Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Ingawa lile Pazia la Chuma liliwazuia Waestonia wasiwasiliane na watu wa nchi nyingine, halingeweza kuzuia chakula cha kiroho kisiwafikie akina ndugu. Kwa miaka mingi akina ndugu walitumia vitabu vya miaka iliyopita. Hata hivyo, walipokuwa uhamishoni huko Siberia, Mashahidi Waestonia waliweza kukutana na ndugu kutoka maeneo mengine ya Muungano wa Sovieti. Waliporudi Estonia, waliendelea kuwasiliana kwa ujasiri na ndugu hao wa Muungano wa Sovieti na mara kwa mara, waliweza kupata chakula cha kiroho cha karibuni. Kwa mfano, kuanzia mwaka wa 1956, waliwasiliana na Ivan Dziabko na ndugu wengine kutoka Ukrainia na walipata vitabu kutoka kwao. Lakini waliwasiliana nao mara chache na walipata vitabu vichache. Mengi zaidi yalihitaji kufanywa, na muda si muda Yehova akabariki jitihada za ujasiri za ndugu zetu.

      Chini ya mwelekezo wa Baraza Linaloongoza, ofisi ya tawi ya Finland ilifanya mipango ya kuwasaidia ndugu Waestonia kwa njia yenye utaratibu zaidi. Vilho Eloranta, aliyekuwa painia nchini Estonia miaka ya 1930, alipewa mgawo wa kuwasiliana nao. Katika ziara yake ya kwanza nchini humo, mapema miaka ya 1960, alikutana na Fanny Hietala. Baada ya hapo, ndugu wengi waliojifanya watalii walizuru Finland na walitumika kama wajumbe wa kusafirisha vitabu na barua na hivyo kusaidia kuendeleza mawasiliano. Hatimaye, ndugu wa Estonia walianza kuwasiliana na “Mama,” kama akina ndugu walivyoliita tengenezo la Yehova. Waliweza kutuma barua na ripoti za huduma ya shambani na waliweza kupokea vitabu kwenye mikanda ya filamu yenye maandishi madogo. Hata hivyo, kwa kuwa mambo hayo yalihitaji kufanywa kwa siri kabisa na kwa busara sana, mawasiliano yalifanywa mara mbili au tatu kwa mwaka.

  • Estonia
    2011 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
    • Baraza Linaloongoza lilipanga mmoja wa washiriki wake, Lloyd Barry, pamoja na Viv Mouritz, kutoka ofisi ya tawi ya Finland, wakutane na Adolf Kose, aliyekuwa akisimamia kazi nchini Estonia. Walikutana katika bustani huko Leningrad (sasa ni St. Petersburg).

      Ndugu Mouritz anasema hivi kuhusu mkutano wao wa siri, “Mara ya kwanza Ndugu Kose alisita kuzungumza, na kwa tahadhari akainua gazeti lake kana kwamba analisoma. Lakini baada ya kuzungumza kwa muda, Adolf alishusha gazeti hilo, na akaanza kuongea kwa uhuru.”

      Ndugu Barry alisema hivi, “Tulipomwalika kula pamoja nasi, alikataa akisema kwamba ilikuwa ni vizuri kukazia uangalifu mambo yaliyokuwa ya maana zaidi.”

      Wakati Ndugu Kose alipoelezea wasiwasi wake kuhusu mateso na vizuizi ambavyo Mashahidi katika Muungano wa Sovieti walikuwa wanakabili, Ndugu Mouritz na Barry walimpa mapendekezo mengi yenye kutia moyo. Walimweleza hivi: “Hata katika nchi nyingine tunakabili majaribu pia. Majaribu hayo yanaonekana kuwa rahisi, lakini ni hatari zaidi! Tuna vishawishi vingi ambavyo ninyi hamvikabili, na tunapoteza watu wengi katika nchi za Magharibi kuliko hapa.”

      Hiyo ilikuwa ziara ya wakati unaofaa na yenye kuimarisha sana kwa Ndugu Kose. Alikuja kugundua baadaye kwamba alikuwa anazungumza na mshiriki wa Baraza Linaloongoza, na kwa shangwe aliwasilisha habari zenye kutia moyo kutoka katika tengenezo la Yehova kwa wote walioendelea kudumisha utimilifu wao chini ya utawala wenye kukandamiza.

      Baadaye Ndugu Barry aliandika hivi: “Tunawahurumia sana ndugu zetu katika Muungano wa Sovieti. Lilikuwa jambo zuri kukutana na Ndugu Kose na tulipokuwa tukiagana naye alitupa mkono na kutukumbatia, na hivyo tukamaliza mkutano wetu wenye kupendeza.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki