-
Ratiba ya Juma Linaloanza Septemba 28Huduma ya Ufalme—2015 | Septemba
-
-
Ratiba ya Juma Linaloanza Septemba 28
JUMA LINALOANZA SEPTEMBA 28
Wimbo 73 na Sala
Funzo la Biblia la Kutaniko:
cl sura ya 31 ¶1-12 (Dak. 30)
Shule ya Huduma ya Kitheokrasi:
Usomaji wa Biblia: 2 Wafalme 23-25 (Dak. 8)
Na. 1: 2 Wafalme 23:8-15 (Isizidi dak. 3)
Na. 2: Malaika Wana Majukumu Gani Katika Kusudi la Mungu? (Dak. 5)
Na. 3: Inamaanisha Nini Kuitendea Dhambi Roho Takatifu?—td 3D (Dak. 5)
Mkutano wa Utumishi:
Kichwa cha Mwezi Huu: ‘Toa ushahidi kamili kuhusu habari njema.’ —Mdo. 20:24.
Dak. 10: Paulo na Waandamani Wake Walihubiri kwa Bidii Huko Filipi. Mazungumzo. Waombe wasikilizaji wasome Mdo. 16:11-15. Zungumzia jinsi simulizi hili linavyoweza kutusaidia katika huduma yetu.
Dak. 20: “Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari Njema.” Maswali na majibu. Baada ya kuzungumzia fungu la 3, panga onyesho la mhubiri aliyejitayarisha vizuri akitoa broshua Habari Njema na kuzungumzia fungu moja.
Wimbo 114 na Sala
-
-
Kufundisha kwa Kutumia Broshua Habari NjemaHuduma ya Ufalme—2015 | Septemba
-
-
1. Ni nini kusudi la broshua Habari Njema?
1 Kama ilivyoelezwa katika makala ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Julai, broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu! ni mojawapo ya kifaa muhimu tunachotumia kufundishia. Maandiko yaliyoonyeshwa, hayajanukuliwa ili wanafunzi wafurahie kujifunza moja kwa moja kutoka kwenye Biblia. Ingawa machapisho yetu mengi yameandikwa kwa njia ambayo msomaji anaweza kujifunza mwenyewe, broshua hii imekusudiwa kutumiwa kwa njia ya mazungumzo yanayoongozwa na mwalimu. Kwa hiyo, tunapomwachia mwanafunzi broshua hiyo, tunapaswa kumwonyesha funzo linavyoongozwa ili aone jinsi kujifunza habari njema za Biblia kunavyosisimua.—Mt. 13:44.
-