Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 2
  • Biblia Inatupatia Tumaini

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Biblia Inatupatia Tumaini
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Biblia Inatupatia Tumaini
    Furahia Maisha Milele—Masomo ya Kwanza ya Biblia
  • Tumaini Bora la Wakati Ujao
    Habari Zaidi
  • Sababu za Kuwa na Tumaini Katika 2023—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
  • Kupata Tumaini Mwaka wa 2024​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zaidi
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 2
Somo la 2. Jua likichomoza juu ya shamba kubwa la ngano.

SOMO LA 02

Biblia Inatupatia Tumaini

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Watu ulimwenguni pote wanakabili matatizo yanayowafanya wawe na huzuni, wasiwasi, na hata maumivu. Je, umewahi kupatwa na hali iliyofanya uhisi hivyo? Labda unateseka kwa sababu ya ugonjwa au kwa sababu umefiwa na mtu unayempenda. Huenda unajiuliza, ‘Je, maisha yangu yatabadilika na kuwa mazuri?’ Biblia inajibu swali hilo kwa njia yenye kufariji.

1. Biblia inatupatia tumaini gani?

Biblia inaeleza sababu zinazofanya ulimwengu ujae matatizo, vilevile inatupatia habari njema kwamba matatizo haya ni ya muda mfupi na yatakwisha hivi karibuni. Ahadi za Biblia zinaweza kukupatia “wakati ujao na tumaini.” (Soma Yeremia 29:11, 12.) Ahadi hizo zinatusaidia kukabiliana na matatizo sasa, kuwa na mtazamo mzuri, na kupata furaha ya kudumu.

2. Biblia inaahidi nini kuhusu wakati ujao?

Biblia inaeleza kwamba wakati ujao “kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.” (Soma Ufunuo 21:4.) Matatizo yanayofanya tukate tamaa maishani leo, kama vile umaskini, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo, hayatakuwapo tena. Biblia inaahidi kwamba wanadamu watafurahia kuishi milele katika Paradiso duniani.

3. Unawezaje kuwa na hakika kwamba ahadi za Biblia zitatimia?

Watu wengi wangependa kuwa na maisha mazuri, lakini hawana hakika ikiwa matarajio yao yatatimia. Hata hivyo, ahadi zilizo katika Biblia zitatimia. Tunaweza kuwa na uhakika kuhusu ahadi hizo kwa ‘kuyachunguza Maandiko kwa uangalifu.’ (Matendo 17:11) Unapojifunza Biblia, utapata usadikisho ambao utakusaidia kuamini mambo ambayo Biblia inasema kuhusu wakati ujao.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza baadhi ya hali ambazo Biblia inaahidi kuhusu wakati ujao. Ona jinsi tumaini ambalo Biblia inatupatia linavyowasaidia watu leo.

Picha: Hali ambazo watu wanakabili leo na hali za wakati ujao ambazo Biblia inaahidi. Hali hizo zimeonyeshwa katika somo hili.

4. Biblia inatupatia tumaini la kuishi milele bila matatizo

Ona orodha ifuatayo ya ahadi zilizo katika Biblia. Ni ahadi gani ambazo unapenda zaidi? Kwa nini?

Soma maandiko yaliyoambatanishwa na ahadi hizi, kisha ufikirie maswali haya:

  • Je, maandiko haya yanakupatia tumaini? Je, yanaweza kuwapatia tumaini watu wa familia yako na marafiki?

Wazia ukiishi katika ulimwengu ambao

HAKUNA MTU AMBAYE . . .

KILA MTU . . .

  • atahisi maumivu, atadhoofika kwa sababu ya kuzeeka, au kufa.​—Isaya 25:8.

  • atawaona wapendwa wake wakifufuliwa, na kuishi duniani.​—Yohana 5:28, 29.

  • atapatwa na magonjwa au kuishi na ulemavu.​—Isaya 33:24; 35:5, 6.

  • atafurahia kuwa na afya nzuri na nguvu za ujana.​—Ayubu 33:25.

  • atatendewa bila haki.​—Isaya 32:16, 17.

  • atakuwa na chakula tele, makao mazuri, na kazi yenye kuridhisha.​—Zaburi 72:16; Isaya 65:21, 22.

  • atateseka kwa sababu ya vita.​—Zaburi 46:9.

  • atakuwa na amani kwa wingi.​—Zaburi 37:11.

  • atasumbuliwa na mawazo au kumbukumbu mbaya.​—Isaya 65:17.

  • ataishi milele katika hali bora.​—Zaburi 37:29.

Mvulana aliyekuwa mgonjwa amepona na anamkumbatia mama yake. Mwanamume aliyekuwa amezeeka sasa amebeba mzigo wa mazao. Watoto waliokuwa na njaa na waliofanya kazi ya kulazimishwa sasa wanafanya kazi shambani na kucheza mpira. Mwanamke aliyekuwa amejikunyata na kukata tamaa sasa amesimama akiwa anatabasamu.

5. Tumaini la Biblia linaweza kubadili maisha yako

Watu wengi huvunjika moyo au kukasirika kwa sababu ya matatizo wanayokabili. Wengine hujitahidi sana kuleta mabadiliko. Ona jinsi ahadi ya Biblia kwamba hali zitabadilika inavyowasaidia watu leo. Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie maswali haya:

VIDEO: Nilitaka Kupigania Haki (4:07)

Picha: Picha zilizo katika video ‘Nilitaka Kupigania Haki.’ 1. Rafika akivuna pamba akiwa pamoja na watu wa jamii yake alipokuwa msichana. 2. Rafika anafurahi kuona watu wa jamii mbalimbali wakiwa pamoja alipohudhuria kusanyiko la Mashahidi wa Yehova kwa mara ya kwanza.
  • Katika video hiyo, ni ukosefu gani wa haki ambao ulimhangaisha Rafika?

  • Ingawa ukosefu wa haki alioona haukwisha, Biblia ilimsaidiaje?

Biblia inatupatia tumaini la wakati ujao ambalo linatusaidia kuwa na furaha na kutovunjika moyo ingawa tuna matatizo. Soma Methali 17:22 na Waroma 12:12, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, unafikiri tumaini ambalo Biblia inatupatia linaweza kubadili maisha yako sasa? Kwa nini?

WATU FULANI HUSEMA: “Ahadi za Biblia kuhusu wakati ujao ni mambo ya kuwaziwa tu.”

  • Kwa nini unapaswa kuchunguza uthibitisho?

MUHTASARI

Biblia inatupatia tumaini zuri la wakati ujao ambalo hutusaidia kukabiliana na matatizo.

Ungejibuje?

  • Kwa nini watu wanahitaji tumaini?

  • Biblia inaahidi nini kuhusu wakati ujao?

  • Tumaini la wakati ujao linaweza kukusaidiaje sasa?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi tumaini linavyoweza kukusaidia kukabiliana na matatizo.

“Tumaini​—Je, Linaweza Kutusaidia?” (Amkeni!, Aprili 22, 2004)

Ona jinsi ambavyo tumaini la wakati ujao limewasaidia watu wenye magonjwa ya kudumu.

“Je, Biblia Inaweza Kunisaidia Ikiwa Nina Ugonjwa wa Kudumu?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Unapotazama video hii ya muziki, jiwazie wewe na familia yako mkifurahia maisha katika Paradiso ya wakati ujao iliyoahidiwa katika Biblia.

Wazia Maisha Paradiso (3:37)

Soma jinsi maisha ya mwanaharakati wa masuala ya kijamii yalivyobadilika alipojifunza kuhusu tumaini la wakati ujao ambalo linapatikana katika Biblia.

“Sitamani Tena Kuubadili Ulimwengu” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2013)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki