-
Sehemu ya 8—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye MaendeleoHuduma ya Ufalme—2005 | Aprili
-
-
Sehemu ya 8—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
Kuwaelekeza Wanafunzi Kwenye Tengenezo
1 Tunapoongoza mafunzo ya Biblia, lengo letu si kuwafundisha wanafunzi mafundisho ya msingi tu, bali pia kuwasaidia wawe sehemu ya kutaniko la Kikristo. (Zek. 8:23) Tunaweza kutumia broshua Mashahidi wa Yehova–Wao Ni Nani? Wanaamini Nini? ili kutimiza lengo hilo. Waachie wanafunzi wapya wa Biblia broshua hiyo na uwatie moyo kuisoma. Pia, tumia dakika chache kila juma wakati wa funzo kuwaeleza jambo fulani kuhusu tengenezo la Yehova.
2 Mikutano ya Kutaniko: Kushirikiana nasi katika mikutano ya kutaniko ni njia muhimu zaidi ya kuwasaidia wanafunzi kulifahamu tengenezo la Mungu. (1 Kor. 14:24, 25) Hivyo, wajulishe wanafunzi kuhusu mikutano yetu mitano kwa kuzungumzia mkutano mmojammoja unapowatembelea. Watajie kichwa cha hotuba ya watu wote itakayotolewa. Waonyeshe habari itakayozungumziwa katika Funzo la Mnara wa Mlinzi, na katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Waeleze kuhusu Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na Mkutano wa Utumishi. Ikiwa una hotuba katika shule unaweza kufanya mazoezi ya hotuba hiyo pamoja nao. Waambie mambo makuu yaliyozungumziwa katika mikutano. Waonyeshe picha zilizo katika vichapo vyetu ili kuwasaidia kuelewa jinsi mikutano yetu inavyofanywa. Mwanzoni kabisa, wakati unapoanzisha funzo, waalike kwenye mikutano.
3 Ukumbusho, makusanyiko, na ziara ya mwangalizi wa mzunguko inapokaribia, tumia dakika chache kuwaeleza wanafunzi kuhusu mipango hiyo ili waithamini. Hatua kwa hatua jibu maswali kama vile: Kwa nini tunaitwa Mashahidi wa Yehova? Kwa nini tunaita mahali tunapofanyia mikutano yetu Jumba la Ufalme? Wazee na watumishi wa huduma hufanya kazi gani? Kazi ya kuhubiri na maeneo tunayohubiri hupangwaje? Vichapo vyetu hutengenezwaje? Pesa za kuendesha shughuli za tengenezo zinatoka wapi? Ofisi ya tawi na Baraza Linaloongoza husimamiaje kazi yetu?
4 Video Zenye Mafundisho: Tunaweza pia kuwafundisha wanafunzi kuhusu tengenezo la Yehova lenye kuvutia kwa kutumia video zetu. Video To the Ends of the Earth, inaonyesha jinsi tunavyohubiri ulimwenguni pote; Our Whole Association of Brothers, inaonyesha udugu wetu wa ulimwenguni pote; na United by Divine Teaching, inaonyesha umoja uliopo miongoni mwa Mashahidi wa Yehova. Mwanamke aliyepokea magazeti na vichapo vyetu vingine kwa kipindi cha miaka mitano alitokwa na machozi alipoitazama ile video Jehovah’s Witnesses—The Organization Behind the Name. Aliwatumaini Mashahidi waliokuwa wakimtembelea, lakini baada ya kuitazama video hiyo alihisi kwamba anaweza pia kulitumaini tengenezo. Alianza kujifunza, na juma lililofuata akahudhuria mikutano katika Jumba la Ufalme.
5 Tukitumia vichapo tulivyo navyo kwa dakika chache kila juma, tunaweza kuwaelekeza wanafunzi wa Biblia hatua kwa hatua kwenye tengenezo ambalo Yehova hutumia leo.
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu MagazetiHuduma ya Ufalme—2005 | Aprili
-
-
Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Mac. 15
“Watu ulimwenguni pote husifu mafundisho ya Yesu. [Soma nukuu iliyo katika ukurasa wa 3, fungu la kwanza.] Lakini je, unafikiri kwamba mafundisho ya Yesu, kama lile linalopatikana katika andiko hili, yanafaa hali zetu leo? [Soma Mathayo 5:21, 22a, kisha ungoje jibu.] Gazeti hili linazungumzia mafundisho ya Yesu na jinsi yanavyoweza kutufaidi.”
Amkeni! Mac. 22
“Watu wengi hupendezwa na milima kwa kuwa ni maridadi, lakini unajua kwamba milima ni muhimu kwa uhai? [Ngojea jibu.] Gazeti hili huzungumzia umuhimu wa milima na matatizo yanayoikabili. Pia linaeleza jinsi Muumba atakavyookoa milima.” Soma Zaburi 95:4.
Mnara wa Mlinzi Apr. 1
“Je, umewahi kuwasikia watu wakisema kwamba sayansi na Biblia zinapingana? [Ngojea jibu.] Gazeti hili linazungumzia mabishano ya muda mrefu kati ya sayansi na dini. Isitoshe, linaonyesha jinsi sayansi ya kweli inavyopatana na Biblia.” Mwonyeshe ukurasa wa 6-7, kisha usome Mhubiri 1:7.
Amkeni! Apr. 8
“Wazazi wanaweza kuwasaidiaje watoto wao waepuke matatizo katika miaka migumu ya ujana? [Ngojea jibu, kisha usome Isaya 48:17, 18.] Gazeti hili linaonyesha jinsi wazazi wanavyoweza kufuata ushauri wa Biblia ili kuboresha mawasiliano kati yao na watoto wao na jinsi ya kuwawekea mipaka inayofaa.”
-