Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Fundisha Kweli
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2016 | Agosti
    • MAISHA YA MKRISTO

      Fundisha Kweli

      Kuanzia Septemba, Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha litakuwa na pendekezo jipya kwa ajili ya utumishi lenye kichwa “Fundisha Kweli.” Lengo letu litakuwa kukazia kweli ya msingi kutoka katika Biblia, kwa kutumia swali na andiko.

      Tukitambua kwamba mtu amependezwa, tunaweza kuchochea hamu kwa ajili ya ziara inayofuata kwa kumwachia chapisho au kwa kumwonyesha video kutoka kwenye jw.org. Tunapaswa kujaribu kurudi baada ya siku chache ili kuendeleza upendezi ulioonyeshwa. Mapendekezo hayo mapya na pia migawo ya wanafunzi, itategemea muhtasari ulio mwishoni mwa sura za kitabu Biblia Inatufundisha Nini? Sehemu hiyo itakuwa na maswali ya ziada na maandiko ya kutusaidia kufanya ziara za kurudia na kuongoza funzo kwa kutumia Biblia peke yake.

      Kuna barabara moja tu inayoelekea kwenye uzima. (Mt 7:13, 14) Kwa kuwa tunazungumza na watu wa dini na malezi mbalimbali, tunapaswa kuonyesha kweli za Biblia zitakazopendeza kila mmoja wao. (1Ti 2:4) Tunapojitahidi kuelewa habari mbalimbali zilizo katika Biblia na kuboresha ustadi wetu wa ‘kulitumia sawasawa neno la kweli’ shangwe yetu itaongezeka, na tutafaulu kuwafundisha wengine kweli.​—2Ti 2:15.

  • Kampeni ya Pekee ya Kusambaza Mnara wa Mlinzi Mwezi wa Septemba
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha—2016 | Agosti
    • MAISHA YA MKRISTO

      Kampeni ya Pekee ya Kusambaza Mnara wa Mlinzi Mwezi wa Septemba

      Mnara wa Mlinzi Na. 5 2016 | Unaweza Kupata Wapi Faraja?

      Watu ulimwenguni pote wanahitaji faraja. (Mhu 4:1) Mwezi wote wa Septemba tutafanya jitihada ya pekee kutoa gazeti la Mnara wa Mlinzi. Habari kuu ya gazeti hilo itakuwa kuhusu faraja. Jitahidini kutoa gazeti hilo kadiri iwezekanavyo. Kwa sababu tungependa kuzungumza moja kwa moja na watu ili kuwafariji, hatutaacha gazeti hilo kwenye nyumba ambazo hazina watu.

      JAMBO LA KUSEMA

      “Mara kwa mara, kila mmoja wetu anahitaji faraja. Unafikiri tunaweza kuipataje? [Soma 2 Wakorintho 1:3, 4.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linaonyesha jinsi Mungu anavyotufariji.”

      Mtu akionyesha upendezi na kukubali gazeti hilo, . . .

      ONYESHA VIDEO KWA NINI UJIFUNZE BIBLIA?

      Mweleze kuhusu mpango wa kujifunza Biblia.

      WEKA MSINGI WA ZIARA YA KURUDIA

      Muulize swali ambalo utajibu utakaporudi, kama vile, “Kwa nini Mungu anawaacha watu wateseke?”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki