Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia
    Huduma ya Ufalme—2005 | Juni
    • Kuhubiri Hutusaidia Kuvumilia

      1 Neno la Mungu linatuhimiza “tukimbie kwa uvumilivu shindano la mbio lililowekwa mbele yetu.” (Ebr. 12:1) Kama mkimbiaji anavyohitaji kuvumilia ili amalize mbio, ndivyo tunavyohitaji kuvumilia ili tupate zawadi ya uzima wa milele. (Ebr. 10:36) Huduma ya Kikristo inaweza kutusaidiaje kuvumilia kwa uaminifu mpaka mwisho?—Mt. 24:13.

      2 Tunaimarishwa Kiroho: Kutangaza ahadi nzuri ya Biblia kuhusu ulimwengu mpya wenye uadilifu hutusaidia kudumisha uhakika wa tumaini letu wenyewe. (1 The. 5:8) Tunapohubiri kwa ukawaida, tunakuwa na fursa ya kuwajulisha wengine kweli ambazo tumejifunza kutoka katika Biblia. Tunapata fursa ya kuitetea imani yetu, na kufanya hivyo hutuimarisha kiroho.

      3 Ni lazima tuelewe waziwazi kweli za Biblia ili tuweze kuwafundisha wengine vizuri. Tunahitaji kufanya utafiti na kutafakari kuhusu habari hiyo. Tunapojitahidi kufanya hivyo, ujuzi wetu unaongezeka, imani yetu inaimarika, na tunapata nguvu mpya ya kiroho. (Met. 2:3-5) Kwa hiyo, tunapojitahidi kuwasaidia wengine, tunajiimarisha sisi wenyewe.—1 Tim. 4:15, 16.

      4 Kuhubiri kwa bidii ni sehemu muhimu ya “mavazi kamili ya silaha kutoka kwa Mungu,” ambayo tunahitaji ili kusimama imara dhidi ya Ibilisi na roho wake waovu. (Efe. 6:10-13, 15) Kujishughulisha sana na utumishi mtakatifu hutusaidia kukazia akilini mwetu mambo yanayojenga na kuepuka kuchafuliwa na ulimwengu wa Shetani. (Kol. 3:2) Tunapowafundisha wengine njia za Yehova, tunakumbushwa daima kwamba sisi pia tunahitaji kudumisha mwenendo mtakatifu.—1 Pet. 2:12.

      5 Mungu Anatutia Nguvu: Hatimaye, kushiriki katika kazi ya kueneza injili hutufundisha kumtegemea Yehova. (2 Kor. 4:1, 7) Ni baraka iliyoje! Kusitawisha sifa hiyo ya kumtegemea Yehova hutusaidia kutimiza huduma yetu na vilevile kukabiliana na hali yoyote maishani. (Flp. 4:11-13) Kwa kweli, kujifunza kumtegemea Yehova kabisa ndio msingi wa kuvumilia. (Zab. 55:22) Kuhubiri hutusaidia katika njia nyingi kuvumilia.

  • Sehemu ya 10—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Juni
    • Sehemu ya 10—Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

      Kuwazoeza Wanafunzi Katika Huduma ya Nyumba kwa Nyumba

      1 Wazee wanapoona kwamba mwanafunzi wa Biblia anastahili kuwa mhubiri ambaye hajabatizwa, mwanafunzi huyo anaweza kuanza kushiriki na kutaniko katika kazi ya kuhubiri hadharani. (Ona Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, uku. 79-81.) Tunawezaje kumzoeza mwanafunzi kuhubiri nyumba kwa nyumba?

      2 Kutayarisha Pamoja: Ni lazima ajitayarishe vizuri ili afaulu. Mwonyeshe mwanafunzi mahali ambapo anaweza kupata utangulizi katika Huduma Yetu ya Ufalme na kitabu Kutoa Sababu, na umsaidie kuchagua utangulizi rahisi ambao unafaa eneo lenu. Tangu mwanzo, mtie moyo atumie Biblia katika huduma yake.—2 Tim. 4:2.

      3 Vipindi vya mazoezi humsaidia sana mhubiri mpya. Mwanafunzi anapojizoeza kutoa utangulizi, mwonyeshe jinsi ya kushughulikia kwa busara itikio la watu katika eneo lenu. (Kol. 4:6) Mhakikishie kwamba si lazima wahudumu Wakristo wajue jibu la kila swali ambalo huenda mwenye nyumba akauliza. Mara nyingi ni vizuri kumwambia mwenye nyumba kwamba ungependa kufanya utafiti kuhusu swali lake na utarudi baadaye kuzungumzia habari hiyo zaidi.—Met. 15:28.

      4 Kuhubiri Pamoja: Mwanafunzi anaposhiriki kwa mara ya kwanza katika huduma ya nyumba kwa nyumba, mwache aangalie jinsi unavyotoa utangulizi ambao mlitayarisha pamoja. Halafu mshirikishe. Nyakati nyingine, huenda ikafaa kwa mwanafunzi huyo mpya kushiriki kidogo kwa kusoma andiko na kulifafanua. Zingatia utu na uwezo wa mwanafunzi. (Flp. 4:5) Mpongeze sana unapoendelea kumzoeza katika sehemu mbalimbali za kazi ya kuhubiri.

      5 Ni muhimu kumsaidia mhubiri mpya kuwa na ratiba ya kushiriki kwa ukawaida katika huduma, na afanye hivyo kila juma ikiwezekana. (Flp. 3:16) Fanyeni mipango hususa ya kushiriki pamoja katika utumishi, na umtie moyo ahubiri pia na wahubiri wengine wenye bidii. Kielelezo chao na ushirika wao utamsaidia kuwa stadi na kupata shangwe katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki