Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Sitawisha Upendezi wa Watu Unaowapelekea Magazeti kwa Ukawaida
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Sitawisha Upendezi wa Watu Unaowapelekea Magazeti kwa Ukawaida

      1 Watu wengi tunaowakuta katika huduma hutukaribisha na kukubali vichapo vyetu, lakini husita kukubali funzo la Biblia la kawaida. Njia moja ya kusitawisha upendezi wao ni kwa kuwapelekea magazeti kwa ukawaida. Unapomwachia mtu magazeti, andika jina na anwani yake, tarehe uliyomtembelea, magazeti aliyochukua, andiko mlilozungumzia, na jambo lingine lolote lililokusaidia kutambua mambo yanayompendeza mtu huyo. Unapopata magazeti mapya, yasome na utafute mambo ambayo yatawavutia wale unaowapelekea magazeti kwa ukawaida, kisha uzungumzie mambo hayo unapowatembelea. (1 Kor. 9:19-23) Baada ya muda, huenda wakavutiwa na jambo fulani katika magazeti yetu na wakataka kujifunza zaidi.

      2 Hata hivyo, tunatambua kwamba watu wengi hawatakuwa watumishi wa Yehova kwa kusoma magazeti tu. Kwa kuwa ni muhimu watu wamtafute Yehova sasa, tunaweza kuwasaidiaje wafanye hivyo? (Sef. 2:2, 3; Ufu. 14:6, 7) Tunaweza kusitawisha upendezi wao kwa kusoma nao andiko moja ambalo tumelichagua kwa uangalifu kila wakati tunapowapelekea magazeti.

      3 Kuzungumzia Andiko Moja: Fikiria wale unaowapelekea magazeti kwa ukawaida, kisha utayarishe mazungumzo yanayotegemea andiko moja ambalo mtazungumzia na kila mmoja wao ikitegemea mahitaji yake. (Flp. 2:4) Kwa mfano, ikiwa mmoja wao amefiwa na mpendwa wake, unaweza kumrudia mara kadhaa ili mzungumzie yale ambayo Biblia inasema kuhusu hali ya wafu na tumaini la ufufuo. Maelezo yanayopatikana katika kitabu Kutoa Sababu chini ya kichwa “Kifo” na “Ufufuo” yanaweza kutumiwa kutayarisha mazungumzo yanayotegemea andiko moja. Baadaye huenda ikawa rahisi kuendelea na mazungumzo kwa kuzungumzia mambo kama vile kuondolewa kabisa kwa ugonjwa, uzee, na kifo. Nia yetu ni kutafuta jambo linalomvutia mtu na kumwonyesha maoni ya Biblia kulihusu hatua kwa hatua.

      4 Wasaidie Waelewe: Ingawa ni vizuri kuwa na mazungumzo mafupi na rahisi, kusoma tu andiko ulilochagua hakutoshi. Shetani amepofusha fikira za watu ili wasielewe habari njema. (2 Kor. 4:3, 4) Hata wale wanaojua mambo fulani katika Biblia wanahitaji kusaidiwa kuielewa. (Mdo. 8:30, 31) Kwa hiyo, fafanua na ueleze andiko hilo vizuri, kama vile ungefanya ikiwa ungekuwa ukitoa hotuba katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi. (Mdo. 17:3) Hakikisha kwamba mtu huyo amejua jinsi Neno la Mungu linavyoweza kumnufaisha maishani.

      5 Ikiwa mtu huyo anafurahia mambo anayojifunza, hatua kwa hatua ongeza idadi ya maandiko mnayozungumzia kila mara unapomtembelea. Unaweza kuzungumzia maandiko mawili au matatu zaidi. Tafuta fursa ya kuzungumzia broshua Anataka au kitabu Ujuzi. Kwa njia hiyo, mtu huyo ambaye umekuwa ukimpelekea magazeti kwa ukawaida, huenda hatimaye akawa mwanafunzi wa Biblia.

  • Habari Za Kitheokrasi
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Habari Za Kitheokrasi

      ◼ Majumba ya Ufalme yafuatayo yaliwekwa wakfu hivi karibuni:

      Kenya: Nakuru London.

      Tanzania: Chunya Mjini, Lugufu Two Malagarisi (Kambi ya Wakimbizi), na Tanga Magharibi.

      Uganda: Ibanda, Kampala Naguru, na Kampala Nateete.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2005 | Mei
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Apr. 15

      “Je, unafikiri kwamba leo kuna habari nyingi kupita kiasi? [Ngojea jibu.] Hata hivyo, hakuna habari muhimu zaidi kuliko ile inayopatikana katika mstari huu. [Soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linaeleza maana ya ‘uzima wa milele’ na jinsi tunavyoweza kupata ujuzi unaoongoza kwenye uzima huo.”

      Amkeni! Apr. 22

      “Ingawa huenda Yesu Kristo ndiye mtu anayejulikana zaidi aliyepata kuishi, watu wengi wangetaka kumfahamu vizuri. Je, unajua kwamba hata wafuasi wake mwenyewe hawakumfahamu vizuri? [Ngojea jibu, kisha usome Marko 4:41.] Gazeti hili linaeleza kile ambacho Biblia inasema kuhusu utambulisho kamili wa Yesu.”

      Mnara wa Mlinzi Mei 1

      “Wakati mpendwa anapokufa, tunatamani kumwona tena, sivyo? [Ngojea jibu.] Watu wengi wamepata faraja kupitia ahadi ya ufufuo inayopatikana katika Biblia. [Soma Yohana 5:28, 29.] Gazeti hili linazungumzia wakati ambapo ufufuo utatukia na wale watakaofufuliwa.”

      Amkeni! Mei 8

      “Wazazi wengi huwachagulia watoto wao sinema watakazotazama. Je, umeona kuwa ni vigumu kupata sinema zinazofaa kwa ajili ya familia yako? [Ngojea jibu, kisha usome Waefeso 4:17.] Gazeti hili linazungumzia jinsi wazazi wanavyoweza kuwasaidia watoto wao wachague sinema zinazofaa.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki