SOMO LA 3
Kutumia Maswali
Mathayo 16:13-16
MUHTASARI: Uliza maswali kwa busara ili kuchochea na kudumisha upendezi, kujadiliana na wasikilizaji wako, na kukazia mambo muhimu.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Chochea na kudumisha upendezi. Uliza maswali yasiyohitaji majibu ambayo yatachochea udadisi wa msikilizaji wako na kumfanya afikiri.
Zungumzia habari kwa mfuatano mzuri. Wasaidie wasikilizaji wako wafuate mawazo kwa mpangilio fulani kwa kuuliza mfululizo wa maswali yanayowasaidia kufikia mkataa unaofaa.
Kazia mambo muhimu. Uliza swali lenye kuchochea ili kutokeza wazo kuu. Tumia maswali ya pitio baada ya kuzungumzia jambo muhimu au unapomalizia mazungumzo yako.