WIMBO NA. 78
‘Kufundisha Neno la Mungu’
Makala Iliyochapishwa
1. Tuwafundishapo watu,
Neno lake Mungu.
Baraka tunazopata,
Hazina kifani.
Tunamwiga Kristo Yesu,
Alivyofundisha.
Tungependa tufundishao
Wawe rafikize.
2. Tukiwa walimu stadi
Tuweke mfano;
Waone unyofu wetu,
Tuangaze nuru.
Tuchunguze Maandiko,
Tuyatafakari.
Tujifunze ili tufunze
Na wengine pia.
3. Yehova hutuwezesha,
Kufundisha Neno.
Tukimwomba msaada,
Atatusikia.
Twalipenda Neno Lake,
Tunalithamini.
Tuwapende tuwafunzao
Wajiunge nasi.
(Ona pia Zab. 119:97; 2 Tim. 4:2; Tito 2:7; 1 Yoh. 5:14.)