-
Kuwatia Moyo na Kuwatia Nguvu WasikilizajiFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
nguvu kutawasaidia kutambua wazi kwamba Yehova anawajali na kwamba kwa kweli atawasaidia wanapokabili majaribu yoyote wakati huu.—Isa. 41:10, 13; 1 Pet. 5:7.
Furahia Matendo ya Mungu Sasa. Unapotaka kuwatia moyo ndugu zako, waonyeshe mambo ambayo Yehova anafanya sasa. Ukizungumzia mambo hayo kwa furaha, utawachochea wasikilizaji pia wayafurahie katika mioyo yao.
Zungumzia jinsi Yehova anavyotusaidia kushinda mikazo ya maisha. Anatuonyesha njia bora zaidi ya kuishi. (Isa. 30:21) Anatueleza chanzo cha uhalifu, ukosefu wa haki, umaskini, ugonjwa, na kifo na kutuambia jinsi atakavyokomesha mambo hayo yote. Ametuzingira kwa udugu wenye upendo. Ametupatia pendeleo kubwa la sala. Ametukabidhi pendeleo la kuwa Mashahidi wake. Ametufunulia kwamba tayari Kristo ametawazwa mbinguni na kwamba siku za mwisho za mfumo huu wa kale zinamalizika upesi.—Ufu. 12:1-12.
Mbali na baraka hizo, kuna mikutano ya kutaniko na makusanyiko. Unapozungumzia maandalizi hayo kwa njia inayoonyesha unayathamini sana, utatia nguvu azimio la wengine la kukusanyika pamoja na akina ndugu bila kukosa.—Ebr. 10:23-25.
Tunatiwa nguvu pia na ripoti zinazothibitisha kwamba kwa kweli Yehova anabariki jitihada zetu katika huduma ya shambani. Katika karne ya kwanza wakati Paulo na Barnaba walipokuwa njiani kuelekea Yerusalemu, ‘walisababisha shangwe kubwa kwa akina ndugu wote’ kwa kuwasimulia kwa undani jinsi watu wa mataifa walivyogeuka. (Mdo. 15:3) Wewe pia unaweza kuwapa akina ndugu shangwe kwa kuwasimulia mambo yaliyoonwa yanayopendeza.
Watu hutiwa moyo zaidi wanaposaidiwa kuona umuhimu wa utendaji wao. Wapongeze kwa kazi wanayofanya katika huduma ya Kikristo. Wapongeze wale ambao utendaji wao umepungua kwa sababu ya uzee au ugonjwa lakini bado wanaendelea kuvumilia kwa uaminifu. Wakumbushe kwamba Yehova hasahau upendo ambao wameonyesha kwa ajili ya jina lake. (Ebr. 6:10) Imani inayothibitishwa na jaribu ni bora sana. (1 Pet. 1:6, 7) Akina ndugu wanahitaji kukumbushwa jambo hilo.
Zungumza kwa Hisia Kuhusu Tumaini la Wakati Ujao. Ahadi za Mungu za mambo yajayo huwatia moyo sana wote wanaompenda. Labda wengi miongoni mwa wasikilizaji wamesikia ahadi hizo. Lakini unaweza kufanya baraka hizo ziwe halisi kwa kuzizungumzia kwa uthamini sana, na kuwahakikishia wasikilizaji kwamba zitatimizwa, na kufanya mioyo yao ijae shukrani. Kutumia mambo ambayo umejifunza katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi kunaweza kukusaidia kutimiza jambo hilo.
Yehova mwenyewe ndiye Chanzo kikuu cha kitia-moyo na nguvu. Lakini unaweza kushirikiana naye kuwatia moyo wengine na kuwapa nguvu. Unapohutubia kutaniko, tumia vizuri pindi hiyo kuwatia moyo na kuwapa nguvu akina ndugu.
-
-
Endelea Kufanya MaendelioFaidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
-
-
Endelea Kufanya Maendelio
JE, UMEFANYIA kazi kila shauri katika programu hii ya shule? Je, pia umemaliza mazoezi yanayoonyeshwa? Je, unatumia kila sha-uri unapotoa hotuba, katika shule au katika mikutano mingine, na unapokuwa katika utumishi wa shambani?
Endelea kufaidika na elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokra-si. Hata kama umetoa hotuba kwa muda mrefu kadiri gani, kuna sehemu ambazo unaweza kufanyia maendeleo zaidi.
-