Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Machi uku. 7
  • Ufufuo Unawezekana kwa Msingi wa Fidia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ufufuo Unawezekana kwa Msingi wa Fidia
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
  • Habari Zinazolingana
  • Tumaini Hakika kwa Wapendwa Wako Ambao Wamekufa
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Tujapohuzunika, Hatujakosa Tumaini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1995
  • Suluhisho Pekee la Kifo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
  • Wapendwa Wako Wanaweza Kuwa Hai Tena!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo (2016)
mwb16 Machi uku. 7

MAISHA YA MKRISTO

Ufufuo Unawezekana kwa Msingi wa Fidia

Baada ya watu wa familia na marafiki kumwombolezea mwanamke kijana aliyekufa, dada yake anatafuta faraja kwa kutafakari ahadi ya ufufuo ya wakati ujao

Ukumbusho unaandaa fursa nzuri ya kutafakari baraka za wakati ujao kupitia fidia, kama vile ufufuo. Yehova hakukusudia kamwe wanadamu wafe. Hiyo ndiyo sababu sisi huhuzunika sana mpendwa wetu anapokufa. (1Ko 15:26) Yesu alihuzunika alipowaona wanafunzi wake wakiomboleza kifo cha Lazaro. (Yoh 11:33-35) Kwa sababu Yesu anamwiga Baba yake kikamili, tunaweza kuwa na uhakika kwamba Yehova pia anaumia anapotuona tukiomboleza wapendwa wetu wanapokufa. (Yoh 14:7) Yehova anatamani sana wakati ambapo atawafufua watumishi wake, sisi pia tunatamani kuwaona wapendwa wetu waliokufa.—Ayu 14:14, 15.

Kwa sababu Yehova ni Mungu wa mpango, inapatana na akili kuamini kwamba wafu watafufuliwa kwa mpangilio. (1Ko 14:33, 40) Badala ya mazishi, tutawakaribisha watakaofufuliwa. Je, wewe hutafakari kuhusu ufufuo, hasa wakati wa huzuni? (2Ko 4:17, 18) Je, unamshukuru Yehova kwa kuandaa mpango wa fidia na kufunua katika Maandiko kwamba wafu wataishi tena?—Kol 3:15.

  • Kati ya ndugu na rafiki zako ni nani hasa unayetazamia kwa hamu kumwona tena?

  • Ni nani katika Biblia ambaye ungependa sana kukutana naye na kuongea naye?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki