-
Acha “Sheria ya Fadhili Zenye Upendo” Ilinde Ulimi WakoMnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
-
-
18, 19. Kwa nini sheria ya fadhili zenye upendo haipaswi kuondoka kwenye ulimi wetu tunaposhughulika na waabudu wenzetu?
18 Tunapaswa kuonyesha upendo mshikamanifu katika mambo yote tunaposhughulika na waabudu wenzetu wa Yehova. Hata tunapokabiliana na hali ngumu, sheria ya fadhili zenye upendo haipaswi kuondoka kwenye ulimi wetu. Yehova alikasirika wakati fadhili zenye upendo za wana wa Israeli zilipokuwa “kama umande ambao hutoweka mapema.” (Hos. 6:4, 6) Kwa upande mwingine, Yehova anafurahi wakati tunapokuwa na zoea la kuonyesha fadhili zenye upendo kwa ukawaida. Hebu ona jinsi anavyowabariki wale wanaofuatilia fadhili zenye upendo.
-
-
Kwa Nini Unapaswa Kufika kwa Wakati?Mnara wa Mlinzi—2010 | Agosti 15
-
-
Kwa Nini Unapaswa Kufika kwa Wakati?
SI RAHISI kufika kwa wakati sikuzote. Huenda tukahitaji kukabiliana na matatizo kama vile kusafiri mbali sana, msongamano mkubwa wa magari, na ratiba zenye shughuli nyingi. Hata hivyo, kufika kwa wakati ni jambo la maana. Kwa mfano, kwa ujumla mtu anayefika kazini kwa wakati anaonwa kuwa mtu mwenye kutegemeka na mwenye bidii. Kwa upande mwingine, mtu ambaye anafika akiwa amechelewa anaweza kuvuruga kazi za wengine na kupunguza ubora wa kazi au huduma. Mwanafunzi anayechelewa anaweza kukosa vipindi fulani vya masomo na hilo linaweza kumzuia kufanya vizuri shuleni. Kuchelewa kufika kumwona daktari wa kitiba au wa meno kunaweza kufanya upokee matibabu yasiyofaa.
Hata hivyo, katika sehemu fulani, watu hawaoni kufika kwa wakati kuwa jambo la maana sana. Katika mazingira hayo, ni rahisi sana kuwa na zoea la kuchelewa. Ikiwa ndivyo ilivyo, ni jambo la maana kwamba tusitawishe tamaa ya kufika kwa wakati. Tukithamini umuhimu wa kufika kwa wakati, bila shaka hilo litatusaidia kutochelewa. Tuna sababu gani za kufika kwa wakati? Tunaweza kufanya nini ili tufike kwa wakati? Na ni faida gani tunazoweza kupata tukifika kwa wakati?
Yehova Ni Mungu Anayefuata Wakati
Sababu kuu zaidi ambayo inatufanya tusiwe na zoea la kuchelewa ni kwamba tunataka kumwiga Mungu tunayemwabudu. (Efe. 5:1) Yehova anaweka mfano bora kabisa katika kufuata
-