Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • th somo la 7 uku. 10
  • Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha
  • Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Habari Zinazolingana
  • Kusema Mambo Yaliyo Sahihi
    Faidika na Elimu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
  • Kutoa Utangulizi Mzuri wa Maandiko
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kuonyesha Wasikilizaji Manufaa ya Habari Unayozungumzia
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
  • Kutumia Maswali
    Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
Pata Habari Zaidi
Boresha Uwezo Wako wa Kusoma na Kufundisha
th somo la 7 uku. 10

SOMO LA 7

Kusema Mambo Sahihi na Yenye Kusadikisha

Andiko lililotajwa

Luka 1:3

MUHTASARI: Tumia habari zinazoaminika kuwasaidia wasikilizaji kufikia mkataa sahihi.

JINSI YA KUFANYA HIVYO:

  • Tegemea vyanzo vinavyoaminika. Tumia Neno la Mungu kutegemeza maneno yako, ukisoma moja kwa moja kutoka katika Biblia inapowezekana. Ikiwa unataja jambo la kisayansi, taarifa ya habari, jambo lililoonwa, au habari nyingine inayounga mkono jambo unalosema, chunguza mapema ikiwa chanzo hicho kinategemeka na ni cha karibuni zaidi.

  • Tumia marejeo vizuri. Eleza maandiko kupatana na muktadha wake, ujumbe mkuu wa Biblia, na machapisho ya “mtumwa mwaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Unapotumia vyanzo ambavyo si vya kimaandiko, hakikisha kwamba unafanya hivyo kwa usahihi bila kubadili maana ya awali au kusema kitu kwa njia tofauti na kile ambacho mwandishi alikusudia.

    Dokezo linalofaa

    Unapotaja mambo hakika na tarakimu usitie chumvi. Uwe mwangalifu usibadili maneno. Kwa mfano, usibadili “baadhi ya watu” kuwa “watu wengi,” “katika visa fulani” kuwa “nyakati zote,” na “huenda halikutokea” kuwa “haiwezekani lilitokea.”

  • Wasaidie wasikilizaji wafikirie uthibitisho huo. Baada ya kusoma andiko au rejeo fulani, waulize wasikilizaji maswali kwa busara au utoe mfano unaoonyesha jambo kuu ili kuwasaidia wasikilizaji wafikie mkataa.

KATIKA HUDUMA

Unapojitayarisha kuhubiri, tafakari ni maswali gani ambayo huenda ukaulizwa, kisha ufanye utafiti wa jinsi utakavyoyajibu. Mwenye nyumba akiuliza swali ambalo hujui jibu, mwombe ukafanye utafiti kisha urudi wakati mwingine.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki