Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Matangazo
    Huduma ya Ufalme—2005 | Novemba
    • Matangazo

      ◼ Novemba: Tutatoa kitabu Jifunze Kutoka kwa Mwalimu Mkuu. Mwenye nyumba akisema hana watoto, mtolee kitabu Ujuzi au trakti Je, Ungependa Kujua Mengi Zaidi Kuhusu Biblia? Desemba: Tutatoa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi. Unaweza kutoa vitabu vingine kama Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia, au Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani iwapo vinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiswahili inaweza kutolewa pia. Januari 2006: Tutatoa kitabu chochote cha kurasa 192 chenye karatasi inayochujuka, au kitabu chochote kilichochapishwa kabla ya mwaka wa 1991. Makutaniko yasiyo na vitabu hivyo vya zamani akibani yanaweza kutoa kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu ikiwa kinapatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiswahili inaweza kutolewa pia. Februari: Tutatoa kitabu Mkaribie Yehova. Makutaniko ambayo hayana kitabu hicho yanaweza kutoa kitabu kingine cha zamani kinachopatikana kutanikoni. Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo katika Kiswahili inaweza kutolewa pia.

      ◼ Mwangalizi-msimamizi au ndugu fulani aliyeteuliwa naye anapaswa kukagua hesabu za kutaniko mnamo Desemba 1, au upesi iwezekanavyo baada ya tarehe hiyo. Ikiwa kuna akaunti nyingine ya benki, kama vile akaunti ya ujenzi au ya udumishaji wa Jumba la Ufalme, mipango inapaswa kufanywa ili kuzikagua. Ukaguzi ukikamilishwa, kutaniko linapaswa kutangaziwa ripoti ya ukaguzi pamoja na ripoti ya hesabu itakayofuata.

      ◼ Mwandishi wa kila kutaniko ambalo lina Jumba la Ufalme anapaswa kuhakikisha kwamba wameondolewa wajibu wa kulipa ushuru au kodi kwa ajili ya Jumba la Ufalme ikiwa wajibu huo unaweza kuondolewa.

      ◼ Kuanzia juma la Aprili 17, 2006, tutajifunza kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa? katika Funzo la Kitabu la Kutaniko. Makutaniko yanapaswa kuwa na idadi ya kutosha ya chapa ya kawaida na chapa kubwa ya kitabu hicho kufikia wakati huo.

      ◼ Video inayoitwa Transfusion Alternative Health Care—Meeting Patient Needs and Rights itazungumziwa katika Mkutano wa Utumishi mwezi wa Januari. Ikihitajiwa, video hiyo inaweza kuombwa kupitia kutaniko haraka iwezekanavyo.

  • Tunaweza Kusaidiaje?
    Huduma ya Ufalme—2005 | Novemba
    • Tunaweza Kusaidiaje?

      1 Swali hili: “Tunaweza kusaidiaje?” huulizwa mara nyingi na Mashahidi wa Yehova wanaposikia kuhusu msiba ambao umetokea katika eneo fulani ulimwenguni. Andiko la Matendo 11:27-30 linaonyesha kwamba Wakristo katika karne ya kwanza walitoa msaada ili kuwasaidia ndugu zao waliokumbwa na njaa huko Yudea.

      2 Katika nyakati zetu, sheria zinazohusu tengenezo letu zinaturuhusu kutumia fedha ili kuandaa msaada kwa ajili ya watu wanaokumbwa na misiba ya asili au ile inayosababishwa na wanadamu. Zinaturuhusu pia kutumia fedha hizo nyakati nyingine za uhitaji.

      3 Kwa mfano, mwaka uliopita ndugu wengi walitoa msaada kwa ajili ya wale walioathiriwa na tsunami huko Asia Kusini. Hatua hiyo ya huruma ya kutoa michango ili kuandaa msaada inathaminiwa sana. Hata hivyo, kulingana na sheria za nchi fulani, michango inapotolewa kwa ajili ya msiba fulani mahususi, fedha hizo zinapaswa kutumiwa tu kwa kusudi ambalo mfadhili ametaja na katika kipindi fulani cha wakati, hata kama mahitaji ya ndugu zetu katika eneo linalohusika yamekwisha timizwa.

      4 Kwa hiyo, inapendekezwa kwamba michango kwa ajili ya msaada iwekwe katika sanduku la michango ya kazi ya ulimwenguni pote. Hazina hiyo hutumiwa kutoa msaada na pia kushughulikia mahitaji ya kiroho ya ndugu zetu Wakristo. Ikiwa kwa sababu fulani mtu anataka kutoa mchango kwa kusudi tu la kuwasaidia akina ndugu, mchango wake utakubaliwa na kutumiwa kokote unakohitajiwa. Hata hivyo, ingefaa kama michango hiyo ingetolewa bila masharti ya jinsi itakavyotumiwa au mahali itakapotumiwa.

      5 Tunapotoa michango yetu hasa kwa ajili ya kazi ya ulimwenguni pote, tunakuwa na fedha zaidi za kutumia katika kazi zote zinazohusiana na Ufalme, badala ya kuhifadhi michango fulani kwa ajili tu ya kuandaa msaada wakati ujao. Hilo linapatana na andiko la Waefeso 4:16 linalotuhimiza tushirikiane kutoa kinachohitajiwa kwa ajili ya “ukuzi wa mwili ili huo ujijenge wenyewe katika upendo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki