MAISHA YA MKRISTO
Kuboresha Ustadi Wetu katika Huduma—Kutumia Maswali Vizuri
KWA NINI NI MUHIMU: Ikiwa “mawazo yaliyo moyoni mwa mtu ni kama maji yenye kina,” basi maswali ni kama ndoo inayotumiwa kuyateka. (Met 20:5) Maswali yanatusaidia kuwahusisha wasikilizaji. Majibu ya maswali yaliyoteuliwa vizuri yanatusaidia kupata habari muhimu. Yesu alitumia maswali kwa njia inayofaa. Tunaweza kumwigaje?
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Uliza maswali ya maoni. Yesu aliuliza mfululizo wa maswali ili kujua maoni ya wanafunzi wake. (Mt 16:13-16; be 238 ¶3-5) Unaweza kuuliza maswali gani ya maoni?
Uliza maswali ya kumsaidia mtu kufikiri. Ili kurekebisha kufikiri kwa Petro, Yesu aliuliza maswali na kumweleza mambo kadhaa ambayo yangemsaidia Petro kufikia mkataa unaofaa. (Mt 17:24-26) Unaweza kuuliza maswali gani yatakayomsaidia mtu kufikiri na kufikia mkataa unaofaa?
Mpongeze msikilizaji wako. Baada ya mwandishi fulani “[kujibu] kwa kutumia akili,” Yesu alimpongeza. (Mk 12:34) Unaweza kumpongeza jinsi gani mtu anayejibu swali ulilouliza?
TAZAMENI SEHEMU YA KWANZA YA VIDEO FANYA KAZI AMBAYO YESU ALIFANYA—FUNDISHA, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ingawa habari zilizozungumziwa ni sahihi, kwa nini huo ni mfano mbaya wa ufundishaji?
Kwa nini hatupaswi kueleza tu habari?
TAZAMENI SEHEMU YA PILI YA VIDEO, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ndugu huyo alitumiaje maswali kwa njia yenye matokeo?
Ni mambo gani mengine tunayoweza kuiga kutokana na ufundishaji wake?
Ufundishaji wetu utawaathiri wengine jinsi gani? (Lu 24:32)