Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 58
  • Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Kukabili Mtihani wa Uaminifu-Mshikamanifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1996
  • Jinsi Dini za Uwongo Zinavyopotosha Ukweli Kumhusu Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • “Wewe Peke Yako Ni Mwaminifu-Mshikamanifu”
    Mkaribie Yehova
  • Epuka Ibada ya Uwongo!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 58
Somo la 58. Familia ikipita karibu na kikundi cha waasi-imani wanaowadhihaki watu wanaowasili kwenye kusanyiko la Mashahidi wa Yehova.

SOMO LA 58

Endelea Kuwa Mshikamanifu kwa Yehova

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Wakristo wa kweli wameazimia kwamba hawataruhusu kamwe kitu au mtu yeyote aharibu uhusiano wao na Yehova. Tuna hakika wewe pia unahisi hivyo. Yehova anathamini ushikamanifu wako. (Soma 1 Mambo ya Nyakati 28:9.) Ni hali gani zinazoweza kufanya iwe vigumu kwako kuendelea kuwa mshikamanifu kwa Yehova, na ni nini kinachoweza kukusaidia?

1. Wengine wanawezaje kufanya iwe vigumu kwetu kuendelea kuwa washikamanifu kwa Yehova?

Watu fulani watajaribu kutushawishi tuache kumtumikia Yehova. Je, kuna watu wanaoweza kufanya jambo baya hivyo? Baadhi ya watu ambao wameacha kumtumikia Yehova, wanaeneza uwongo kuhusu tengenezo la Mungu ili kuharibu imani yetu. Watu hao wanaitwa waasi-imani. Pia, baadhi ya viongozi wa dini hueneza uwongo kutuhusu ili kuwafanya watu wasio waangalifu waache kumtumikia Yehova. Ni hatari kubishana na watu wanaotupinga, kusoma vitabu na mijadala yao kwenye mitandao, kutembelea tovuti zao, au kutazama video zao. Yesu alisema hivi kuhusu wale wanaojaribu kuwavunja moyo wengine waache kuwa washikamanifu kwa Yehova: “Waacheni. Wao ni viongozi vipofu. Basi, kipofu akimwongoza kipofu, wote wawili watatumbukia ndani ya shimo.”—Mathayo 15:14.

2. Ni maamuzi gani yanayoweza kuonyesha kwamba sisi ni washikamanifu kwa Yehova?

Upendo wetu kwa Yehova utatuchochea kuepuka kushirikiana kwa njia yoyote na dini za uwongo. Hatupaswi kufanya kazi au kushirikiana na shirika lolote la kidini wala kujihusisha na shughuli zozote zinazohusiana na dini za uwongo. Yehova anatuonya hivi: “Tokeni [katika Babiloni Mkubwa], watu wangu.”—Ufunuo 18:2, 4.

CHIMBA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyoweza kuepuka kumruhusu mtu yeyote avunje ushikamanifu wako kwa Yehova. Pia, chunguza jinsi unavyoweza kuonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa kujitenga na Babiloni Mkubwa.

3. Jihadhari na walimu wa uwongo

Tunapaswa kutendaje tunaposikia habari zisizofaa kuhusu tengenezo la Yehova? Soma Methali 14:15, kisha mzungumzie swali hili:

  • Kwa nini hatupaswi kuwa wepesi kuamini kila jambo tunalosikia?

Soma 2 Yohana 9-11, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Tunapaswa kuwatendeaje waasi-imani?

  • Mbali na kuepuka kushirikiana na waasi-imani moja kwa moja, ni mambo gani mengine tunayopaswa kuepuka ili tusishawishiwe na mafundisho yao?

  • Unafikiri Yehova atahisije ikiwa tutasikiliza mambo yasiyofaa yanayosemwa kumhusu au kuhusu tengenezo lake?

4. Uwe mshikamanifu kwa Mungu, Mkristo mwenzako anapotenda dhambi

Unapotambua kwamba mtu fulani kutanikoni amefanya dhambi nzito, unapaswa kuchukua hatua gani? Fikiria kanuni iliyo katika Sheria ambayo Mungu aliwapa Waisraeli wa kale. Soma Mambo ya Walawi 5:1.

Kulingana na mstari huo, tunapotambua kwamba mtu fulani amefanya dhambi nzito, tunapaswa kuwaambia wazee habari tunazojua. Hata hivyo, kabla ya kuchukua hatua hiyo, ni jambo la fadhili kumhimiza mtu huyo aende kwa wazee na kuungama dhambi yake. Asipofanya hivyo, ushikamanifu wetu kwa Yehova utatuchochea kuwaambia wazee habari tunazojua. Kuchukua hatua hizo kunaonyeshaje upendo mshikamanifu kwa . . .

  • Yehova Mungu?

  • mtu aliyetenda dhambi?

  • watu wengine kutanikoni?

Picha: Ndugu anamsaidia ndugu mwingine ambaye amefanya kosa. 1. Ndugu huyo anaona jambo lisilofaa kwenye simu yake. 2. Ndugu huyo anamwonyesha simu yule ndugu mwingine, lakini ndugu huyo hakubaliani naye. 3. Yule ndugu mwingine anawaonyesha wazee wawili simu yake na kuzungumza nao.

Ikiwa Mkristo mwenzako yuko hatarini, msaidie!

5. Jitenge na Babiloni Mkubwa

Onyesha VIDEO.

VIDEO: Tokeni Katika Babiloni Mkubwa!

Picha ya video ‘Tokeni Katika Babiloni Mkubwa!’ Mwanafunzi wa Biblia akiondoka kwenye meza ya kasisi baada ya kuacha kazi kanisani.

Soma Luka 4:8 na Ufunuo 18:4, 5, kisha ujibu maswali haya:

  • Je, bado jina langu limeandikwa kwenye orodha ya wafuasi wa dini ya uwongo?

  • Je, ninashirikiana na shirika linalohusiana na dini nyingine?

  • Je, kazi yangu inaunga mkono dini ya uwongo kwa njia yoyote?

  • Je, kuna hatua nyingine ambayo ninahitaji kuchukua ili kujitenga na dini ya uwongo?

  • Ikiwa nimejibu ndiyo kwa mojawapo ya maswali hayo, ninapaswa kufanya mabadiliko gani?

Katika visa hivyo vyote, fanya uamuzi utakaokuacha ukiwa na dhamiri safi na utakaoonyesha kwamba wewe ni mshikamanifu kwa Yehova.

Dada na mwanawe wakitoka dukani. Wanapita kando ya mwanamke anayekusanya michango kwa ajili shirika la kidini.

Utafanya nini ukiombwa utoe mchango wa kusaidia mashirika ya kidini?

WATU FULANI HUSEMA: “Ninahitaji kujua mambo ambayo waasi-imani wanasema kuhusu Mashahidi wa Yehova ili nitetee ukweli.”

  • Je, hilo ni jambo la hekima? Kwa nini?

MUHTASARI

Ili tuendelee kuwa washikamanifu kwa Yehova, tunapaswa kuepuka kushirikiana na watu wanaotaka kutupotosha.

Ungejibuje?

  • Kwa nini hatupaswi kusikiliza habari za waasi-imani?

  • Tunapaswa kufanya nini tukijua kwamba ndugu au dada ametenda dhambi nzito?

  • Tunawezaje kutii agizo la kutoka kwenye dini za uwongo?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Jifunze jinsi unavyopaswa kutenda unaposikia habari za uwongo kuhusu Mashahidi wa Yehova.

“Je, Una Habari Kamili?” (Mnara wa Mlinzi, Agosti 2018)

Unawezaje kutambua mashirika au shughuli zinazounga mkono Babiloni Mkubwa?

“Uwe na Mengi ya Kufanya Katika Kipindi cha Mwisho cha ‘Siku za Mwisho’” (Mnara wa Mlinzi, Oktoba 2019, fungu la 16-18)

Baadhi ya wapinzani wamefanya nini ili kujaribu kudhoofisha imani yetu?

Jihadhari na Udanganyifu (9:32)

Katika simulizi “Nimekuwa Nikimtafuta Mungu Tangu Utotoni,” soma kuhusu kuhani wa dini ya Shinto aliyeacha kushirikiana na dini ya uwongo.

“Biblia Inabadili Maisha” (Mnara wa Mlinzi, Julai 1, 2011)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki