-
Mashahidi wa YehovaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Unaweza kujibu hivi: ‘Hilo ni jambo lenye kupendeza. Na ni kweli kwamba tunapaswa kuwa mashahidi wa Yesu. Ndiyo sababu cheo cha Yesu katika kusudi la Mungu kinakaziwa katika vichapo vyetu. (Unaweza kutumia kitabu cha sasa au gazeti ili kuonyesha jambo hilo.) Lakini hapa pana jambo fulani ambalo huenda likawa jipya kwako. (Ufu. 1:5) . . . Yesu alikuwa “Shahidi Mwaminifu” wa nani? (Yoh. 5:43; 17:6) . . . Yesu alituwekea mfano tunaopaswa kufuata, sivyo? . . . Kwa nini ni muhimu sana kumjua Yesu na Baba yake pia? (Yoh. 17:3)’
-
-
MbinguKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Mbingu
Maana: Makao ya Yehova Mungu na viumbe roho waaminifu; makao yasiyoonekana kwa macho ya kibinadamu. Biblia pia inatumia neno “mbingu” katika maana nyingine mbalimbali; kwa mfano: kuwakilisha Mungu mwenyewe, tengenezo lake la viumbe roho waaminifu, hali ya kuwa na kibali cha Mungu, ulimwengu unaoonekana mbali na dunia, anga inayozunguka Dunia, serikali za kibinadamu chini ya utawala wa Shetani, na serikali mpya ya mbinguni yenye uadilifu ambayo Yesu Kristo pamoja na warithi-washirika wake wamepewa mamlaka na Yehova watawale ndani yake.
Je, sisi sote tulikuwa katika makao ya kiroho kabla hatujazaliwa tukiwa wanadamu?
Yoh. 8:23: “[Yesu Kristo alisema:] ‘Ninyi mnatoka kwenye makao ya chini; mimi ninatoka kwenye makao ya juu. Ninyi mnatoka katika ulimwengu huu; mimi sitoki katika ulimwengu huu.’” (Yesu alitoka katika makao ya kiroho. Lakini, kama Yesu alivyosema, wanadamu wengine hawakutoka huko.)
Rom. 9:10-12: “Rebeka alipochukua mimba ya mapacha . . . Walipokuwa bado hawajazaliwa wala kufanya jambo lolote jema au baya, ili kusudi la Mungu kuhusu kuchagua liendelee kutegemea, si matendo, bali Yeye ambaye huita, Rebeka aliambiwa: ‘Mkubwa atakuwa mtumwa wa mdogo.’” (Bila shaka, ikiwa mapacha hao, Yakobo na Esau, walikuwa wameishi katika makao ya kiroho kwa hakika wangekuwa na sifa ya kuwa wema au wabaya ikitegemea mwenendo wao huko, sivyo? Lakini hawakuwa na sifa zozote za aina hiyo mpaka baada ya kuzaliwa kwao wakiwa wanadamu.)
Je, watu wote wema huenda mbinguni?
Mdo. 2:34: “Daudi [ambaye Biblia inasema kwamba ni ‘mtu aliyekubalika kwa moyo wa Yehova’] hakupanda mbinguni.”
Mt. 11:11: “Kwa kweli nawaambia ninyi, Kati ya wale waliozaliwa na wanawake hajatokea mkuu kuliko Yohana Mbatizaji; lakini mtu aliye mdogo zaidi katika ufalme wa mbinguni ni mkuu kuliko yeye.” (Kwa hiyo Yohana hakuenda mbinguni alipokufa.)
Zab. 37:9, 11, 29: “Watenda-maovu watakatiliwa mbali, bali wale wanaomtumaini Yehova ndio watakaoimiliki dunia . . . Wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani. Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake.”
-