamefanywa ili kupata nishati bila kuchafua mazingira. Linazungumzia pia yule ambaye ni chanzo cha nishati yote.” Soma Isaya 40:26.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki