Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Utatu
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • katika Biblia? . . . (Rejelea konkodansi katika Biblia yako.) Lakini je, Kristo anatajwa katika Biblia? . . . Ndiyo, nasi tunamwamini. Ona hapa katika konkodansi chini ya “Kristo” kwamba mojawapo ya marejeo ni andiko la Mathayo 16:16. (Lisome.) Hilo ndilo ninaloamini.’

      Au unaweza kujibu hivi: (ikiwa mtu anataja kihususa andiko la Yohana 1:1): ‘Naujua mstari huo. Tafsiri fulani za Biblia husema kwamba Yesu ni “Mungu,” na nyingine husema kwamba yeye ni “mungu.” Kwa nini hivyo?’ (1) ‘Je, labda ni kwa sababu mstari unaofuata unasema kwamba yeye alikuwa “pamoja na Mungu”?’ (2) ‘Je, labda pia ni kwa sababu ya yale yanayopatikana hapa katika Yohana 1:18?’ (3) ‘Je, umewahi kujiuliza ikiwa Yesu mwenyewe humwabudu mwingine akiwa Mungu? (Yoh. 20:17)’

      ‘Je, unaamini kwamba Kristo ni mungu?’

      Unaweza kujibu hivi: ‘Ndiyo, bila shaka naamini. Lakini labda maoni yangu ni tofauti na yako unaposema “Kristo ni mungu.”’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Kwa nini nasema hivyo? Katika andiko la Isaya 9:6 Yesu Kristo anaitwa “Mungu Mwenye Nguvu,” lakini Baba yake peke yake ndiye anayeitwa Mungu Mweza-Yote katika Biblia.’ (2) ‘Na ona kwamba katika Yohana 17:3 Yesu anamwita Baba yake kuwa “Mungu wa pekee wa kweli.” Kwa hiyo, Yesu ni mrudisho tu wa utukufu wa Mungu wa kweli.’ (3) ‘Tunapaswa kufanya nini ili tumpendeze Mungu? (Yoh. 4:23, 24)’

  • Uumbaji
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
    • Uumbaji

      Maana: Uumbaji, kama unavyoelezwa katika Biblia, humaanisha kwamba Mungu Mweza-Yote aliubuni na kuutokeza ulimwengu, kutia ndani watu wengine wa kiroho na aina zote za msingi za viumbe vilivyo duniani.

      Katika ulimwengu huu wa kisasa, wa kisayansi, je, ni jambo linalopatana na akili kuamini uumbaji?

      “Sheria za asili za ulimwengu ni sahihi sana hivi kwamba si vigumu kutengeneza vyombo vya angani viruke mpaka mwezini na tunaweza kupima kwa usahihi safari yake hata kwa sehemu ya sekunde. Lazima sheria hizo ziliwekwa na mtu fulani.”—Akasema Wernher von Braun, aliyehusika sana katika kuwatuma wanaanga wa Marekani mwezini.

      Ulimwengu unaoonekana: Ikiwa ungepata saa iliyo sahihi, je, ungekata shauri kwamba ilijitokeza yenyewe kutokana na mavumbi yaliyopulizwa pamoja? Kwa wazi, ilitengenezwa na mtu mwenye akili. Kuna “saa” iliyo ya ajabu hata zaidi. Sayari zilizo katika mfumo wetu wa jua, pia nyota zilizo ulimwenguni, husafiri kwa mwendo sahihi kuliko saa nyingi zilizobuniwa na kutengenezwa na mwanadamu. Galaksi iliyo na mfumo wetu wa jua ina nyota zaidi ya bilioni 100, na wataalamu wa nyota hukadiria kwamba kuna bilioni 100 za galaksi kama hizo ulimwenguni. Ikiwa saa hubuniwa na mtu mwenye akili, je, ulimwengu ulio mkubwa zaidi na mgumu kufahamika haukuhitaji kubuniwa na mtu mwenye akili hata zaidi? Biblia humtaja Mbuni wake kuwa “Mungu wa kweli, Yehova, Muumba wa mbingu na Mkuu anayezitandaza.”—Isa. 42:5; 40:26; Zab. 19:1.

      Dunia: Unapovuka jangwa lenye ukame, ikiwa ungefika mahali penye nyumba nzuri sana, iliyo na vifaa mbalimbali na chakula tele, je, ungeamini kwamba ilijitokeza yenyewe baada ya mlipuko fulani? Hapana; ungetambua kwamba mtu fulani mwenye hekima aliijenga. Wanasayansi bado hawajapata uhai katika sayari yoyote ya mfumo wetu wa jua isipokuwa katika dunia hii; uthibitisho uliopo huonyesha kwamba sayari nyingine hazina uhai. Kitabu The Earth kinasema dunia hii ni “ajabu ya ulimwengu, sayari isiyo na kifani.” (New York, 1963, Arthur Beiser, uku. 10) Iko umbali unaofaa kabisa kutoka kwenye jua kwa ajili ya uhai wa kibinadamu, na inasonga kwa mwendo unaofaa kabisa ili isitoke kwenye mzingo wake. Hali ya hewa, ya aina inayopatikana duniani tu, imefanyizwa kwa mchanganyiko unaofaa wa gesi ili kuendeleza uhai. Kwa kustaajabisha, nuru kutoka kwenye jua, kaboni-dioksidi kutoka kwenye hewa, na maji na madini kutoka kwenye udongo wenye rutuba huungana ili kuzalisha chakula kwa ajili ya wakaaji wa dunia. Je, yote hayo yalitokea kwa sababu ya mlipuko fulani angani ambao haukuongozwa na mtu? Jarida Science News hukubali hivi: “Inaonekana kwamba hali hususa na sahihi kama hizo hazingaliweza kutokea zenyewe tu.” (Agosti 24 na 31, 1974, uku. 124) Uamuzi huu wa Biblia unapatana na akili: “Bila shaka, kila nyumba hujengwa na mtu fulani, lakini yeye aliyevijenga vitu vyote ni Mungu.”—Ebr. 3:4.

      Ubongo wa binadamu: Kompyuta za kisasa zimetengenezwa baada ya uchunguzi na ufundi mkubwa. ‘Hazikutokea zenyewe tu.’ Namna gani ubongo wa binadamu? Tofauti na ubongo wa mnyama yeyote, ubongo wa mtoto mchanga wa binadamu huongezeka ukubwa mara tatu katika mwaka wake wa kwanza. Jinsi unavyotenda kazi bado ni fumbo kubwa kwa wanasayansi. Wanadamu wana uwezo wa asili wa kujifunza lugha ngumu, kufurahia uzuri, kutunga muziki, kutafakari chanzo na maana ya uhai. Robert White, daktari anayepasua ubongo, alisema: “Sina la kusema ila kukubali kwamba kuna Akili Iliyo Kubwa Zaidi, iliyobuni na kusitawisha uhusiano wa ajabu kati ya akili na ubongo—jambo ambalo mwanadamu hawezi kabisa kulielewa.” (The Reader’s Digest, Septemba 1978, uku. 99) Jambo hilo la ajabu huanza kwa chembe ndogo iliyotungwa katika tumbo la uzazi. Akiwa na ufahamu huo wa ajabu, Daudi mwandikaji wa Biblia alimwambia Yehova: “Nitakusifu kwa sababu nimeumbwa kwa njia ya ajabu yenye kuogopesha. Kazi zako ni za ajabu, kama vile nafsi yangu inavyojua vema.”—Zab. 139:14.

      Chembe hai: Chembe hai ndogo mara nyingine hutajwa kuwa namna “rahisi” ya uhai. Lakini mnyama mwenye chembe moja anaweza kukamata chakula, kukimeng’enya, kuondoa taka mwilini, kujijengea nyumba na kujamiiana. Kila chembe ya mwili wa binadamu imefananishwa na jiji lenye kuta, lenye serikali kuu ya kudumisha utaratibu, kiwanda cha kutokeza nishati, viwanda vya kutengeneza protini, mfumo tata wa usafirishaji, na walinzi wa kusimamia kinachoruhusiwa kuingia. Na mwili mmoja wa binadamu umefanyizwa kwa chembe zipatazo trilioni 100. Jinsi yanavyofaa maneno ya Zaburi 104:24: “Jinsi kazi zako zilivyo nyingi, Ee Yehova! Zote umezifanya kwa hekima”!

      Je, wazo la kwamba Mungu alitumia mageuzi ili kufanyiza aina mbalimbali za vitu vilivyo hai linapatana na Biblia?

      Mwanzo 1:11, 12 husema kwamba majani na miti vilifanywa vizae kila kimoja “kulingana na aina yake.” Mistari 21, 24, 25 huongeza kwamba Mungu aliumba viumbe vya baharini, viumbe vinavyoruka na wanyama wa nchi kavu, vyote “kulingana na aina yake.” Kwa hiyo,

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki