Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 17
  • Yesu Ana Sifa Gani?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yesu Ana Sifa Gani?
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Yesu Ni Nani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • ‘Mwana Anapenda Kumfunua Baba’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Yesu Kristo Ni Nani?
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Yesu Alifanya Nini Alipokuwa Duniani?
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 17
Somo la 17. Yesu ananyoosha mikono yake na kumponya kimuujiza mwanamume mgonjwa.

SOMO LA 17

Yesu Ana Sifa Gani?

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Tunapojifunza kuhusu mambo ambayo Yesu alisema na kufanya alipokuwa duniani, tunajifunza sifa ambazo zinatusaidia kumkaribia yeye na Yehova Baba yake. Baadhi ya sifa hizo zenye kuvutia ni zipi? Na tunawezaje kumwiga Yesu katika maisha yetu?

1. Yesu anafanana na Baba yake kwa njia gani?

Yesu akiwa mbinguni amemtazama Baba yake mwenye upendo na kujifunza kutoka kwake kwa mabilioni ya miaka. Na hivyo anafikiri, anahisi, na kutenda kama Baba yake. (Soma Yohana 5:19.) Yesu anaonyesha sifa za Baba yake kikamili hivi kwamba alisema: “Yeyote ambaye ameniona mimi amemwona Baba pia.” (Yohana 14:9) Unapojifunza kuhusu sifa za Yesu, utamjua Yehova vizuri zaidi. Kwa mfano, huruma ya Yesu kuelekea watu inaonyesha kwamba Yehova anakujali.

2. Yesu ameonyeshaje kwamba anampenda Yehova?

Yesu alisema: “Ili ulimwengu ujue kwamba ninampenda Baba, ninafanya kama vile Baba alivyoniamuru.” (Yohana 14:31) Alipokuwa duniani, Yesu alionyesha kwamba anampenda sana Baba yake kwa kumtii hata ilipokuwa vigumu kufanya hivyo. Pia, Yesu alipenda kuzungumza kumhusu Baba yake na kuwasaidia wengine wawe na urafiki wa karibu na Yehova.​—Yohana 14:23.

3. Yesu ameonyeshaje kwamba anawapenda watu?

Biblia inasema kwamba Yesu ‘anawapenda sana wanadamu.’ (Methali 8:31) Alionyesha kwamba anawapenda watu kwa kuwatia moyo na kuwasaidia bila ubinafsi. Alifanya miujiza iliyoonyesha kwamba ana nguvu na pia anawahurumia watu. (Marko 1:40-42) Aliwatendea watu kwa fadhili bila ubaguzi. Maneno yake yaliwafariji na kuwapatia tumaini watu wote wenye moyo mnyoofu waliomsikiliza. Yesu alikuwa tayari kuteseka na kufa kwa sababu aliwapenda wanadamu wote. Lakini anawapenda hasa wale wanaofuata mafundisho yake.​—Soma Yohana 15:13, 14.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze kuhusu sifa za Yesu. Na uchunguze jinsi unavyoweza kuiga upendo na ukarimu wake.

4. Yesu anampenda Baba yake

Yesu alituwekea mfano wa jinsi ya kuonyesha kwamba tunampenda Mungu. Soma Luka 6:12 na Yohana 15:10; 17:26. Baada ya kusoma kila andiko, zungumzieni swali hili:

  • Tunawezaje kumwiga Yesu na kuonyesha kwamba tunampenda Yehova?

Yesu akisali.

Yesu alimpenda Baba yake wa mbinguni na alizungumza naye mara nyingi kupitia sala

5. Yesu anawajali watu wenye uhitaji

Yesu alitanguliza mahitaji ya watu wengine. Hata alipokuwa amechoka alitumia wakati na nguvu zake kuwasaidia watu. Soma Marko 6:30-44, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Katika simulizi hili, Yesu alionyeshaje kwamba anawajali wengine?​—Ona mstari wa 31, 34, 41, na 42.

  • Ni nini kilichomchochea Yesu awasaidie watu?​—Ona mstari wa 34.

  • Kwa kuwa Yesu alionyesha sifa za Yehova, hilo linakufundisha nini kumhusu Yehova?

  • Unaweza kumwiga Yesu kwa njia gani ili uonyeshe kwamba unawajali wengine?

Yesu alisha kimuujiza maelfu ya watu kwa kutumia mikate mitano na samaki wawili wadogo. Nao wanafunzi wanagawa kwa wanaume, wanawake, na watoto.

6. Yesu ni mkarimu

Yesu alikuwa mkarimu ingawa hakuwa na vitu vingi vya kimwili, na alitutia moyo tuwe wakarimu. Soma Matendo 20:35, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kulingana na maneno hayo ya Yesu, tunawezaje kuwa na furaha?

Onyesha VIDEO, kisha mzungumzie swali linalofuata.

VIDEO: “Kuna Furaha Zaidi Katika Kutoa”​—Kisehemu (4:00)

  • Tunaweza kutoa katika njia zipi, hata ikiwa hatuna vitu vingi vya kimwili?

Je, wajua?

Biblia inatufundisha tusali kwa Yehova kupitia jina la Yesu. (Soma Yohana 16:23, 24.) Tunaposali kwa njia hiyo, tunaonyesha kwamba tunatambua jambo ambalo Yesu amefanya ili kutusaidia tuwe rafiki za Yehova.

WATU FULANI HUSEMA: “Mungu hajali tunapoteseka.”

  • Kwa kuwa Yesu alionyesha sifa za Baba yake, matendo yake yanathibitishaje kwamba Yehova anatujali?

MUHTASARI

Yesu anampenda Yehova, na pia anawapenda watu. Kwa kuwa Yesu anaonyesha sifa za Baba yake, unapozidi kumjua Yesu ndivyo utakavyozidi kumjua Yehova.

Ungejibuje?

  • Kama Yesu, tunawezaje kuonyesha kwamba tunampenda Yehova?

  • Kama Yesu, tunawezaje kuonyesha kwamba tunawapenda watu?

  • Ni sifa gani ya Yesu inayokuvutia zaidi?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Chunguza baadhi ya sifa za Yesu ambazo tunaweza kuiga.

“Mwige Yesu kwa Kusitawisha Sifa Zifuatazo . . .” (Yesu​—Njia, Kweli, na Uzima, ukurasa wa 317)

Jifunze kwa nini unapaswa kusali kupitia jina la Yesu.

“Kwa Nini Tusali Katika Jina la Yesu?” (Mnara wa Mlinzi, Februari 1, 2008)

Je, Biblia ina habari zozote kuhusu sura ya Yesu?

“Yesu Alikuwa na Sura ya Aina Gani?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Tunajifunza nini kutokana na jinsi Yesu alivyowatendea wanawake?

“Heshima na Staha Chini ya Utunzaji wa Mungu” (Mnara wa Mlinzi, Septemba 1, 2012)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki