Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • bm uku. 3
  • Kwa Nini Uichunguze Biblia?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Uichunguze Biblia?
  • Biblia—Ina Ujumbe Gani?
Biblia—Ina Ujumbe Gani?
bm uku. 3
Mwanaume akitazama katika Biblia

Kwa Nini Uichunguze Biblia?

Je, wewe unaifahamu Biblia? Hakuna kitabu kingine chochote katika historia ambacho kimesambazwa sana kama Biblia. Ujumbe wake umewafariji na kuwapa tumaini watu wa tamaduni zote, nao wamefaidika na mashauri yake maishani. Hata hivyo, watu wengi leo hawaijui Biblia vizuri. Iwe wewe ni mfuasi wa dini fulani au sivyo, huenda kuna mambo fulani ambayo ungependa kujua kuhusu Biblia. Broshua hii imekusudiwa kukusaidia kupata picha ya ujumla kuhusu Biblia.

KABLA ya kuchukua Biblia na kuanza kuisoma, ingefaa kujua mpangilio wake. Biblia, ambayo pia huitwa Maandiko Matakatifu, ni mkusanyo wa vitabu au sehemu 66, kuanzia Mwanzo mpaka Ufunuo.

Biblia ilitungwa na nani? Hilo ni swali ambalo limewasumbua watu wengi. Ukweli ni kwamba Maandiko hayo yaliandikwa na wanaume wapatao 40 katika kipindi cha miaka 1,600 hivi. Hata hivyo, wanaume hao hawakudai kamwe kuwa watungaji wa Biblia. Mmoja wao aliandika: “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Mwandikaji mwingine alisema: “Roho ya Yehova ndiyo iliyosema kupitia mimi, na neno lake lilikuwa kwenye ulimi wangu.” (2 Samweli 23:2) Kulingana na waandikaji hao, Yehova Mungu ndiye Mtungaji wa Biblia naye anataka kuwa na uhusiano wa karibu na wanadamu.

Kuna jambo lingine muhimu linalohitajika ili kuielewa Biblia. Biblia ina ujumbe mmoja wa msingi: kutetewa kwa haki ya Mungu ya kuwatawala wanadamu kupitia Ufalme wa mbinguni. Katika broshua hii, utaona jinsi ujumbe huo unavyojitokeza kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka Ufunuo.

Ukiwa na hayo akilini, sasa chunguza ujumbe ulio katika kitabu maarufu zaidi ulimwenguni, Biblia.

HABARI MUHIMU KUHUSU BIBLIA

  • Ilichukua miaka 1,610 kuandikwa, tangu mwaka wa 1513 K.W.K. mpaka mwaka wa 98 W.K.a

  • Vitabu 39 vya kwanza—vilivyoandikwa hasa katika Kiebrania, na sehemu kadhaa katika Kiaramu—vinaitwa Maandiko ya Kiebrania, au “Agano la Kale.”

  • Vitabu 27 vya mwisho—vilivyoandikwa katika Kigiriki—vinaitwa Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo, au “Agano Jipya.”

  • Biblia imegawanywa katika sura na mistari. Kwa mfano, Mathayo 6:9, 10 inarejelea sura ya 6 ya kitabu cha Mathayo, mstari wa 9 na wa 10.

a Kuna njia mbalimbali za kutaja tarehe. Katika broshua hii, herufi W.K. zinamaanisha “Wakati wa Kawaida” na K.W.K. zinamaanisha “Kabla ya Wakati wa Kawaida.” Herufi hizo zinatumiwa katika chati iliyo sehemu ya chini ya kurasa.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki