WIMBO NA. 119
Lazima Tuwe na Imani
Makala Iliyochapishwa
1. Kale Yehova Mungu kasema,
Kupitia manabii.
Leo kupitia Mwana wake,
Anasema: ‘Tubuni! ’
(KORASI)
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
2. Amri ya Yesu Kristo twatii,
Ufalme tunatangaza.
Tuutangaze ujumbe wake
Utakaotimizwa.
(KORASI)
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
3. Tuna imani nayo ni ngao;
Kamwe hatutaogopa.
Tunavumilia tukijua,
Wokovu u karibu.
(KORASI)
Je, tuna imani kweli?
Ni lazima tuijenge.
Je, ni ya matendo kweli?
Imani iokoayo nafsi.
(Ona pia Rom. 10:10; Efe. 3:12; Ebr. 11:6; 1 Yoh. 5:4.)