Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Iga Ushikamanifu wa Ittai
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 15
    • Kwa mfano, kuna simulizi la yule Mgathi aliyeitwa Itai.

      ‘Mgeni na Mhamishwa’

      Inadhaniwa kwamba Itai alikuwa mwenyeji wa jiji maarufu la Ufilisti lililoitwa Gathi, nyumbani kwa lile jitu Goliathi na maadui wengine wenye kuogopesha wa Israeli. Katika Biblia, shujaa huyu wa vita, Itai, anatajwa kwa mara ya kwanza wakati Absalomu anapomwasi Mfalme Daudi. Wakati huo, Itai na wanaume 600 Wafilisti waliokuwa wamemfuata waliishi uhamishoni karibu na Yerusalemu.

      Huenda hali ya Itai na wafuasi wake ilimkumbusha Daudi wakati alipokuwa mkimbizi, wakati yeye na mashujaa 600 Waisraeli walipohamia eneo la Ufilisti na kuingia katika milki ya Akishi, mfalme wa Gathi. (1 Sam. 27:2, 3) Itai na wanaume wake wangefanya nini wakati ambapo Daudi angekabiliana na uasi wa mwana wake Absalomu? Je, wangemuunga mkono Absalomu, wangeamua kutounga mkono upande wowote, au wangejiunga na Daudi na wanaume wake?

      Wazia hali ilivyokuwa wakati Daudi alipokuwa akikimbia kutoka Yerusalemu na kusimama mahali panapoitwa Beth-merhaki, jina linalomaanisha “Nyumba ya Mbali.” Huenda ndiyo nyumba ya mwisho katika eneo la Mlima wa Mizeituni huko Yerusalemu kabla tu ya kuvuka Bonde la Kidroni. (2 Sam. 15:17) Akiwa hapo, Daudi anakagua tena majeshi yake yanapopita. Tazama! Daudi haandamani tu na Waisraeli washikamanifu bali pia na Wakerethi wote na Wapelethi wote. Zaidi ya hilo, Wagathi wote, yaani, Itai na mashujaa wake wa vita 600 wamefuatana naye.—2 Sam. 15:18.

      Daudi anamwambia hivi Itai kwa huruma nyingi: “Kwa nini wewe pia uende pamoja nasi? Rudi, ukae na mfalme [huenda alimaanisha Absalomu]; kwa maana wewe ni mgeni, na tena, wewe ni mhamishwa kutoka mahali pako. Ulikuja jana tu na je, leo nikufanye utange-tange pamoja nasi, uende wakati ninapoenda na popote ninapoenda? Rudi, na uwachukue ndugu zako urudi pamoja nao, na Yehova akuonyeshe fadhili zenye upendo na uaminifu!”—2 Sam. 15:19, 20.

      Itai anatangaza ushikamanifu wake usioyumbayumba. Anajibu hivi: “Kama Yehova anavyoishi na kama anavyoishi bwana wangu mfalme, mahali atakapokuwa bwana wangu mfalme, iwe ni kifo ama ni uzima, hapo ndipo mtumishi wako atakapokuwa!” (2 Sam. 15:21) Huenda hilo lilimkumbusha Daudi maneno yaliyosemwa na Ruthu, nyanya ya baba yake. (Rut. 1:16, 17) Daudi aliguswa moyo na maneno hayo ya Itai, hivi kwamba akamwambia hivi Itai: “Nenda uvuke” Bonde la Kidroni. Basi, “Itai Mgathi akavuka, na pia watu wake wote na watoto wadogo wote waliokuwa pamoja naye.”—2 Sam. 15:22.

      “Ili Kutufundisha Sisi”

      Andiko la Waroma 15:4 linasema hivi: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi.” Hivyo, tunapaswa kujiuliza hivi: Tunajifunza nini kutokana na mfano wa Itai? Fikiria mambo ambayo huenda yalimchochea awe mshikamanifu kwa Daudi. Hata ingawa alikuwa mgeni na mhamishwa kutoka Ufilisti, Itai alitambua kwamba Yehova ni Mungu aliye hai na Daudi ni mtiwa-mafuta wa Yehova. Itai hakuchochewa na chuki iliyokuwapo kati ya Waisraeli na Wafilisti. Hakuona tu kwamba Daudi ndiye aliyemuua yule shujaa Mfilisti Goliathi na Wafilisti wengine wengi. (1 Sam. 18:6, 7) Itai alimwona Daudi kuwa mtu aliyempenda Yehova na bila shaka aliona sifa nzuri za Daudi. Hivyo, Daudi akamheshimu sana Itai. Zaidi ya hayo, Daudi aliweka sehemu ya tatu ya majeshi yake “chini ya mkono wa Itai” katika vita vya mwisho juu ya majeshi ya Absalomu!—2 Sam. 18:2.

      Sisi pia tunapaswa kujitahidi kuona sifa nzuri za wengine badala ya kukazia fikira tofauti za kitamaduni, kijamii, au kikabila—ubaguzi au chuki yoyote ambayo huenda bado tunayo. Uhusiano mzuri uliositawi kati ya Daudi na Itai unaonyesha kwamba kumjua na kumpenda Yehova kunaweza kutusaidia kushinda vizuizi hivyo.

      Tunapotafakari kuhusu mfano wa Itai, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Je, ninaonyesha ushikamanifu kama huo kwa Daudi Mkuu Zaidi, Kristo Yesu? Je, ninaonyesha kwamba mimi ni mshikamanifu kwa kushiriki kwa bidii katika kazi ya kuhubiri kuhusu Ufalme na kufanya wanafunzi?’ (Mt. 24:14; 28:19, 20) ‘Niko tayari kuvumilia mambo mengi kadiri gani ili nionyeshe kwamba mimi ni mshikamanifu?’

      Vichwa vya familia pia wanafaidika kwa kutafakari kuhusu ushikamanifu wa Itai. Uaminifu wa Itai kwa Daudi na uamuzi wake wa kwenda pamoja na mfalme aliyetiwa mafuta na Mungu uliwachochea wanaume wa Itai. Vivyo hivyo, maamuzi ambayo vichwa vya familia wanafanya ili kutegemeza ibada ya kweli yanaweza kuwa na uvutano kwa familia zao na yanaweza hata kusababisha matatizo ya muda. Hata hivyo, tunahakikishiwa hivi: ‘Kwa mtu mshikamanifu Yehova atatenda kwa ushikamanifu.’—Zab. 18:25.

      Baada ya vita kati ya Daudi na Absalomu, Maandiko hayasemi zaidi kuhusu Itai. Hata hivyo, masimulizi hayo mafupi kumhusu katika Neno la Mungu yanatusaidia kufahamu vizuri utu wake wakati wa kipindi kigumu katika maisha ya Daudi. Kwa kuwa Itai anatajwa katika Maandiko, hilo linaonyesha kwamba Yehova anaona na kuwathawabisha watu washikamanifu.—Ebr. 6:10.

  • Kwa Nini Tumfuate “Kristo”?
    Mnara wa Mlinzi—2009 | Mei 15
    • Kwa Nini Tumfuate “Kristo”?

      “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe . . . na kunifuata sikuzote.”—LUKA 9:23.

      1, 2. Kwa nini ni jambo la maana kwetu kufikiria kwa nini tunapaswa kumfuata “Kristo”?

      YEHOVA anafurahi kama nini kuona ninyi wapya na vijana mkiwa kati ya makundi yaliyokutanika ya waabudu wake duniani! Mnapoendelea kujifunza Biblia, kuhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida, na kupata ujuzi zaidi wa kweli yenye kuokoa uhai iliyo katika Neno la Mungu, mnahitaji kuchukua kwa uzito mwaliko huu wa Yesu: “Mtu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuuchukua mti wake wa mateso siku baada ya siku na kunifuata sikuzote.” (Luka 9:23) Yesu anasema kwamba unapaswa kujikana mwenyewe na kuwa mfuasi wake. Basi, ni jambo la maana kwetu kufikiria kwa nini tunapaswa kumfuata “Kristo.”—Mt. 16:13-16.

      2 Namna gani sisi ambao tayari tunafuata hatua za Yesu Kristo? Tunahimizwa ‘tuendelee kufanya hivyo kwa ukamili zaidi.’ (1 The. 4:1, 2) Iwe tulikubali ibada ya kweli hivi karibuni au miaka mingi iliyopita, kutafakari kwa nini tunapaswa kumfuata Kristo kutatusaidia kutumia himizo la Paulo na kumfuata Kristo kwa ukamili zaidi kila siku. Acheni tufikirie sababu tano zinazoonyesha kwa nini tunapaswa kumfuata Kristo.

      Ili Tuwe na Uhusiano wa Karibu Zaidi na Yehova

      3. Tunaweza kumjua Yehova kupitia njia gani mbili?

      3 Alipokuwa akizungumza na Waathene akiwa ‘amesimama katikati ya Areopago,’ mtume Paulo alisema hivi: “[Mungu] aliamuru nyakati na mipaka ya makao ya watu, ili wao wamtafute Mungu, ikiwa wangeweza

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki