-
Jibu la Yehova kwa Sala ya Kutoka MoyoniMnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
-
-
17. Ni hali gani ngumu ambayo wanadamu wanakabili, na ni maneno gani ambayo tutakumbuka hivi karibuni?
17 Tunajua wazi kwamba wapinzani wataendelea kututesa. Nasi tunaendelea kuwahubiria habari njema hata wapinzani. (Mt. 24:14, 21) Hata hivyo, nafasi inayotolewa sasa kwa wapinzani hao kutubu na kupata wokovu itakwisha hivi karibuni. Kutakaswa kwa jina la Yehova ndilo jambo la maana zaidi hata kuliko wokovu wa wanadamu. (Soma Ezekieli 38:23.) Mataifa yote duniani yanapoungana duniani pote ili kujaribu kuwaangamiza watu wa Mungu kama ilivyotabiriwa, tutakumbuka maneno yafuatayo ya sala ya mtunga-zaburi: “Na waone aibu na kusumbuka nyakati zote, nao wafedheheshwe na kuangamia.”—Zab. 83:17.
18, 19. (a) Wapinzani washupavu wa enzi kuu ya Yehova watapatwa na nini hivi karibuni? (b) Kutetewa kwa mara ya mwisho kwa enzi kuu ya Yehova ambako kunakaribia kunakuchochea ufanye nini?
18 Wapinzani ambao wameazimia kuipinga enzi kuu ya Yehova watapatwa na mwisho wenye kufedhehesha. Neno la Mungu linafunua kwamba wale “wasiotii habari njema,” ambao wataangamizwa kwenye Har–Magedoni, watapata adhabu ya “uharibifu wa milele.” (2 The. 1:7-9) Kuharibiwa kwao na kuokolewa kwa wale ambao wanamwabudu Yehova katika kweli kutathibitisha kwa njia yenye kusadikisha kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli. Katika ulimwengu mpya, ushindi huo mkubwa hautasahauliwa. Wale watakaofufuliwa katika “ufufuo wa waadilifu na wasio waadilifu” watajulishwa kuhusu tendo hilo kuu la Yehova. (Mdo. 24:15) Katika ulimwengu mpya, wataona uthibitisho wenye kusadikisha kwamba kuishi chini ya enzi kuu ya Yehova ni jambo la hekima. Na wapole kati yao watasadiki haraka kwamba Yehova ndiye Mungu wa pekee wa kweli.
-
-
“Kwa Kweli Hilo Ni Jina la Mungu Ambalo Ni Takatifu na Kuu Zaidi”Mnara wa Mlinzi—2008 | Oktoba 15
-
-
“Kwa Kweli Hilo Ni Jina la Mungu Ambalo Ni Takatifu na Kuu Zaidi”
Nicholas wa Cusa alisema maneno hayo katika mahubiri yake mwaka wa 1430.a Nicholas alipendezwa na habari mbalimbali. Kwa mfano, alijifunza Kigiriki, Kiebrania, falsafa, elimu ya dini, hesabu, na elimu ya nyota. Alikuwa mtaalamu wa sheria za Kanisa Katoliki akiwa na umri wa miaka 22. Katika mwaka wa 1448 aliteuliwa kuwa kadinali.
Miaka 550 hivi iliyopita, Nicholas wa Cusa alianzisha hospitali ya kuwatunzia wazee katika mji wa Kues, ambao sasa unaitwa Bernkastel-Kues, kilomita 130 hivi kusini mwa Bonn, huko Ujerumani. Kwa sasa maktaba ya Cusa iliyo na hati zaidi ya 310 iko katika jengo hilo. Moja ya hati hizo ni Kodeksi Cusanus 220 ambayo ina hotuba ya Cusa ya mwaka wa 1430. Katika hotuba hiyo, In principio erat verbum (Hapo Mwanzo Alikuwako Neno), Nicholas wa Cusa alitumia jina Yehova kama linavyoandikwa katika Kilatini, yaani, Iehoua.b Ukurasa wa 56 una maneno yafuatayo kuhusu jina la Mungu: “Ni jina ambalo Mungu amejipa. Ni Tetragramatoni, yaani, jina ambalo linafanyizwa kwa herufi nne. . . . Kwa kweli hilo ni jina la Mungu ambalo ni takatifu na kuu zaidi.” Maneno ya Nicholas wa Cusa yanaunga mkono kupatikana kwa jina la Mungu katika maandishi ya awali ya Maandiko ya Kiebrania.—Kut. 6:3.
Kodeksi hiyo ya karne ya 15 ni moja ya hati za zamani zaidi zilizopo ambamo Tetragramatoni inatafsiriwa kuwa “Iehoua.” Maandishi hayo ni uthibitisho mwingine wa kwamba tafsiri mbalimbali za jina la Mungu zinazofanana na “Yehova” ndizo zimejulikana zaidi kwa muda wa karne nyingi.
-