Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Fidia Hutukuza Uadilifu wa Mungu
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • kufufuliwa na kuishi katika ulimwengu mpya wa Mungu. Hiyo itatia ndani watumishi waaminifu wa Mungu waliokufa kabla ya Yesu kulipa fidia, na hata wengi waliokufa bila kumjua Mungu na kumwabudu. Biblia inasema hivi: “Kutakuwa na ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu pia.” (Matendo 24:15) Wakati huo, kwa msingi wa fidia, Yehova atawapa wanadamu wote watiifu uzima wa milele. (Yohana 3:36) Yesu mwenyewe alisema: “Mungu aliupenda ulimwengu sana hivi kwamba akamtoa Mwana wake mzaliwa-pekee, ili kila mtu anayemwamini asiangamizwe bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16) Wanadamu watapata faida hizo zote kwa sababu ya maandalizi ya Mungu ya dhabihu ya fidia.

      Hata hivyo, jambo kuu zaidi kuhusu fidia, si faida zinazotokana nayo. Jambo muhimu zaidi ni kile ambacho fidia ya Kristo inatimiza kuhusiana na jina la Yehova. Fidia inathibitisha kwamba Yehova ni Mungu mwenye haki kamilifu ambaye anaweza kushughulika na wanadamu wenye dhambi huku akiendelea kuwa safi na mtakatifu. Ikiwa Mungu hangekusudia kuandaa fidia, hakuna mzao wa Adamu, kutia ndani Enoko, Noa, na Abrahamu, ambaye angeweza kutembea pamoja na Yehova au kuwa rafiki yake. Mtunga-zaburi alitambua jambo hilo, naye akaandika: “Kama ungekuwa unaangalia makosa, Ee Yah, Ee Yehova, ni nani angesimama?” (Zaburi 130:3) Tunapaswa kumshukuru sana Yehova kwa kumtuma Mwana wake mpendwa duniani na vilevile kumshukuru Yesu kwa kukubali kwa hiari kutoa uhai wake kuwa fidia kwa ajili yetu!—Marko 10:45.

  • Mwenendo Mwema Huleta Matokeo Mazuri
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Novemba 1
    • Mwenendo Mwema Huleta Matokeo Mazuri

      KATIKA kisiwa kidogo kwenye pwani ya kusini ya Japani, mama mmoja na watoto wake watatu walianza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova. Majirani katika kisiwa hicho chenye kufuatia utamaduni sana, walipojua hivyo, walianza kumpuuza mama huyo walipokutana naye. Anaeleza hivi: “Kilichoniudhi hata zaidi ni kwamba walimdharau mume wangu na watoto wangu.” Hata hivyo, aliwaambia watoto wake: “Tutaendelea kuwasalimu majirani wetu,  kwa ajili ya jina la Yehova.”—Mathayo 5:47, 48.

      Akiwa nyumbani, aliwafundisha watoto wake kuwa wenye adabu licha ya kukataliwa na watu. Wakiwa njiani kutembelea chemchemi za maji ya moto, watoto hao walifanya mazoezi ya kusalimiana ndani ya gari. Walipoingia kwenye jengo hilo, sikuzote watoto hao walisema hivi kwa shauku “Konnichiwa!” yaani, “Siku njema!” Kwa subira, familia hiyo iliendelea kuwasalimu watu wote waliokutana nao hata ingawa majirani hawakuwachangamkia. Lakini watu hawakukosa kutambua adabu nzuri ya watoto hao.

      Hatimaye, majirani mbalimbali walijibu kwa kusema “Konnichiwa.” Baada ya miaka miwili, karibu kila mtu mjini alikuwa akijibu aliposalimiwa na familia hiyo. Pia, majirani walianza kusalimiana na kuonyeshana shauku. Msaidizi wa meya alitaka kuwapa tuzo watoto hao kwa sababu ya kuchangia badiliko hilo. Lakini mama yao alimweleza kwamba walifanya tu kile ambacho Wakristo wanapaswa kufanya. Baadaye, katika mashindano ya kuzungumza mbele ya watu yaliyofanywa katika kisiwa hicho, mwana mmoja wa mama huyo alieleza jinsi mama yao alivyokuwa amewazoeza kuwasalimu wengine kwa heshima bila kujali itikio lao. Alipata tuzo la kwanza na hotuba yake ikachapishwa katika gazeti la mji. Leo, familia hiyo inafurahi sana kwa sababu walipata matokeo mazuri kwa kufuata kanuni za Kikristo. Ni rahisi kuwahubiria wengine habari njema ikiwa wana urafiki.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki