Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Uwezo wa Neno Lenye Fadhili
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Oktoba 1
    • Uwezo wa Neno Lenye Fadhili

      “Moyo uliolemewa na hangaiko, jinsi unavyoweza kufarijiwa na neno lenye fadhili!”—Mithali 12:25, Knox.

      WAKRISTO hawalindwi kabisa kutokana na taabu. Nyakati nyingine wao hupatwa na hangaiko kwa sababu ya kuishi katika hizi “nyakati za hatari.”—2 Timotheo 3:1.

      Tunapopatwa na msiba kama huo, ni baraka kama nini kusikia maneno yenye fadhili kutoka kwa rafiki mwaminifu-mshikamanifu! “Rafiki hupenda sikuzote; na ndugu amezaliwa kwa siku ya taabu,” yasema Biblia. (Mithali 17:17) Mtu mwaminifu Ayubu alijulikana kuwa rafiki wa aina hiyo. Hata Elifazi alisema hivi kumhusu: “Mtu alipojikwaa, akawa dhaifu na kuchoka, maneno yako yalimtia moyo akasimame.”—Ayubu 4:4, Today’s English Version.

      Hata hivyo, Ayubu mwenyewe alipohitaji kitia-moyo, Elifazi na waandamani wake hawakutamka maneno yenye fadhili. Wao walimlaumu Ayubu kwa ajili ya taabu yake, wakidokeza kwamba ni lazima alikuwa na kosa fulani la siri. (Ayubu 4:8) The Interpreter’s Bible chaeleza hivi: “Kile Ayubu ahitajicho ni huruma ya moyo wa kibinadamu. Yeye apokea tu mfululizo wa misemo ya kidini ya kurudiwa-rudiwa yaliyo ‘kweli’ kabisa na yanayovutia kabisa na maadili yaleyale.” Ayubu alivunjika moyo sana kwa kusikia hotuba za Elifazi na waandamani wake hivi kwamba alilazimika kupaza sauti hivi: “Je, mtanichukiza nafsi yangu hata lini, na kunivunja-vunja kwa maneno?”—Ayubu 19:2.

      Tusimfanye kamwe mtumishi mwenzetu wa Mungu alie kwa dhiki kwa sababu ya maneno yetu yasiyo na maana na yasiyo ya fadhili. (Linganisha Kumbukumbu la Torati 24:15.) Mithali moja ya Biblia yaonya hivi: “Yale uyasemayo yaweza kuokoa uhai au kuuharibu; kwa hiyo ni lazima ukubali matokeo ya maneno yako.”—Mithali 18:21, TEV.

      Kwa kutambua uwezo wa usemi, na tufuate kielelezo cha mtume Paulo. Alipokuwa Makedonia, yeye alikuwa ‘akiwafariji kwa maneno mengi.’—Matendo 20:2.

  • Je! Wewe Ungekaribisha Ziara?
    Mnara wa Mlinzi—1994 | Oktoba 1
    • Je! Wewe Ungekaribisha Ziara?

      Hata katika ulimwengu huu wenye matatizo, wewe waweza kupata furaha kutokana na ujuzi sahihi wa Biblia kuhusu Mungu, Ufalme wake, na kusudi lake zuri ajabu kwa ainabinadamu. Ikiwa ungependa habari zaidi au ungependa kutembelewa na mtu fulani ili aongoze funzo la Biblia nyumbani pamoja na wewe bila malipo, tafadhali andikia I.B.S.A., Box 47788, Nairobi, Kenya, au tumia anwani ifaayo iliyoorodheshwa kwenye ukurasa 2.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki