Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fg somo la 8 maswali 1-5
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
  • Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Habari Zinazolingana
  • Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Majibu ya Maswali Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Kwa Nini Kuna Mateso Mengi Ulimwenguni?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kwa Nini Wanadamu Wanateseka na Kupatwa na Mambo Mabaya?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
fg somo la 8 maswali 1-5

SOMO LA 8

Kwa Nini Mungu Anaruhusu Uovu na Kuteseka?

1. Uovu ulianzaje?

1. Adamu akiliangalia tunda walilokatazwa kula; 2. Watawala mbalimbali wa kibinadamu; 3. Vita

Mungu amewaruhusu wanadamu watawale kwa kipindi kinachotosha kuthibitisha kwamba hawawezi kutatua matatizo yao

Uovu ulianza duniani wakati Shetani aliposema uwongo wa kwanza. Shetani hakuwa mwovu alipoumbwa. Alikuwa malaika mkamilifu, lakini “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alikuza tamaa ya kutaka kuabudiwa ambayo ni haki ya Mungu pekee. Shetani alimdanganya mwanamke wa kwanza, Hawa, na kumshawishi amtii yeye badala ya kumtii Mungu. Adamu alijiunga na Hawa katika kutomtii Mungu. Uamuzi huo wa Adamu ulileta mateso na kifo.​—Soma Mwanzo 3:1-6, 19.

Shetani alipomshawishi Hawa asimtii Mungu, alianzisha uasi dhidi ya enzi kuu ya Mungu, au haki ya Mungu ya kutawala. Wanadamu wengi wamejiunga na Shetani katika kumkataa Mungu kuwa Mtawala wao. Hivyo, Shetani amekuwa “mtawala wa ulimwengu.”​—Soma Yohana 14:30; 1 Yohana 5:19.

2. Je, uumbaji wa Mungu ulikuwa na kasoro?

Kazi zote za Mungu ni kamilifu. Wanadamu na malaika waliumbwa na Mungu wakiwa na uwezo kamili wa kutii matakwa yake. (Kumbukumbu la Torati 32:4, 5) Mungu alituumba tukiwa na uhuru wa kuchagua kufanya mema au mabaya. Uhuru huo unatupa nafasi ya kuonyesha upendo wetu kwa Mungu.​—Soma Yakobo 1:13-15; 1 Yohana 5:3.

3. Kwa nini Mungu ameruhusu wanadamu waendelee kuteseka?

Kwa muda fulani Yehova Mungu amevumilia uasi dhidi ya enzi yake kuu. Kwa nini? Ili kuthibitisha kwamba jitihada yoyote ya kutawala bila kumtegemea yeye haiwezi kuwanufaisha wanadamu. (Mhubiri 7:29; 8:9) Baada ya miaka 6,000 ya historia ya wanadamu, jambo hilo limethibitika kuwa kweli. Watawala wa kibinadamu wameshindwa kukomesha vita, uhalifu, ukosefu wa haki, na magonjwa.​—Soma Yeremia 10:23; Waroma 9:17.

Tofauti na utawala wa wanadamu, utawala wa Mungu unawanufaisha wale wanaoukubali. (Isaya 48:17, 18) Hivi karibuni, Mungu ataziharibu serikali zote za wanadamu. Watu pekee watakaokaa duniani ni wale tu wanaochagua kutawaliwa na Mungu.—Isaya 11:9.​—Soma Danieli 2:44.

Tazama video Kwa Nini Mungu Anaruhusu Kuteseka?

4. Subira ya Mungu inatupa nafasi ya kufanya nini?

Shetani alidai kwamba hakuna mwanadamu anayeweza kumtumikia Yehova kwa kupenda, pasipo ubinafsi. Je, ungependa kukanusha uwongo huo? Unaweza kufanya hivyo! Subira ya Mungu inatupa sisi sote nafasi ya kuonyesha ikiwa tunaunga mkono utawala wa Mungu au wa wanadamu. Tunaonyesha tunaunga mkono utawala gani kupitia jinsi tunavyoishi.​—Soma Ayubu 1:8-12; Methali 27:11.

5. Tunaweza kumchagua Mungu kuwa Mtawala wetu jinsi gani?

Watu wakijifunza Biblia

Maamuzi yetu yanaonyesha ikiwa tunataka Mungu awe Mtawala wetu

Tunaweza kumchagua Mungu kuwa Mtawala wetu kwa kujifunza na kushiriki katika ibada ya kweli inayotegemea Neno lake, Biblia. (Yohana 4:23) Tunaweza kumkataa Shetani kuwa mtawala wetu kwa kujiepusha na siasa na vita, kama Yesu alivyofanya.​—Soma Yohana 17:14.

Shetani anatumia nguvu zake kuwachochea watu waishi maisha mapotovu na kufanya mambo yanayowaumiza wengine. Tunapoyaacha mambo hayo, baadhi ya rafiki zetu na majirani wanaweza kutudhihaki au kutupinga. (1 Petro 4:3, 4) Hivyo, kuna maamuzi tunayopaswa kufanya. Je, tutashirikiana na watu wanaompenda Mungu? Je, tutatii sheria zake zenye hekima na upendo? Ikiwa tutafanya hivyo, tutathibitisha kwamba Shetani alidanganya alipodai kuwa hakuna mtu ambaye angemtii Mungu hali zikiwa ngumu.​—Soma 1 Wakorintho 6:9, 10; 15:33.

Upendo wa Mungu kuelekea wanadamu ni uthibitisho wa kwamba uovu na mateso yataisha. Wale wanaouchagua utawala wa Mungu, watafurahia uhai wa milele duniani.​—Soma Yohana 3:16.

Unaweza kupata habari zaidi katika sura ya 11 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki