Wimbo Na. 47
Tangaza Habari Njema
Makala Iliyochapishwa
1. Kweli ya Ufalme ilikuwa siri.
Kale Yehova Uzao katabiri.
Kwa kuwa Yehova anapenda haki.
Kuangamiza wanadamu hataki.
Kristo taji Yehova amemuvika.
Na wakati wa utawala umefika.
Bibi-arusi wa Kristo yu tayari,
Kundi dogo la wasio na dosari.
2. Habari njema leo tunatangaza.
Twataka wote wazisikie sasa.
Na malaika wanatutegemeza,
Kazi ya Ufalme kuitekeleza.
Tuna pendeleo kubwa leo hasa,
Jina la Yehova Mungu kulitakasa.
Tumependelewa kuwa Mashahidi.
Kutangaza habari njema tuzidi.
(Ona pia Marko 4:11; Mdo. 5:31; 1 Kor. 2:1, 7.)