Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kwa Nini Ubatizwe?
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Aprili 1
    • 15. Kwa nini wanaotaka kubatizwa huzamishwa katika maji?

      15 Tunapojiweka wakfu kwa Mungu kupitia Kristo, tunadhihirisha azimio letu la kutumia maisha yetu kufanya mapenzi ya Mungu kama yanavyoonyeshwa katika Maandiko. Wanaotaka kubatizwa huonyesha wakfu wao kwa kubatizwa katika maji, kama vile Yesu alivyobatizwa katika Mto Yordani kuonyesha kwamba amejitoa kwa Mungu. (Mathayo 3:13) Twapasa kutambua kwamba Yesu alikuwa akisali wakati huo muhimu.—Luka 3:21, 22.

      16. Tunaweza kuonyeshaje shangwe yetu kwa njia inayofaa tunapoona watu wakibatizwa?

      16 Mbali na kuwa tukio muhimu sana, ubatizo wa Yesu ulileta shangwe nyingi. Ndivyo ilivyo na ubatizo wa Kikristo leo. Tunapoona watu wakionyesha wakfu wao kwa Mungu, twaweza kuonyesha shangwe yetu kwa kupiga makofi na kutoa pongezi changamfu kwa heshima. Lakini hatushangilii kwa vigelegele au kupiga mbinja, kwa kuwa tunaheshimu tukio hilo takatifu la kudhihirisha imani. Tunaonyesha shangwe yetu kwa njia ya heshima.

      17, 18. Ni nini kinachosaidia kuamua kama mtu anastahili kubatizwa?

      17 Tofauti na watu ambao huwanyunyizia maji watoto wachanga, au kulazimisha watu wasio na ujuzi wa Biblia wabatizwe, Mashahidi wa Yehova hawalazimishi mtu yeyote kamwe abatizwe. Hata hawabatizi watu wasiostahili kiroho. Hata kabla mtu hajawa mhubiri asiyebatizwa wa habari njema, wazee Wakristo huhakikisha kwamba anaelewa mafundisho ya msingi ya Biblia, anaishi kupatana nayo, naye hujibu ndiyo kwa swali kama vile, “Je, kwa kweli unataka kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova?”

      18 Mara nyingi, watu ambao wameshiriki vya kutosha kuhubiri kuhusu Ufalme wanaposema kwamba wanataka kubatizwa, wazee Wakristo huwa na mazungumzo pamoja nao ili kuhakikisha kwamba wao ni waamini ambao wamejiweka wakfu kwa Yehova na wanatimiza matakwa yake kuhusu ubatizo. (Matendo 4:4; 18:8) Majibu wanayotoa kwa maswali 100 kuhusu mafundisho ya Biblia husaidia wazee kujua iwapo wale wanaojibu wanatimiza matakwa ya Kimaandiko kuhusu ubatizo. Wengine hukosa kustahili na hivyo hawakubaliwi kubatizwa wawe Wakristo.

      Je, Kuna Jambo Linalokuzuia?

      19. Kwa kuzingatia andiko la Yohana 6:44, ni nani watakaotawala pamoja na Yesu?

      19 Watu wengi waliolazimishwa kubatizwa huenda waliambiwa kwamba wakifa wataenda mbinguni. Lakini akirejezea wafuasi wake, Yesu alisema: “Hakuna mtu awezaye kuja kwangu isipokuwa Baba, aliyenituma, amvute yeye.” (Yohana 6:44) Yehova amevuta kwa Kristo watu 144,000 watakaotawala pamoja na Yesu katika Ufalme wa mbinguni. Ubatizo wa kulazimishwa haujawahi kumtakasa mtu yeyote kuwa mshiriki wa mpango huo mtukufu wa Mungu.—Waroma 8:14-17; 2 Wathesalonike 2:13; Ufunuo 14:1.

      20. Ni nini kinachoweza kuwasaidia watu fulani ambao bado hawajabatizwa?

      20 Tangu katikati ya miaka ya 1930 hasa, umati wa watu wanaotumaini kuokoka “dhiki kubwa” na kuishi duniani milele wamejiunga na “kondoo wengine” wa Yesu. (Ufunuo 7:9, 14; Yohana 10:16) Wanastahili kubatizwa kwa sababu wanaishi kupatana na Neno la Mungu na wanampenda kwa ‘moyo wao wote, nafsi, nguvu, na akili.’ (Luka 10:25-28) Ingawa watu fulani wanatambua kwamba Mashahidi wa Yehova ‘huabudu Mungu katika roho na kweli,’ bado hawafuati kielelezo cha Yesu kwa kuonyesha hadharani upendo wao wa kweli na kumpa Yehova ujitoaji usiohusisha wengine kwa kubatizwa. (Yohana 4:23, 24; Kumbukumbu la Torati 4:24; Marko 1:9-11) Kusali kwa bidii na kutaja mambo waziwazi kuhusu hatua hii muhimu kwaweza kuwapa kichocheo na ujasiri wa kujipatanisha kabisa na Neno la Mungu, na kujiweka wakfu kwa Yehova Mungu kwa hiari na kubatizwa.

      21, 22. Kwa nini wengine husitasita kujiweka wakfu na kubatizwa?

      21 Watu fulani husitasita kujiweka wakfu na kubatizwa kwa sababu wanajihusisha sana na mambo ya ulimwengu au kufuatia mali hivi kwamba hawana wakati wa kutosha kwa ajili ya mambo ya kiroho. (Mathayo 13:22; 1 Yohana 2:15-17) Wangepata furaha iliyoje iwapo wangebadili maoni na miradi yao! Kumkaribia Yehova kutawatajirisha kiroho, kutawasaidia wasiwe na mahangaiko mengi sana, na kuwapa amani na uradhi unaotokana na kufanya mapenzi ya Mungu.—Zaburi 16:11; 40:8; Mithali 10:22; Wafilipi 4:6, 7.

      22 Wengine husema kwamba wanampenda Yehova lakini hawataki kujiweka wakfu na kubatizwa kwa sababu wanafikiri kwamba kwa kutobatizwa hawatatoa hesabu kwa Mungu. Lakini kila mmoja wetu lazima atoe hesabu kwa Mungu. Tunawajibika tunapolisikia neno la Yehova. (Ezekieli 33:7-9; Waroma 14:12) Wakiwa ‘watu waliochaguliwa,’ Waisraeli wa kale walizaliwa katika taifa lililokuwa wakfu kwa Yehova, na kwa hiyo walikuwa na daraka la kumtumikia kwa uaminifu kulingana na maagizo yake. (Kumbukumbu la Torati 7:6, 11) Hakuna mtu anayezaliwa katika taifa kama hilo leo, lakini ikiwa tumepokea mafundisho sahihi ya Kimaandiko, twapaswa kutenda kwa imani.

      23, 24. Ni hofu gani isiyopaswa kuzuia watu wasibatizwe?

      23 Huenda wengine wakasita kubatizwa kwa sababu ya kuhofu kwamba hawana ujuzi wa kutosha. Hata hivyo, sote tuna mambo mengi ya kujifunza kwa sababu ‘mwanadamu hawezi kuvumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.’ (Mhubiri 3:11) Fikiria towashi Mwethiopia. Akiwa mgeuzwa-imani, alifahamu Maandiko kwa kadiri fulani, lakini hakufahamu mambo yote kuhusu kusudi la Mungu. Hata hivyo, baada ya kujifunza mpango wa Yehova wa wokovu kupitia dhabihu ya ukombozi ya Yesu, towashi huyo alibatizwa katika maji.—Matendo 8:26-38.

      24 Wengine husitasita kujiweka wakfu kwa Mungu kwa sababu wanahofu kwamba hawataweza kuishi kupatana na wakfu wao. Monique, mwenye umri wa miaka 17 asema: “Nimekuwa nikisitasita kubatizwa kwa sababu ya kuhofu kwamba sitaweza kuishi kupatana na wakfu wangu.” Hata hivyo, tukimtumaini Yehova kwa moyo wetu wote, ‘atanyosha mapito yetu.’ Atatusaidia ‘tuendelee kutembea katika kweli’ tukiwa watumishi wake waaminifu waliojiweka wakfu.—Mithali 3:5, 6; 3 Yohana 4.

      25. Inafaa tuchunguze swali gani?

      25 Kwa sababu ya kumtumaini Yehova kabisa na kumpenda kwa moyo wote, kila mwaka maelfu huchochewa kujiweka wakfu na kubatizwa. Kwa kweli watumishi wote wa Mungu waliojiweka wakfu wanataka kuwa waaminifu kwake. Hata hivyo, tunaishi katika nyakati za hatari, na tunakabili majaribu mbalimbali ya imani. (2 Timotheo 3:1-5) Tunaweza kufanya nini ili kuishi kupatana na wakfu wetu kwa Yehova? Tutachunguza swali hilo katika makala ifuatayo.

  • Endelea Kumtumikia Yehova kwa Moyo Thabiti
    Mnara wa Mlinzi—2002 | Aprili 1
    • Endelea Kumtumikia Yehova kwa Moyo Thabiti

      “Ee Mungu, moyo wangu u thabiti, moyo wangu u thabiti.”—ZABURI 57:7.

      1. Kwa nini tunaweza kuwa na usadikisho kama wa Daudi?

      YEHOVA anaweza kutufanya tuwe na imani thabiti ya Kikristo ili tushikamane na Ukristo wa kweli tukiwa watumishi wake waliojiweka wakfu. (Waroma 14:4) Kwa hiyo, tunaweza kuwa na usadikisho kama wa mtunga-zaburi Daudi aliyechochewa kuimba: “Ee Mungu, moyo wangu u thabiti.” (Zaburi 108:1) Ikiwa moyo wetu ni thabiti, tutachochewa kuishi kupatana na wakfu wetu kwa Mungu. Na kwa kumtegemea ili kupata mwongozo na nguvu, tunaweza kuwa imara, wenye usadikisho thabiti tukiwa washika uaminifu-maadili, ‘sikuzote tukiwa na mengi ya kufanya katika kazi ya Bwana.’—1 Wakorintho 15:58.

      2, 3. Himizo la Paulo katika 1 Wakorintho 16:13 linamaanisha nini?

      2 Mtume Paulo alisema hivi kuwahimiza wafuasi wa Yesu huko Korintho la kale na pia Wakristo wa sasa: “Kaeni macho, simameni imara katika imani, endeleeni kama wanaume, kueni mwe wenye uweza.” (1 Wakorintho 16:13) Katika Kigiriki maagizo hayo yote yako katika hali ya wakati uliopo, kwa hiyo yatuhimiza tuendelee kutenda. Himizo hilo linamaanisha nini?

      3 Tunaweza ‘kukaa macho’ kiroho kwa kumpinga Ibilisi na kumkaribia Mungu. (Yakobo 4:7, 8) Kumtegemea Yehova hutuwezesha kudumisha muungano na ‘kusimama imara katika imani ya Kikristo.’ Sisi—kutia ndani wanawake wengi walio miongoni mwetu—‘tunaendelea kama wanaume’ kumtumikia Mungu kwa ujasiri tukiwa watangazaji wa Ufalme. (Zaburi 68:11) ‘Tunakua wenye uweza’ kwa kuendelea kumtegemea Baba yetu wa kimbingu atupatie nguvu za kufanya mapenzi yake.—Wafilipi 4:13.

      4. Ni matayarisho gani tuliyofanya ili kubatizwa na kuwa Wakristo?

      4 Tulionyesha kwamba tumekubali kweli

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki