Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Tunaweza Kuwasaidiaje Watakaohudhuria Ukumbusho?
    Huduma ya Ufalme—2008 | Machi
    • Tunaweza Kuwasaidiaje Watakaohudhuria Ukumbusho?

      1. Ni ushahidi gani wenye nguvu utakaotolewa Machi 22, 2008?

      1 Machi 22, 2008, mamilioni ya watu ulimwenguni pote watapata ushahidi wenye nguvu. Wale watakaohudhuria Ukumbusho watasikia kuhusu upendo mkubwa wa Yehova katika kuandaa fidia kwa ajili ya wanadamu. (Yoh. 3:16) Watajifunza kuhusu Ufalme na jinsi ambavyo Yehova atautumia kutimiza mapenzi yake kwa ajili ya dunia yote. (Mt. 6:9, 10) Wataona upendo na umoja wa watu wa Mungu na kuhisi ukarimu wetu. —Zab. 133:1.

      2. Tunaweza kuwasaidiaje wanafunzi wa Biblia ambao watahudhuria?

      2 Wanafunzi wa Biblia: Baadhi ya wale watakaohudhuria ni watu ambao wameanza tu kujifunza Biblia pamoja nasi. Wajulishe kwa akina ndugu na dada. Waeleze kuhusu mikutano ya kila juma, na uwaonyeshe sehemu mbalimbali za Jumba la Ufalme. Wakati wa hotuba, msemaji atawatia moyo watu kama hao wazidi kufanya maendeleo ya kiroho. Unaweza kutumia maelezo yake kuwatia moyo wanafunzi wako.

      3. Ni nini kinachoweza kufanywa ili kuwatia moyo wahubiri wasiotenda ambao watahudhuria Ukumbusho?

      3 Wasiotenda: Pia kutakuwa na wahubiri wasiotenda kati ya wahudhuriaji. Wasalimu kwa uchangamfu. Epuka kuwauliza maswali ya kibinafsi au kusema mambo yatakayowaaibisha. Muda mfupi baada ya Ukumbusho, wazee wanapaswa kuwatembelea wahubiri wowote wasiotenda ambao walihudhuria, kuwapongeza kwa kujitahidi kuhudhuria, na kuwakaribisha kwa uchangamfu kwa mkutano wa kutaniko utakaofuata.

      4. Kila mmoja wetu anaweza kuwasaidiaje wageni?

      4 Wageni: Baadhi ya wahudhuriaji watakuwa marafiki au watu wa familia ambao tumewakaribisha. Wengine labda walipata mwaliko wakati wa kampeni ya pekee. Ukiona watu usiowafahamu, jitambulishe na uwakaribishe. Huenda hawajawahi kuhudhuria mkutano wetu wowote kabla ya hapo. Mnapozungumza, unaweza kujua jinsi ya kuwasiliana nao. Ukiwatembelea au kuwapigia simu siku chache baada ya Ukumbusho, unaweza kujaribu kuwachochea wapendezwe zaidi na kuwapendekezea wajifunze Biblia.

      5. Tunaweza kuanzishaje funzo la Biblia?

      5 Habari iliyozungumziwa katika hotuba ya Ukumbusho inaweza kutumiwa kama msingi wa kutoa kitabu Biblia Inafundisha unapofanya ziara ya kurudia. Kwa mfano, msemaji katika Ukumbusho atasoma Isaya 65:21-23. Unapofanya ziara ya kurudia, unaweza kutaja hotuba hiyo kisha umwambie, “Acha nikuonyeshe baraka nyingine zinazotegemea fidia.” Kisha pitia ukurasa wa 4-5 wa kitabu Biblia Inafundisha. Au unaweza kusema, “Watu wengi wanajiuliza ikiwa tutaona utimizo wa unabii wa Isaya.” Baada ya hapo zungumzia mafungu ya 1-3 katika sura ya 9. Pendekezo lingine ni kutaja maelezo ya msemaji kuhusu Ukumbusho, kutoa kitabu Biblia Inafundisha, na kuonyesha jinsi ambavyo tunajifunza Biblia.

      6. Tutapata fursa gani tutakapokuwa tukitii amri ya Yesu ya kuadhimisha kifo chake?

      6 Acheni sote tuwe macho kutumia kila fursa za kuwasaidia wanafunzi wa Biblia, wasiotenda, na wageni ambao watahudhuria. (Luka 22:19) Bila shaka, Yehova atabariki jitihada zozote za ziada katika utumishi wetu wa Ufalme.

  • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti
    Huduma ya Ufalme—2008 | Machi
    • Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti

      Mnara wa Mlinzi Feb. 1

      “Unafikiri familia zingekuwaje ikiwa zingefuata shauri hili? [Soma Waefeso 4:31. Kisha mruhusu ajibu.] Makala hii inatoa mapendekezo yanayofaa kutoka katika Biblia kuhusu kutatua matatizo na kudumisha furaha katika ndoa.” Zungumzia makala iliyo kwenye ukurasa wa 18.

      Amkeni! Feb.

      “Watu fulani wanaamini kwamba Mungu anarekodi kila kosa tunalofanya. Wengine wanafikiri kwamba anasamehe dhambi zote, hata ziwe nzito kadiri gani. Una maoni gani? [Mruhusu ajibu. Kisha usome Matendo 3:19.] Makala hii inazungumzia hatua tatu zinazotajwa katika Biblia ambazo mtu anahitaji kuchukua ili aonyeshwe rehema na Mungu.” Zungumzia makala iliyo kwenye ukurasa wa 10.

      Mnara wa Mlinzi Mac. 1

      “Ningependa kupata maoni yako kuhusu andiko hili linalojulikana sana. [Soma Yohana 3:16.] Je, umewahi kujiuliza kifo cha mtu mmoja kingewezaje kuwaletea wengine uzima wa milele? [Mruhusu ajibu.] Gazeti hili linatoa maelezo yaliyo wazi na yenye kuridhisha kuhusu jinsi tunavyoweza kunufaika kutokana na kifo cha Yesu.”

      Amkeni! Mac.

      “Je, unafikiri dini zote ni nzuri? [Mruhusu ajibu.] Ona yale ambayo Biblia inasema kuhusu ibada ya watu fulani. [Soma Marko 7:7.] Mtu anaweza kujuaje ikiwa dini inafundisha kweli wala si ‘amri za wanadamu’? Je, kweli ya kidini inaweza kupatikana? Gazeti hili linajibu maswali hayo.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki